Kwanini Magufuli ana hofu akitoka mwingine ataharibu? Nini kifanyike kusiwe na hofu?

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Moja ya hofu kubwa aliyonayo Rais John Magufuli ambaye pia anagombea nafasi ya Urais ni Kuwa watanzania wawe makini na kura Maana wanaweza kuwapigia Kura Watu halafu wakaiuza nchi ama wengine kuharibu miundombinu ambayo Serikali yake inaijenga.Rais ameenda mbali na kuwataka watanzania wasifanye majaribio Kwenye kuchagua.

Nadhani namna pekee ambayo inaweza kuwa tiba dhidi ya hofu ya Mh Rais ni kuibadili katiba yetu pamoja na mfumo mzima wa kiutawala ili tujenge taifa lenye Taasisi Imara Kama alivyopata kushauri Prof Mussa Assad wakati akihojiwa na idhaa ya Kiswahili ya umoja wa mataifa.

Kama hofu ya Rais Magufuli inatoka moyoni na anamaanisha basi Hii ni ishara nchi hii....

1.Katiba yake ni dhaifu Maana haina ubavu wa kumzuia mtu kutorosha mali,Kwa nini Rais Magufuli Kwenye Kampeni zake asianze Sasa kuahidi kuendeleza mchakato wa kuandika Katiba mpya ili tuwe na Katiba inayowadhibiti viongozi?

2.Nchi Hii ina taasisi dhaifu ambazo haziwezi kuwadhibiti viongozi wasifanye watakavyo,Kama ni hivyo Kwa nini Rais Magufuli asiwaahidi watanzania Kuwa akichaguliwa Kuwa Rais atabadili Katiba ili tuwe NA Katiba ambayo itajenga taasisi imara(Bunge,Mahakama,Vyombo vya ulinzi na usalama),ambavyo vitawadhibiti viongozi wetu wasifanye watakavyo.

Binafsi nauona mwarobaini wa hofu aliyonayo Mh Rais,labda huko mbele ataungana na wagombea wengine kuahidi mabadiliko ya Katiba Kwa kuandika Katiba mpya ambayo itajibu changamoto za nchi.

Wasalaam.
 
Kabla ya yeye kuwa Raisi walikuwepo wenzake waliongoza kwa muda waliondoka kama yeye atavyoondoka 28.09.2020 Jiwe ni muoga anajua maovu aliyofanya madikteta wengi wakishaingia madarakani wanajiona wao tuu wanaweza kuongoza tuu #NIYEYE
 
Ana jua akiingia yule bwana cha kwanza ni kulipa visasi kwanza mengine ndo yafate.
 
Kuna maeneo kadhaa anajuwa alikurupuka na ameharibu kama ifuatavyo:
1. Kuhamia Dodoma
2. STIGLERS GORGE
3. SGR kuanza kwenda Rwanda badala ya Uganda
4. Kiwanja cha ndege Chato
5. Kivuko cha Lake Victoria
6. Kununua ma-Dreamliner bila mpangilio

Haya ma miradi hata akija msaidizi wake wa Karibu kama Kassim Majaliwa au Palamagamba Kabudi atapindua ndani ya siku100 za kwanza. Siyo lazima CDM kwa kuwa haihitaji kuwa na PhD kujua kwamba yalifanywa kwa ajili ya sifa na hayana upembuzi yakinifu
 
Atawale milele hadi kiti kitakqpo mkuta,ndiyo hofu itaisha.
 
Kweli zito kabwe alisema tumewakabidhi nchi wasamba na malimbukeni.

Mtu anashindwa kutengeneza taasisi na mifumo Bora ya uongozi, Badala yake anajenga vitisho na kudhani kuwa ataishi milele.

Kinana na nape walisema " jamaa ni mshamba sana"
 
Hadi hapa hakuna jinsi jiwe ataondoka madarakani asipate shida hata kama rais atakayefuata ni kutoka ccm, walioko ccm wanajua unafiki vizuri na wanatunza tu nafasi zao na watamwonesha sura zao halisi atakapomaliza muda wake. Amekuwa rais wa hovyo kuwahi kutokea.
 
Katiba ni dhaifu na hawataki kuibadilisha tuwaiteje hawa watu wanaofurahia udhaifu wa katiba yetu, ni kwa hakika udhaifu huo wana maslahi nao binafsi.
 
Ukiona ana hofu hiyo, ujue hata yeye huenda kuna mipango iliyobuniwa na watangulizi wake, na alipoingia madarakani aliitupilia mbali.
 
Hofu yake inakishindo na ukweli, wapinzani wake wanaponda kila kilichofanyika, Kwa namna hiyo ni lazima astuke kuwa hawa watu ni robotii au? Je wataweza kuendekeza kweli hiyo Miradi wanayoiponda kuwa haina maana yote
 
Kwani yeye kafanya nini chamaana? usihadaike na wapuuzi wanaoongea ujinga sababu yakujaza maatumbo yao hana cha maana alichofanya
 
Hawawezi kuweka katiba mpya hao, wanajua wanawaandalia mazigira watoto wao, si unajua wameifanya Nchi kama ya familia zao
 
Mkuu Wala usichukulie maanani mambo yanayosemwa na incompetent people like Magufuli,ni ushamba na incompetency yake tu ndo inamfanya aone amefanya kazi kubwa na ya maana sana ambayo haiwezi kufanya na mwingine, kutokana kukosa akili hata hajiulizi kwamba akifa kesho na nchi hii itakufa? Ethiopia Wana ndege 125,Bwawa kubwa la umeme Africa,SGR na maflyovers but waziri mkuu kaondoka madarakani sembuse huyu incompetent?
 
Haya Mambo ya katiba na mifumo ya utawala wa nchi ni Mambo makubwa sana ambayo huyo unaemwambia hana akili nayo.Huyo anajua maguvu na kufoka foka.Incompentent individual
 
Anaogopa akiingia mwanasheria ikulu baada yake kila siku atakuwa anahukumiwa kwenda jela, atakuwa na kesi nyingi sana za kujibu.
 
Back
Top Bottom