Kwanini Makonda na Magufuli na Nyerere wanaiga....CCM inadanganya

Kessy Wa Kilimanjaro

JF-Expert Member
Jan 23, 2016
327
208
Ukisikiliza kwa umakini kila wakati magufuli au makonda wakiwa wanatoa hotuba au Maraisi waliopita, utasikia jinsi wanavyopenda kuongelea mifano kutoka Nchi kama China.

Kwanini wafanyasiasa watanzania na Viongozi wanapenda kuiga nchi kama China. Kwasababu mfumo wa CCM, and fikra za sera zinafanana.

CCM inatamani kuwa kama chama kinacho tawala china ambacho ni the Communist Party Of China, au Chinese Communist Party, CCP. Hiki chama pekee ndiyo kinatawala China Nzima.

Haya yote yalianza wakati wa Nyerere kujihusisha na wachina. Alipoenda kufundishwa Ujamaa na wachina ndipo walipompa mbinu za kuhakikisha chama chake pekee ndiyo kitakachotawala nchi.


Tangia Nyerere CCM imehakikisha kwamba itabaki madarakani kama Chama cha wachina ili ipitishe sera zao za Ujamaa ambazo China inazipenda ndiyo maana wanaendelea kujipendekeza kwa Magufuli na wengine waliopita kama kikwete.

MAIN POINTS AND CONCLUSIONS.

Kwasababu CCM inafwata mfano wa chama cha china basi hakutakuwa na chama chochote kingine ambacho kitaingia madarakani bila kuwepo na ugomvi au vita. CCM itaendelea kuiba kura au kudanganya vyovyote ili ibaki madarakani.

Sababu ya kuwa na elections ni ili tu waonekane democratic kwa watoa misaada lakini hamana kitu democratic kuhusu Tanzania.

Kwasababu CCM wanaiga mfano wa China, hawajui kwamba China inadanganya kuhusu uchumi wao kukua. China inafeki GDP yake, and inashusha interest rate yake na inapoteza hela kwenye majengo na miradi ambayo hamna mtu anaishi.


CHA MUHIMU KUELEWA NI KWAMBA KILA SERA ITAKAYO PITISHWA NA MAGUFULI AU MAKONDA ITAFELI KWASABABU HAWA NI WATU AMBAO HAWAELEWI UCHUMI NA WALA HAWAJUI JINSI YA KULETA MAENDELEO BALI WANAIGA NCHI KAMA CHINA AMBAYO INAFEKI UKUBWA WA UCHUMI WAKE. JIULIZENI KATI YA MIRADI ILIYOAHIDIWA NA CCM MPAKA SASA NI MINGAPI IMEFANIKIWA NA IKALETA MAENDELEO?
 
Usiitie Najisi Serikali Ya China Kufananisha na Watu Dhaifu Kama Hao.

Chinese Hawatengenezi Vyeti Bandia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom