Kwanini mashine za EFD zijae? Si ni unyonyaji mwingine

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,152
10,862
Hizi mashine eti zinajaa na ikitokea hivyo unanunua kwa bei ile ile ya karibu ya milioni.

Ajabu ni kuwa mashine hizi zinazotumiwa na TRA kukusanyia kodi haziendi hata miaka 3 kujaa kwake na hasa ukiwa ni mlipa kodi mzuri unayetoa risiti kwa kila mauzo.

Inakuwaje mashine hizi zikijaa zisifutwe tu kile kilichojaa kama hakitakiwi tena na mlipa kodi akaendelea na mashine yake.

Au kwanini kusiwe ni kifaa cha pesa ndogo kubadilishwa na mashine kuendelea kutumika.

Kwanini tumeruhusu teknolojia ya kinyonyaji na kuongeza uzito wa biashara.Na kwanini tuendekeze matakwa ya makampuni ya kinyonyaji badala ya wao kufuata masharti yetu katika kutuuzia vifaa vyao.

Ukiondoa huko kujaa kwa mashine pia mashine zenyewe hazikawii kuharibika na kosa lolote wasambazaji wanataka pesa tele kuiangalia.

Vipi TRA hawaoni kuharibika mara kwa mara kwa vifaa hivi vinachangia kupunguza kodi na kwamba ni mzigo kwa mlipa kodi.
 
Hizi mashine eti zinajaa na ikitokea hivyo unanunua kwa bei ile ile ya karibu ya milioni.

Ajabu ni kuwa mashine hizi zinazotumiwa na TRA kukusanyia kodi haziendi hata miaka 3 kujaa kwake na hasa ukiwa ni mlipa kodi mzuri unayetoa risiti kwa kila mauzo.

Inakuwaje mashine hizi zikijaa zisifutwe tu kile kilichojaa kama hakitakiwi tena na mlipa kodi akaendelea na mashine yake.

Au kwanini kusiwe ni kifaa cha pesa ndogo kubadilishwa na mashine kuendelea kutumika.

Kwanini tumeruhusu teknolojia ya kinyonyaji na kuongeza uzito wa biashara.Na kwanini tuendekeze matakwa ya makampuni ya kinyonyaji badala ya wao kufuata masharti yetu katika kutuuzia vifaa vyao.

Ukiondoa huko kujaa kwa mashine pia mashine zenyewe hazikawii kuharibika na kosa lolote wasambazaji wanataka pesa tele kuiangalia.

Vipi TRA hawaoni kuharibika mara kwa mara kwa vifaa hivi vinachangia kupunguza kodi na kwamba ni mzigo kwa mlipa kodi.
Kufa kufaana. Tangu ujio wa mashine hizo iligunduliwa msambazaji mkuu alikuwa ni mtoto wa mkazi no 1 wa ikulu kwa wakati huo, and the price was highly inflated. Mbali ya kuongeza gharama kwa mfanya biashara, kitaifa hukomba fedha za kigeni kwani hazitengenezwi nchini.
 
Kufa kufaana. Tangu ujio wa mashine hizo iligunduliwa msambazaji mkuu alikuwa ni mtoto wa mkazi no 1 wa ikulu kwa wakati huo, and the price was highly inflated. Mbali ya kuongeza gharama kwa mfanya biashara, kitaifa hukomba fedha za kigeni kwani hazitengenezwi nchini.
Nakumbuka mkuu wa mkoa wa Lindi mhe. Godfrey Zambi enzi hizo akiwa mbunge wa Mbozi aliliongelea sana suala hili bungeni, kwamba kule China mashine hizi za EFD zinauzwa kati ya dola 100 mpaka 123, Zikija Tanzania wanauza laki 8 mpaka milioni. Na zilikuwa na waagizaji maalum ambao wako approved na TRA kwa monopoly style. Alihoji kwa nini wasingeruhusu kila mtu aagize anakotaka, lakini ziwe na standards ambazo ni approved na TRA? Iwe kama zilivyo simu, kwamba lazima zikidhi vigezo fulani kabla hazijaingia sokoni. Naona hizi mashine ni biashara za wakubwa
 
Mfumo ullio eleweka wa data machine yeyote ni uwezo wa ku upload data kwenda data storage nyengine iwe USB stick au server mfano servers za TRA ,siku yeyeto muda wowote hapo hapo ku release storage kwa matumizi mengine. Kama ni kweli mashine zinajaa hilo ni fatal design flaw ambayo haikubaliki.
 
Hawa wajinga waliniuzia mashine mbovu yaani muda naoitumia ni mdogo kuliko unaotumika kwenye matengenezo.
 
Kwa sababu zikiharibika hawazitaki tena basi matumizi kama hayo ya redio yangepunguza machungu kwa muda huu hatujapata kitu bora kuliko hizo efd.
Kiukweli mashine EFD ni moja ya miradi ya kinyonyaji tulionao nchini spare zake ghali mno
 
Hizi mashine eti zinajaa na ikitokea hivyo unanunua kwa bei ile ile ya karibu ya milioni.

Ajabu ni kuwa mashine hizi zinazotumiwa na TRA kukusanyia kodi haziendi hata miaka 3 kujaa kwake na hasa ukiwa ni mlipa kodi mzuri unayetoa risiti kwa kila mauzo.

Inakuwaje mashine hizi zikijaa zisifutwe tu kile kilichojaa kama hakitakiwi tena na mlipa kodi akaendelea na mashine yake.

Au kwanini kusiwe ni kifaa cha pesa ndogo kubadilishwa na mashine kuendelea kutumika.

Kwanini tumeruhusu teknolojia ya kinyonyaji na kuongeza uzito wa biashara.Na kwanini tuendekeze matakwa ya makampuni ya kinyonyaji badala ya wao kufuata masharti yetu katika kutuuzia vifaa vyao.

Ukiondoa huko kujaa kwa mashine pia mashine zenyewe hazikawii kuharibika na kosa lolote wasambazaji wanataka pesa tele kuiangalia.

Vipi TRA hawaoni kuharibika mara kwa mara kwa vifaa hivi vinachangia kupunguza kodi na kwamba ni mzigo kwa mlipa kodi.
Inajaa vipi? Kwamba unalipa sana kodi ndio inajaa(bilioni ngapi inajaa)?
 
Hii ya kujaa ndio naisikia. Ni hivi hizi machine zinawekewaga sales limit yaani unawekewa may be million mia. Sasa ukiuza ukifikia hicho kikomo hutoweza endelea ku punch na si kua hutoweza kutumia tena hiyo machine bali utaenda kwa dealer ataweka limit nyingine na utaendelea ku punch kama kawaida.
 
Inajaa vipi? Kwamba unalipa sana kodi ndio inajaa(bilioni ngapi inajaa)?
Kiukweli mauzo yangu si makubwa kwa hivyo risiti pia zitoi nyingi pamoja na hivyo imejaa miaka 3 haijaisha.Nashangaa wale wauzaji wakubwa wa jumla huwa wananunua mashine ngapi kwa mwaka.Lakini wao sio mimi haiwaumi sana kwa vile fehda zinaingia za kutosha
 
Hii ya kujaa ndio naisikia. Ni hivi hizi machine zinawekewaga sales limit yaani unawekewa may be million mia. Sasa ukiuza ukifikia hicho kikomo hutoweza endelea ku punch na si kua hutoweza kutumia tena hiyo machine bali utaenda kwa dealer ataweka limit nyingine na utaendelea ku punch kama kawaida.
Hamna kitu kama hicho na kama kipo kuna haja gani kuwa na mashine si turudi kwenye makadirio tu.Nionavyo mimi madhumuni ni uandike risiti kila unachouza ili kodi iongezeke na ujulikane kiwango chako cha makadirio ya mikupua,ipande au ishuke na jee umeshafikia kiwango cha kuingizwa VAT ili ulipe zaidi ya awali.
 
Back
Top Bottom