Elections 2015 Kwanini Magufuli hafai kuwa Rais?

pepsin

JF-Expert Member
Apr 23, 2015
3,465
6,109
Magufuli hafai kuwa rais kwa sababu hizi,
1.Sio mwanasiasa.Tanzania bado haipo tayari kuongozwa na mtu asiye mwanasiasa.Tanzania inahitaji kiongozi mwanasiasa anayeweza fanya lobbying na mwanadiplomasia.
Hii pekee inakufanya usimpe Magufuli kura.
2.Magufuli ni mtendaji na sio kiongozi,tunahitaji kiongozi.
Tanzania haimtafuti bwana miradi au mkurugenzi wa maendeleo!Tunamtafuta mtu wa kutoa dira na kukwamua nchi penye mikwamo.Magufuli ni msimamizi mzuri wa miradi ila sio kiongozi wa mfano.Nchi inaweza kujikuta kwenye migogoro na mikwamo kama kiongozi wake hana ushawishi wa kutoa dira.
Hizi ni sababu kubwa za kutokumpa kura yangu Magufuli.
 
Wee sio mzima kabisa,nchi hii imefikishwa kwenye majanga kama haya na wanasiasa kwa sasa tunataka rais mtendaji na mwanasayansi ambaye akiongea kitu lazima akakisimamie na anahakikisha kimetekelezeka ,
 
hivi nyie si ndo kilasiku mlikuwa mnaimba mnamtaka rais dikteta baada ya Kikwete 'kuchekacheka' sana?
 
tatizo la Magufuli ni moja tu, yupo chini ya CCM.... Hilo tu, mengine yote Magufuli yuko fit sana...
EL kinachomnyanyua ni kimoja tu, yupo chini ya UKAWA, hilo tu.. mengine yote hayuko fit kabisa.
 
Nyerere tu ndio alikuwa mwanasiasa.Wengine waliomfuata ni shidaaah!
Magufuli kama sio mwanasiasa ataitangazaje nchi? Kwa kusoma idadi ya samaki na kilometer za barabara?
Noooon.Tunahitaji kiongozi! Baada ya Nyerere hatujapata kiongozi bali watawala! Sasa tumweke mtu mwingine anayekiri kuwa siasa kwake ni shida?? Hapana.
 
Tatizo liko ccm... ndo maana Dr. Magufuli naye ameshawastukia... Wanalumumba wanaangaika kuandaa hotuba akipewa asome anaiweka pembeni anakuja na ya kwake mwenyewe...
Magufuli ameshabaini kuwa ili ashinde inabidi ajitofautishe na wanaccm wengine...
Ikumbukwe kuwa Magufuli hakujiandaa kugombea Urais. Jaribu kufuatilia kwa karibu utaona anajitahidi kuiga kila kitu kutoka kwa Lowassa kuanzia kaulimbiu hadi mavazi...!!

ccm ni matapeli na hapa wanamtapeli Dr. Magufuli mchana kweupe..!! Mtu tokea awali alijiandaa kwenda kumpigia kura Lowassa kwenye preliminaries kule ccm ghafla bin vuu anajikuta kabebeshwa zigo lote la choo chakavu...!!
Badala ya kumpa support amepewa watukanaji na wapi dili...
Kwa ninavyomfahamu Magufuli atakuwa anajuta sana...
 
Tatizo liko ccm... ndo maana Dr. Magufuli naye ameshawastukia... Wanalumumba wanaangaika kuandaa hotuba akipewa asome anaiweka pembeni anakuja na ya kwake mwenyewe...
Magufuli ameshabaini kuwa ili ashinde inabidi ajitofautishe na wanaccm wengine...
Ikumbukwe kuwa Magufuli hakujiandaa kugombea Urais. Jaribu kufuatilia kwa karibu utaona anajitahidi kuiga kila kitu kutoka kwa Lowassa kuanzia kaulimbiu hadi mavazi...!!

ccm ni matapeli na hapa wanamtapeli Dr. Magufuli mchana kweupe..!! Mtu tokea awali alijiandaa kwenda kumpigia kura Lowassa kwenye preliminaries kule ccm ghafla bin vuu anajikuta kabebeshwa zigo lote la choo chakavu...!!
Badala ya kumpa support amepewa watukanaji na wapi dili...
Kwa ninavyomfahamu Magufuli atakuwa anajuta sana...

Magufuli.akundaliwa Kua raisi ndio maana ata tshert khanga na kofia za magufuli.hakuna inaonekana alipandishiwa tren kwa mbele
 
Wanasiasa wezi hatuwataki tunataka mchapakazi tu. Hii ni awamu ya Magufuli. Mtoa post Kajipange tena ndo urudi hapa umegonga mwamba.
 
Back
Top Bottom