Kwanini mbunge Musukuma anapenda kuwadharau wasomi wetu?

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Nimesikiliza kwa makini wakati mbunge Musukuma akichangia leo bungeni, moja alikua akichangia kuhusu bajeti na kuwaita wataalamu wetu wa uchumi kua wataaalamu uchwara, hasa akitetea kuhusu wamachinga na kuondolewa barabarani hasa Kariakoo.

Hali iliopelekea Naibu Spika kumtaka aondoe neno hilo. Hivi kwanini mheshimiwa mbunge Musukuma kila akichangia anakua akiwasigina wasomi na kuwatukuza darasa la saba?

Hii inatokana na kutojiamini kwa kukosa elimu au kuna nini kafanyiwa na wasomi hadi chuki yake kufikia kiwango cha juu?

Au ndio kutaka kuwawini wananchi wengi ambao hawana elimu?
 
Inferiority complex tu zinamsumbua. anaona kabisa next round wasomi wata dominate hizo nafasi. ndio maana anajarib kuwashusha hadhi ili waonekane hawana maana.

lakin pia wasomi wetu lazima wajitafakari. they used to be the smart lakin leo wanapelekwa na upepo wa siasa. hali inayopelekea waonekane usomi wao hauwasaidii.
 
nimesikiliza kwa makini wakati mbunge msukuma akichangia leo bungeni, moja alikua akichangia kuhusu bajeti na kuwaita wataalamu wetu wa uchumi kua wataaalamu uchwara. hasa akitetea kuhusu wamachinga na kuondolewa barabarani hasa kariakoo....
Mara nyingi, unapokua mlemavu na ukakosa elimu huwa kila utakalotendewa utahisi unaonewa, sawa na mtoto yatima, ukiishi nae mara nyingi kila utakalofanya atahisi unamuonea, kuhusu Msukuma nadhani anapoona elimu yake ndogo na anapata kila atakacho, na kuna wasomi wanamlilia shida kila siku lazima ataona kupata pesa ni ujanja wake na elimu haina faida.
 
Wasomi wa makaratasi ni mzigo kwa taifa

Wasomi walio soma na kuelimika ni faida kwa taifa na niwachache sana na hawapati nafasi kwenye vikao vya maamuzi

Mtu anae itwa msomi lazima aonekane amefanya kitu zaidi ya yule anae mwona hajasoma

Wasomi wanajidharau wenyewe kwa kulete mambo ambayo hayana faida kwa watanzania
 
Nchi hii hakuna wasomi. Msukuma yuko sahihi kabisa

Wasomi ndiyo wanapiga kelele kuilalamikia serikali juu ya ukosefu wa ajira. Tulitegemea wao ndiyo watatuzi wa tatizo hili badala yake wao ndiyo wanalikuza.

Bibi yangu maisha yake yote anaishi kwa kupambana na ametulea. Hawa wasomi uchwara hawana jipya mtaani
 
Nimesikiliza kwa makini wakati mbunge Musukuma akichangia leo bungeni, moja alikua akichangia kuhusu bajeti na kuwaita wataalamu wetu wa uchumi kua wataaalamu uchwara, hasa akitetea kuhusu wamachinga na kuondolewa barabarani hasa Kariakoo.

Hali iliopelekea Naibu Spika kumtaka aondoe neno hilo. Hivi kwanini mheshimiwa mbunge Musukuma kila akichangia anakua akiwasigina wasomi na kuwatukuza darasa la saba?

Hii inatokana na kutojiamini kwa kukosa elimu au kuna nini kafanyiwa na wasomi hadi chuki yake kufikia kiwango cha juu?

Au ndio kutaka kuwawini wananchi wengi ambao hawana elimu?
Haina majibu hiyo.
Wenye akili wote hawabishani nae.
That will make them come down to his level. Mambo yanaendekea kila mtu anashiba
 
Ni psychological toture hiyo / hata me imewahi kunipata nilipokuwa sina degree
Nimesikiliza kwa makini wakati mbunge Musukuma akichangia leo bungeni, moja alikua akichangia kuhusu bajeti na kuwaita wataalamu wetu wa uchumi kua wataaalamu uchwara, hasa akitetea kuhusu wamachinga na kuondolewa barabarani hasa Kariakoo.

Hali iliopelekea Naibu Spika kumtaka aondoe neno hilo. Hivi kwanini mheshimiwa mbunge Musukuma kila akichangia anakua akiwasigina wasomi na kuwatukuza darasa la saba?

Hii inatokana na kutojiamini kwa kukosa elimu au kuna nini kafanyiwa na wasomi hadi chuki yake kufikia kiwango cha juu?

Au ndio kutaka kuwawini wananchi wengi ambao hawana elimu?
 
Nimesikiliza kwa makini wakati mbunge Musukuma akichangia leo bungeni, moja alikua akichangia kuhusu bajeti na kuwaita wataalamu wetu wa uchumi kua wataaalamu uchwara, hasa akitetea kuhusu wamachinga na kuondolewa barabarani hasa Kariakoo.

Hali iliopelekea Naibu Spika kumtaka aondoe neno hilo. Hivi kwanini mheshimiwa mbunge Musukuma kila akichangia anakua akiwasigina wasomi na kuwatukuza darasa la saba?

Hii inatokana na kutojiamini kwa kukosa elimu au kuna nini kafanyiwa na wasomi hadi chuki yake kufikia kiwango cha juu?

Au ndio kutaka kuwawini wananchi wengi ambao hawana elimu?
Kwa sababu anaamini ana pesa, ila ni mjinga tu kama wajinga wengine
 
Nchi hii hakuna wasomi. Msukuma yuko sahihi kabisa

Wasomi ndiyo wanapiga kelele kuilalamikia serikali juu ya ukosefu wa ajira. Tulitegemea wao ndiyo watatuzi wa tatizo hili badala yake wao ndiyo wanalikuza.

Bibi yangu maisha yake yote anaishi kwa kupambana na ametulea. Hawa wasomi uchwara hawana jipya mtaani
Kabisa!. Fikiria msomi kama Lisu anaamisha watu kwamba yeye akichaguliwa kuwa rais ndio tatizo la ajira litaisha wakati bibi yako kapambana bila hata Lisu kuwa mwenyekiti wake wa kitongoji na amewasomesha!
 
Kabisa!. Fikiria msomi kama Lisu anaamisha watu kwamba yeye akichaguliwa kuwa rais ndio tatizo la ajira litaisha wakati bibi yako kapambana bila hata Lisu kuwa mwenyekiti wake wa kitongoji na amewasomesha!
Hahaha! Mkuu imenibidi nicheke tu, maana umenitukana kifasihi. Asante kwa mitusi.
 
Anahasira maana huenda elimu ilimkataa either kwa hali ya maisha yao yakipindi hicho au hali ya huko upstairs
 
kwasababu hajasoma.
pia mtizamo wake na machinga havitofautiani huwezi ruhusu machinga wawe kila mahali hasa kwenye miji mikubwa , hao machinga anaowatetea mbona wametengewa maeneo yao na hawayatakiii yani inatakiwa bwana Makala akaze uzi wakeee ni kuwa hawafukuzwi ila wanatakiwa kuwa sehemu nzuri iliyo pangika
 
Hivi kwanini mheshimiwa mbunge Musukuma kila akichangia anakua akiwasigina wasomi na kuwatukuza darasa la saba?
Inasemekana Msukuma ametoboa maisha kwa njia ya wizi (utekaji wa mabasi) na uporaji. Yadaiwa walikuwa wanalindwa na mitambo asilia (ndumba) ili wasikamatwe.

Karibu kila mtu jimboni kwake anaijua hii historia chafu ya msukuma. Juzi nilikuwa huko nikapewa ubuyu huu.
 
Nchi hii hakuna wasomi. Msukuma yuko sahihi kabisa

Wasomi ndiyo wanapiga kelele kuilalamikia serikali juu ya ukosefu wa ajira. Tulitegemea wao ndiyo watatuzi wa tatizo hili badala yake wao ndiyo wanalikuza.

Bibi yangu maisha yake yote anaishi kwa kupambana na ametulea. Hawa wasomi uchwara hawana jipya mtaani
Kwahiyo utatuzi wa suala la ajira ni kutokuwa msomi ???
 
Namkubali msukuma,anatumia udhaifu wa wasomi the way wanavyokuwa wanaharakati Bungeni.
Wasomi tujitafakari.
Tembo wapo wengi na nyumbu hadi wanaua watu.
Leo unaongeza kodi kwenye laini,so uuze baadhi ya wanyama ambao Mungu anawalisha.
Jina la msukuma ni maarufu kupitia ujinga wabaadhi ya watu
 
Back
Top Bottom