Kwanini Matajiri, wanasiasa na watu mashuhuri huwa hawaanguki mapepo makanisani?

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,521
15,147
Kuna tuhumu (sina uhakika labda ni wivu tu) kuwa matajiri wengi/wanasiasa/watu mashuhuri wengi afrika hutumia nguvu za kiganga na kishirikina kujizatiti.

Ila jambo la ajabu tabaka hili la watu, kama ilivyokuwa enzi za masinagogi hukaa viti vya mbele karibu na mtume na nabii mpunga pepo. Kwa ajabu zaidi huwezi kuona hawa wakuu hata mmoja wapo anagaragara chini kwa kuangushwa na mapepo.

Maswali

Je mapepo yanaheshimu vyeo vya watu?
Je kuna mapepo ya kitajiri na ya kimasikini?
Je wanajiamini kwa sababu wanajua mitume wengi ni feki?
Je matajiri, watu mashuhuri na wanasiasa ni watu watakatifu sana wasioweza kusumbuliwa na vipepo?

wazoefu wa mambo ya kipepo karibuni mtoe mitiririsho yenu hapa.
 
Kuna tuhumu (sina uhakika labda ni wivu tu) kuwa matajiri wengi/wanasiasa/watu mashuhuri wengi afrika hutumia nguvu za kiganga na kishirikina kujizatiti.

Ila jambo la ajabu tabaka hili la watu, kama ilivyokuwa enzi za masinagogi hukaa viti vya mbele karibu na mtume na nabii mpunga pepo. Kwa ajabu zaidi huwezi kuona hawa wakuu hata mmoja wapo anagaragara chini kwa kuangushwa na mapepo.

Maswali

Je mapepo yanaheshimu vyeo vya watu?
Je kuna mapepo ya kitajiri na ya kimasikini?
Je wanajiamini kwa sababu wanajua mitume wengi ni feki?
Je matajiri, watu mashuhuri na wanasiasa ni watu watakatifu sana wasioweza kusumbuliwa na vipepo?

wazoefu wa mambo ya kipepo karibuni mtoe mitiririsho yenu hapa.
Hii labda Bro Mshana Jr atatupatia majibu !
 
Ongezea na Manabii alafu jiulize tena hili swali
''the law of attraction''.
Kwa hiyo unatakakuniaminisha vile huwa ni vilinge vya kishirikina mkuu.
wacha Mungu ndio wanaanguka mapepo, ila wengine wote lao moja au?
 
Wanaenda makanisa yenye upako?? Umewahi kwenda ecg?? Umewahi kwenda Christ Embasy?? Umewahi kwenda good news?? Fuatilia hayo makanisa utaona wanaanguka kama kawa
mkuu mvizie basi hata mbunge au waziri mmoja akitoa udenda na kupiga mayowe madhabahuni huku mtume na nabii akipunga hilo pepo.

Ingekuwa hivyo kwa wanavyopenda sifa na heshima wale jamaa watakuwa ni mabackbencher maana mbele kwenye ccamera patawashushua hadhi kwenye jamii.

au kuwe na chumba private cha kuwatolea pepo sio kwenye camwra
 
sio matajiri tu, kuna kundi lingine la watu ambao huwezi kuona hata siku moja wakiangushwa na mapepo kwenye makanisa ya kilokole haya ya kisasa.

kundi hili ni la wapiga picha, hapa nazungumzia wale camera operators wanao shoot ibada ikiwa live kwenye television.

hawa jamaa hata siku moja huwezi kuona wakiangushwa na mapepo mchungaji wa kanisa husika anapoomba, wao wapo busy tu na camera zao. huwa najiuliza, kundi hili ni watakatifu sana?.

na tukija katika maisha halisi ya kazi za media, hakuna watu walevi na mafuska kama wapiga picha wa television. hawa jamaa mimi nafanya nao kazi kwenye sector moja, nawafahamu sana. ni watu wa bata sana.
 
sio matajiri tu, kuna kundi lingine la watu ambao huwezi kuona hata siku moja wakiangushwa na mapepo kwenye makanisa ya kilokole haya ya kisasa.

kundi hili ni la wapiga picha, hapa nazungumzia wale camera operators wanao shoot ibada ikiwa live kwenye television.

hawa jamaa hata siku moja huwezi kuona wakiangushwa na mapepo mchungaji wa kanisa husika anapoomba, wao wapo busy tu na camera zao. huwa najiuliza, kundi hili ni watakatifu sana?.

na tukija katika maisha halisi ya kazi za media, hakuna watu walevi na mafuska kama wapiga picha wa television. hawa jamaa mimi nafanya nao kazi kwenye sector moja, nawafahamu sana. ni watu wa bata sana.
pia nasikia hivi vijamaa huwa vinatuhuma za uzinzi sana. Labda jini mahaba huwa linavaa Bulletproof
 
Labda huwa wanajitakasa kabla ya kuingia kwenye huduma. Maana hawa ni team moja na mtume na nabii. siku wakianguka basi na nabii naye lazima alambe sakafu. sijui nani atatuliza hiyo ghasia.
 
shetani hafai aisee. anapiga suti ya kondoo anajichanganya zizini kwa jina la Yesu.
 
Back
Top Bottom