Mpira wa kona
JF-Expert Member
- Nov 25, 2016
- 350
- 338
Nilitegemea suala la Jeshi la Magereza kule Ukonga ambalo Mh.Rais Magufuli alilishughulikia lilikuwa la Waziri wa Mambo ya ndani.Kutokana Na Kuril is hug bulimia niliamini Waziri husika Angejiuzulu lakini hajafanya hivyo.Juzi Waziri Mkuu amelianzisha la Kifaru John Kyle Arusha suala ambalo lilitakiwa ligunduliwe Na Waziri husika lakini hakuligundua.Kutokana Na hayo Matukio mazito kugunduliwa Na Mh.Rais Na Waziri Mkuu ni dhahiri Mawaziri hao wameshindwa kuwajibika ndio maana matukio hayo yametokea bila wao kujua.Nashauri dhana ya Utawala wa kuwajibika Wangejiuzulu Kwa hiari yao ili kuonyesha uwajibikaji.Mbona Mzee Mwinyi aliwahi kujiuzulu Kwa makosa ya watendaji wa chini yake?Mbona Mh.Waziri MKUU Mstaafu Edward Lowassa alijiuzulu Kwa makosa ya mawaziri? Mh.Mwigulu Na Mh.Maghembe Jipimeni.