Kwanini Mchungaji/Askofu/Mwinjilisti anapoingia kwenye siasa za Vyama vingi Mungu anamfuta siku hiyo hiyo katika utume?

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Siku Paulo anaitwa kuwa mpleka injili Mungu alimtambulisha kwa anania kama "CHOMBO CHANGU KITEULE NILICHOKICHAGUA ILI APATE KULICHUKUA JINA LANGU KWA MATAIFA NA WAFALME" Matendo 9:15

Pia ukisoma Isaya 49, Utagundua MTUMISHI wa Mungu ni cheo kikubwa kuliko wafalme na marais. Anasema hapo wafalme,wake zao, wenye vyeo We we ndiye utakuwa mlezi wao, Watakuja kukusujudia (kukuangukia kuomba msaada wa kiroho)

Kwanini Mungu anakata utumishi wako papo hapo unapoonyesha nia ya kuwa mwanasiasa vyama vingi.

1: Wewe ni chombo chake.ukiingia kwenye vyama vingi sio tena chombo cha Mungu Bali chombo kinachoongozwa na katiba za chama na ilani na maamuzi yao.

2: Ushawishi uliopewa ni ili watu wamjue Mungu kupitia sio wakujue wewe kupitia Mungu.

3: Vyama pinzani na hasimu vitapelekea we we ugawanye waumini kwa Misingi ya siasa badala ya kuwagawa kwa misingi ya Utakatifu na Udhambi wao ili wadhambi wasaidiwe.

4: Umepewa kondoo uwachunge, Siku ile Utaulizwa "liko wapi kundi lile nililoliweka mikononi mwako?" Utakuwa umelitapanya kwa Uccm wako au uchadema wako

5: Mungu atakukata katika teuzi zake maana sio lazima uwe tu, anao watu lukuki kwenye queue wanalilia kutumikia kwa dhamiri isiyoghoshiwa.

Mwisho wakati wa Yesu miaka 2000 iliyopita kulikuwa na harakati nyingi sana za kisiasa. Zilikuwa Kali kiasi hata wafuasi wake walimfanya na yeye kama mgombea wa kuwatoa warumi uyahudi. Zaidi ya kuwakemea Yesu hakuwahi kutoa kauli yoyote kuunga au kupinga harakati za kisiasa zaidi ya Kuwatoa watu kuangalia serikali za dunia waangalie serikali ya Mbinguni ambayo haina Wizi, Rushwa,Kujipendekeza,upendeleo, hakuna hospital, hakuna shida. Inamambo ambayo Macho hayajawahi kuona wala sikio haijawahi kusikia.

Kuacha Utumishi na kujihusisha na siasa za vyama vingi au kufanya vyote ni ushahidi kwa kuikana madhabahu takatifu na kuchagua kuwa mtumwa wa mimbari na madhabahu ziharibikazo za wanasiasa.

Usiwe mfuasi wa Mungu kupitia watu hawa maana Mungu hayuko upande wao.

Usiogope kumkemea waziwazi na kumshauri achague moja kuliko kuwa vuguvugu maana atatapikwa.
 
Mkuu, unamjua Daniel aliyekuwa anafanya kazi za kisiasa kwenye Ikulu ya Nebukandreza kule Babeli? Hakuwa mtumishi wa Mungu yule? Je, kuna sehemu kwenye Biblia inamkataza mtumishi wa Mungu kufanya kazi ya kisiasa? Acha kupotosha basi ndugu yangu.
 
mitale na midimu kwanza habari ya siku mkuu?

Twende kwenye bandiko lako ambalo sijui unamuongelea nani hapa, tafadhali kama umeandika kutokana na Josephat please rudi ukatubu.

Aina hii ya Josephat wao muda wa kuliongoza lile kusanyiko lake umekwisha na ndiyo safari inaanza kufikia mwisho, nk.

Kama ni viongozi wanaofahamika tunaweza kuanza mjadala ...
 
Hi

Hizo propanganda mkuu, muache bishop apige kazi. Au unamuogopa mkuu?
maneno haya hayamzuii mtu yoyote kutimiza alichoazimia moyoni mwake vinginevyo labda shetani yuko Likizo.

Kuhusu mgombea ANAYEJIITA BISHOP simuogopi mkuu maana tayari ameshapoteza sifa ya kusikilizwa kwa sababu katika Bibilia mtu kama huyo anaitwa LAODEKIA(Kigeugeu si moto wala Vugu vugu).

Mfano
Leo; Siwezi kugombea Ubunge kwa sababu ni cheo kidogo kuliko alichonipa Mungu, Kesho "Nipeni kula zenu niwe mbunge wenu".

Mtu kama huyu anakidhi viwango vya kusikilizwa kama mwanasiasa sio kama mtumishi wa Serikali ya Mungu.
 
Mkuu, unamjua Daniel aliyekuwa anafanya kazi za kisiasa kwenye Ikulu ya Nebukandreza kule Babeli? Hakuwa mtumishi wa Mungu yule? Je, kuna sehemu kwenye Biblia inamkataza mtumishi wa Mungu kufanya kazi ya kisiasa? Acha kupotosha basi ndugu yangu.
Daniel usimchanganye mkuu.
Daniel alikuwa ni raia tu wa Ufalme wa Yuda, mzao wa kifalme sio KIONGOZI WA DINI, AU MTEULE SIKU ANAINGIA BABELI.
Viongozi wa Kiroho waliokuwepo wakati daniel Yuko hai ni Nabii Yeremia (ktk nchi ya Yuda), NAbii Ezekiel (na Yeye alikuwa huko utumwani Babeli). Na watumishi wa hekalu MAKUHANI na UZAO WAO walikuwepo. HAwaonekani katika sehemu yoyote ya kisiasa.

Pia
Daniel hakuingia katika Siasa za UShindani. Yeye na Wenzake Waliishi maisha yao Ya kiroho na Kuonekana wanaakili kubwa kuliko mtu yoyote. Waliteuliwa katika Teuzi za NEBUKADNEZA HAwakugombania wala kushindana na mtu. Pia WALIPOTEULIWA HAWAKUONGOZWA NA MATAKWA YA manifesto za kibabeli au MEDOPERSIA. Wao waliishi kanuni za Serikali ya Mbinguni hata walipotakiwa kufa ispokuwa wamezikana Walikuwa tayari. LAkini utumishi Bora wa Daniel kwa misingi ya serikali za Mbinguni kwa Serikali za duniani, KWa uaminifu wa kiwango kisicho cha dunia hii, ALiteuliwa kuwa MKUU WA WACHAWI, WASOMI, WAGANGA na KILA MTU YOYOTE WA KIROHO KATIKA DUNIA ILE. Maana yake ni nini? Syrabuss zote za kichawi na kishirikina ilibidi zipigwe chini na zile walizokuwa wanasoma wakina daniel Yaani Biblia ndio iwe mitaala kwa kila mtu.
NDio Maana hata wakati wa Yesu, Wale MAJUSI (Magicians) wachawi wa kibabeli kwa kusoma tabiri za Vitabu vya Kiyahudi walijua YESU KAZALIWA HUKU VIONGOZI WA KIDINI WALIOJICHANGANYA KWENYE SIASA WAKIBAKI HAWANA KITU WANABUNG'AA TU WAKISHIRIKIANA NA SERIKALI KUMUUA Yesu.

Kuna kitu katika bibilia kinatitwa "CONSECRATION". Hii ni kukitenga kitu au mtu wakfu kwa ajili ya matumizi maalumi tu na sio vinginevyo. Tunaamini wachungaji,wainjilisti na maaskofu wote wametengwa wakfu maalum kwa kazi moja tu. Kulea na kukuza Kundi la Kristo na hawafungwi na mipaka ya kijiografia wao utume wao ni dunia nzima sio jimbo, nchi wala mkoa bali popote Mungu atakapotraka waende watatumika.


KWA SIFA HIZO TU MTU KUTUMWA NA KIKUNDI CHA WATU FLANI WENYE CHAMA FLANI ILI AWE MUAKWAKILISHI WA KAKIKUNDI KA WATU, TENA HUKU ANAPINGANA NA WENGINE KWA MISINGI YA KIITIKADI NA SIO BIBILIA ANAYOIAMINI NI KUUKANA NA KUUNAJISI UTUME ALIOITIWA.

MWISHO
KAtika zamani hizi za ROHO MTAKATIFU (Holy spirit Dispensation ). Tangu zamani za |Yohana mbatizaji hadi Yesu anakuja hakuna mtumishi wa Mungu ambaye atajihusisha na siasa na serikali za dunia hii na kubaki kuwa mtuymishi wa Serikali ya Mbinguni. Kazi yao ni SALA NA DUA KWA SERIKALI NA VIONGOZI ILI WATAWALE KWA HAKI NA AMANI ILI IPATIKANE NAFASI YA KUPELEKA NENO.
 
Kwani mnamsema nani alikuwa akifanya kazi ya Mungu?
Angalieni msije mkasema matapeli flani ni watumishi wa Mungu.
Itakuwa kufuru nawaapia, wale ni wasanii na ndio wale waliotajwa ktk maandiko.
mkuu hii ni general formula ambayo ni kipimo cha matapeli na wale halali ambao uroho wa kutaka madaraka serikali za dunia na Vyama vya kisiasa unawanyemelea.

Hao feki hawaendi mbali, Vikombe vyao vikijaa Mungu atawaondoa. Ni subira tu.
" Waovu wastawipo ni kwa ajili ya Uangamivu wao wenyewe"
 
mitale na midimu kwanza habari ya siku mkuu?

Twende kwenye bandiko lako ambalo sijui unamuongelea nani hapa, tafadhali kama umeandika kutokana na Josephat please rudi ukatubu.

Aina hii ya Josephat wao muda wa kuliongoza lile kusanyiko lake umekwisha na ndiyo safari inaanza kufikia mwisho, nk.

Kama ni viongozi wanaofahamika tunaweza kuanza mjadala ...
Asante kwa angalizo mkuu. Mimi nipo tu nafuatilia ingawa Jukwaa letu la Mabo ya kiroho naona sina access ya kukoment tena wenda mijadala kule imeonekana inahatarisha hisia za watu za kiimani na utulivu wa mwmbers na wafuatiliaji.

Mkuu nilidhani na yeye inamuhusu lakini kwa tahadhari yako natubu mkuu. hahaha
 
Back
Top Bottom