Kwanini Marais wengine wastaafu kama Mwl. Nyerere na wengine hawasifiwi kwa kujenga miundombinu?

Nyerere ndiye kiongozi pekee aliyetoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu.
Alijenga viwanda vingi sana mfano ;
Urafiki, Mwatex, kilitex, musoma textiles Sunguratex Moroccans ,moproco mgololo paper mills Mbeya textiles, Twiga cement, Tanga cement na vingine vingi tu

Lakini kubwa zaidi anakumbukwa kama shujaa wa Afrika kwa kuitangazia dunia tulipovamiwa na Nduli IDD Amini, kuwa atampiga.
Akasema, sababu, uwezo na nia anayo na akampiga kweli kweli na kumwondoa madarakani.
Haijawahi kutokea katika historia ya Afrika Rais wa nchi kupigwa na nchi Jirani na kukimbia nchi.Huyu aliwaua RAIA wake zaidi ya 500000 na akavamia Ardhi yetu akaua wananchi wetu, akaharibu na kupora Mali.
Mwl.Nyerere aliwaomba OAU walaani uvamizi huo uliofanywa na nduli Amin waliposhindwa kufanya hivyo, kwa uongozi wake mahili, aliwaunganisha watanzania wote, waliokuwa mstari wa mbele vitani na waliokuwa wakiendelea na shughuri za kiuchumi kupambana kila mtu kwa nafasi yake, na akasema; vita hiyo lele mama,watanzania pambaneni kila MTU kadri ya nafasi yake.
na hatimae tukashinda vita hiyo ya kihistoria na kulejesha utu na heshima ya mtanzania kwenye sura ya dunia.
Ameacha legacy ambayo siyo ya kulazimisha "eti ooh legacy legacy ya mwendazake". Huyu kaacha legacy ambayo ipo tu. Halafu akatokea mtu mmoja akaviua viwanda vyote kwa decision ya ajabu!!!! Naumia sana nikikumbuka viwanda vilivyokuwepo halafu vikauliwa overnight kwa kisingizio cha ubinafsishaji!!! Kuna mashirika kama NBC, TBL, TTCL nk. hayakuwahi kuregister hasara lakini hesabu zikapikwa kuonyesha yana hasara ili yachukuliwe na so called investors!!! Hao investors kwanini wasianzishe vitu vyao? Nakumbuka eulogy ya Madeline Albright kwa late J.K. Nyerere ilivyokuwa nzuri sana!!!
 
Tatizo kuna wanasiasa hasa vijana wasiojua vyema historia ya Tanzania na watu wazima walioamua kujitoa ufahamu tu. Matokeo yake wanaishia kudemka tu badala ya kujadili mambo ya msingi.

Hayati Nyerere siyo tu alijenga reli ya uhuru, ya kisasa kabisa kwa wakati huo, toka Dar es salaam mpaka Kapirimposhi, bali pia alijenga mabwawa kadhaa ya kuzalisha umeme na gridi ya kuweka miundombinu ya kuusambaza umeme huo nchini. Hapo hatujaongelea viwanda mbalimbali ya kati vilivyojengwa sehemu mbalimbali nchini vikiongozwa na vile vya nguo. Lakini kubwa kuliko yote ni umoja wa kitaifa alioujenga na kuusimamia kwa nguvu zake zote. Na pia alikuwa kielelezo cha uadilifu kwa maraisi waliomfuatia na marais wa Afrika. Hapo hatujaongelea uongozi wake katika vita ya kuzikomboa nchi za kusini mwa Afrika zilizokuwa chini ya utawala wa kikoloni na kuifanya Tanzania kituo kikuu cha harakati za ukombozi. Ni yeye pekee ndiye mwenye sifa za kuitwa SHUJAA WA AFRIKA.

Mzee Mwinyi naye amefanya mambo makubwa ikiwemo uamuzi mgumu wa kuruhusu mfumo wa soko huria na kuuondoa mfumo wa uchumi wa dola uliojengwa wakati wa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea kama ilivyoainishwa kwenye Azimio la Arusha. Kupitia azimio la Zanzibar Tanzania ilipitia mabadiliko makubwa ya kiuchumi yaliyowezesha mitaji binafsi kuingia nchini na kubadili mwelekeo wa nchi kiuchumi. Mzee Mwinyi pia ndiye aliyekuwa muasisi wa siasa za ushindani wa vyama vingi.

Hayati Mzee Mkapa kimsingi ndiye chief architect aliyesuka mikakati ya kutufikisha kwenye uchumi wa kati na alifanya maboresho mbali mbali ya kimfumo na kiutendaji ili kuwezesha Ndoto ya kufikia uchumi wa kati 2025 ifikiwe. Katika utawala wake ndiyo ile ndoto ya kuunganisha nchi kwa barabara za lami ilianza kutekelezwa na ninakumbuka vyema alipotoa ahadi ya kuunganisha Bukoba na mtwara kwa lami jinsi ilivyofanyika kazi kwa vitendo.

JK akiendeleza alipoishia Hayati Mzee Mkapa alisimamia miradi mingi sana ya ujenzi wa uchumi ambayo mingi imezinduliwa wakati wa Hayati Mzee Magufuli. Pengine Mzee JK ndiye Rais aliyeanzisha miradi ya ujenzi wa bararaba za lami zenye urefu mkubwa zaidi kuliko raisi mwingine yeyote kwenye historia ya nchi yetu. Miradi ambayo JK aliianzisha na kuisimamia ni pamoja na:
(i) Chuo Kikuu cha Dodoma
(ii) Jakaya Kikwete Cardiac Center Muhimbili
(iii) Ujenzi wa airport Terminal III
(iv) Kutekeleza mradi wa BRT ulioasisiwa na Hayati Mkapa
(v) Mradi wa Bomba la Gesi ya Asili toka Mtwara Mpaka Dar es salaam
(vi) Ujenzi wa shule za sekondari kila kata
(vii) Ujenzi wa barabara ya lami toka Tunduma - Katavi
(viii) Ujenzi wa barabara ya lami toka Ruvuma Mpaka Lindi
(ix) Ujenzi wa barabara ya lami toka Dodoma mpaka Babati
(x) Ujenzi wa daraja la Mfugale
(xi) Ujenzi wa ringroads kupunguza msongamano wa magari DSM
etc. to mentiom a few.

Anayesema hakuna kilichofanyika kabla ya Mwendazake ama haijui vyema historia ya nchi yetu au ni mjinga tu anayehitaji kuelimishwa kwa busara na upole.

Tata said!
Umedadavua vizuri sana. Wajinga wengi humu hawajui haya au vichwa vyao vina walakini kwa kutojkujua haya.
 
Utoto unakusumbua au lack of information!

Hujui kwamba hujui au unajitoa ufahamu?

Nyerere alijenga reli ya Tazara.
Alijenga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Alijenga hospitali ya Muhimbiri.
Alijenga Mzumbe.
Alijenga vyuo vingi sana ambavyo leo vimebadilishwa kuwa vyuo vikuu.
Alinunua ndege nyingi tu.
Alijenga shule za sekondari nyingi ikiwemo Sengerema na ile ya Singida mjini,nimesahau jina lake.
Alijenga zaidi ya viwanda 400!

The list is endless!
Ongeza:

Mtera Hydroelectric Dam
Nyumba ya Mungu Hydroelectric Dam
Hale Hydroelectric Dam
Kidatu Hydroelectric Dam.

Hapo ni suala la umeme tu. Hatujaongelea vyuo vya ualimu, shule za sekondari, etc
 
Nyerere aliiheshimu katiba, Mwinyi pia aliiheshimu na sidhani Kama Kuna mtu alifia mikononi mwa polisi kwa sababu za kisiasa kipindi Cha Mwinyi.
Nawewe endelea.......
Nyerere na Mwinyi hawakua na sababu ya kujitapa na kujitangaza maana waliyofanya yalionekana.
Muogope sana mtu anayejisifu
 
Hivi kwanini Marais wengine wastaafu kama vile Mwl. Nyerere na wenzake waliomtangulia Rais Magufuli wao hawasifi kwa kujenga miundo mbinu?

Swali ni je Marais wastaafu wakiongozwa na Mwl. Nyerere wao hawakujenga miundo mbinu kama Rais wetu mpendwa wa awamu ya 5?

Kila mara anaposifia Rais wetu mpendwa wa awamu ya 5 Rais Magufuli watu wengi wanajikita katika ujenzi wa miundo mbinu.

Swali linalokuja kwa wananchi walio wengi ni je, mbona marais wengine waliopita wao hawasifiwi kwa kujenga miundo mbinu?
Mwenye jibu tafadhali tunaomba atusaidie.
Kwa sababu waliotangulia walifanya mambo yote unayoyaona sasa, ikiwemo kutoa uhuru wa watu kusikia upande wa pili.

Ila miaka mitano ya Magufuli, kizazi cha sasa kililazimishwa kusikia kile anachofanya na kukatazwa kuzungumzia yale waliyoyatamani yafanyike
 
Nyerere madarakani zaidi ya 20 years miundo mbinu aliorithi kwa wakoloni aliharibu ... Hana sifa nzuri zaidi ya mbaya kwa hiyo bora tukanyamaza
Kama ulisoma basi hata vidudu hukustahili, yaani mbumbu uliepitiliza! shukuru Mungu unajua kuandika!! hata pole hustahili.
 
Hivi kwanini Marais wengine wastaafu kama vile Mwl. Nyerere na wenzake waliomtangulia Rais Magufuli wao hawasifi kwa kujenga miundo mbinu?

Swali ni je Marais wastaafu wakiongozwa na Mwl. Nyerere wao hawakujenga miundo mbinu kama Rais wetu mpendwa wa awamu ya 5?

Kila mara anaposifia Rais wetu mpendwa wa awamu ya 5 Rais Magufuli watu wengi wanajikita katika ujenzi wa miundo mbinu.

Swali linalokuja kwa wananchi walio wengi ni je, mbona marais wengine waliopita wao hawasifiwi kwa kujenga miundo mbinu?
Mwenye jibu tafadhali tunaomba atusaidie.
Kwa sababu tuna akili Kama kuku! Huyu Samia she has blood in her hands. She told Magufuli was ok. Nchi zingine angeambiwa ajiuzulu, alidanganya taifa, it is the biggest mistake any president can do, lakini sisi yumeshashau yote hayo, how stupid are we?
 
Nyerere madarakani zaidi ya 20 years miundo mbinu aliorithi kwa wakoloni aliharibu ... Hana sifa nzuri zaidi ya mbaya kwa hiyo bora tukanyamaza
Hujui historia nenda ukalale, Reli ya uhuru(TAZARA) uliijenga wewe?,Bmba la mafuta (TAZAMA) Dar es salaam -Zambia ulilijenga wewe? TanZam Highway barabara ya rami Dar hadi Zambia uliijenga wewe? shule ulikuwa unaenda kufanya nini wewe? kazi kuganjika tu kichwani hamna kitu.
 
Hiyo chuki uliyonayo brother achana nayo huwa siyo nzuri kwa afya.
Mwache apumzike na hukumu yake itakuwa ya haki kwa kadiri ya matendo yake wakati wa uhai wake, na kwako maisha lazima yaendelee, usiruhusu nyongo ianze kukuathiri mapema kiasi hiki.
Mwendazake ana achievements za kawaida sana na nyingi za miradi ni za kumalizia walipoanza watangulizi wake hususan JK na BWM. Yeye zake ni Stiglers, SGR, Mandege na Busisi.

Lakini kuna mafanikio makubwa ambayo watangulizi wake waliyapata bila kuua watu, kudanganya, kutolipa increments za wafanyakazi.

MAUJINGA ya mwendazake ni mengi kuliko anayodaiwa ameyafanya
 
Kila rais anacho kipaji chake chenye kumtofautisha na mwenzake. Mzee Mwinyi alisema pale Chato kuhusu wao watangulizi kushindwa kuhamia Dodoma kwa miaka 42 na hayati JPM akaweza kufanya hilo kwa miaka miwili tu.

JPM alijitofautisha na waliomtangulia kwenye suala zima la kuhakikisha anachotaka kifanyike kinafanyika kwa wakati husika.

Mwalimu alilazimika kujenga miundo mbinu mingi akiwa ni rais wa kwanza wa Tanzania. Nina uhakika kwa kujiamini alikokuwa nako hayati JPM na uwezo wa kuwa na kauli isiyotaka masikhara kama angekuwa ni rais wa kwanza au wa pili, nchi hii ingekuwa mbali sana siku nyingi zilizopita.

Nyerere alijaliwa diplomasia na uwezo wa ushawishi. JPM hana sifa hizo, yeye ni mtendaji asiyetaka utani kazini. Kimataifa hakuna rais kama Nyerere, Mkapa na Kikwete walijaribu lakini hawakumfikia katika sekta hiyo.

JPM analivaa tatizo kwa ukubwa wake na anahakikisha linatatuliwa. Alichokuwa nacho hayati JPM kingemsaidia sana JKN miaka ile ya mwanzo wa ujenzi wa taifa hili kama angepata msaidizi wa viwango vya JPM hawa wakenya na majirani wengine wangetia akili.
 
Back
Top Bottom