ni kwamba katiba inasema ikiwa rais atatoka bora makamu atoke zanzibar virse versa
Iwapo huyo Makamo anatoka zanzibar inakuwaje anashughulikia mambo ya Tanganyika? Na kama ulivyosema alipata wapi ridhaa ya Wazanzibari kuwawakilisha?Takribani Wzanzibar wengi kama mimi wana mawazo kama hayo yako, kwanza huyu sio makamo wa Raisi ktk sheria ya katiba ya Muungano, Kisheria Raisi wa Zanzibar ndio makamo wa Raisi na huchaguliwa na Wzanzibar wenyewe sio huyu alopendekezwa na chama.a.) b.)nikuwa huo Muungano wenyewe haupo tena between Tanganyika na Zanzibar hivi sasa kuna mazowea tu.
Muungano umekufa baada ya kufa tu kwa Tanganyika na katiba ya Tanganyika, sasa hivi tunaishi kutokana na Mazowea ya kuwa tuliungana na ikifa ccm ndio sizani kuwa Muungano utakuwepo Zanzibar.
Sijakataa kuwa hilo jambo limo ndani ya Katiba. Nionavyo mimi hao walioandika kipengele hichi Katiba walilifanyia uchunguzi suwala hili? Huu ulikuwa ni uamuzi wa papo kwa papo wa CCM waliokuwa wakifikiri kuwa hii nchi ni yao peke yao. Sioni mantiki ya kuwepo Makamo wa Rais iwapo Rais anatoka Bara. Tuchukulie mfano wa DR Gharib Bilali hivi sasa yuko kumsaidia Kikwete kwa upande gani, Tanganyika au Zanzibar. Zanzibar kuna Rais wake na ndie mwenye mamlaka ya serikali ya Zanzibar na hata siku moja kwa kipindi cha miaka zaidi ya 15 toka uanze utaratibu huu, Makamo wa Rais hajawahi kushughulikia mambo ya Zanzibar.Kasome katiba.
Wanajamii Forums hapo juu nawakilisha swali langu na pia kueleza mtizamo wangu juu ya jambo hili. Naomba mchango wenu lakini naomba tuchangie kwa hoja za kujenga!
Mkuu.
Hii katiba iliyopo haikufuata utaratibu ule uliokubaliwa na waasisi wa Muungano.
Imekuwa ikibadilishwa na CCM kiaina aina tu, kutokana na political calculations zao.
Bora inawasaidia kubakia katika madaraka.
Sijui lini "watanzania" tutatambua kuwa hii katiba ni bomu tu linalosubiri kutupasukia na kutumaliza.
Vizuri kabla ya Katiba mpya, yatangulie majadiliano ya Muungano wenyewe kwanza.
Mimi ningependa sana iandikwe katiba mpya kwa ajili ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Si lazima kuwa na katiba kwa muungano. makubaliano tu ambayo yako elaborative yanatosha.
La msingi na muhimu ni kuwa na katiba ya Tanganyika na Zanzibari wawe na Katiba yao.
Inapokuja Urais wa Serikali ya Muungano.Iwe ni kwa kubadilishana.Kipindi kimoja Rais kutoka Tannganyika na makamo kutoka Zanzibar na kinyume chake inapofika muhula mwengine.
Hii inaweza kuwa miaka miwili, miwili.
Kuwe na bunge dogo la Muungano.EAC style.
Au iwe Urais uwe katika mikono na marais wawili kwa pamoja. Yaani rais wa Tanganyika na Rais wa Zanzibar kwa pamoja wawe ndio Taasisi ya Urais wa Muungano.
Kwa hivi ilivyo leo katiba iliyopo ,mimi naona hakuna mantiki wala seriousness juu ya Muungano.
Wenzangu najua kuwa Katiba inasema hivyo lakini jee waliotia hili kwenye Katiba walikusudia liwe na maana gani katika Muungano wetu?
Mkuu.Kinachotusumbua ni huu urafiki wa chako chetu na changu changu.
Kwa kuwa Serikali ya Tanganyika haipo, na kama ipo haina Rais, haina Waziri mkuu wala makamu wa Rais, nasema hivi kwa sababu viongozi hawa wakuu ni wa Muungano. Kama tunajiaminisha kuwa serikali ya Muungano ndo ya Tanganyika, Je nani anaiwakilisha Tanganyika kwenye Serikali ya Zanzibar iwapo tunajua Raisi wa Zanzibar ni mjumbe wa Baraza la mawaziri Muungano, na makamu wa Rais anawakilisha Zanzibar?
Fact ni kwamba ktk united republic state yoyote presda anapotoka side flani side nyingine inabidi atoke makamu ili kuensure muungano kwani kwakutofanya hivyo side mojawapo inaweza kujiengua kwa kile kinachoelezwa kuwa kutothaminiwa.