only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
......Kwa wale wakristo wanafahamu kuna andiko kwenye Biblia linasema adui yako ni yule wa nyumbani mwako..Nilikuwa sielewi vyema msingi wa hili andiko..Lakini siku za karibuni nimeona wasichana wawili waliokuwa marafiki mpaka wakaanza kufanana kwa sura na hata kuvaa nguo sare sasa wamekuwa maadui kama paka na panya...na sababu ni za matatizo ambayo yanaweza kutatulika..ni kutofautiana kwa kauli dhidi yao..Nimejaribu kuwasuluhisha lakini wapi.Huu ni mfano mmoja lakini mara nyingi marafiki ndio wanajenga uadui kwanini? Nashindwa kuelewa sayansi iliyopo hapa..Maana nilitegemea kuwa marafiki ndio wanaweza kumaliza tofauti zao kirahisi kitu ambacho hakitokei kwa ulimwengu wa leo.