Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakubahatika kuchaguliwa kujiunga na mafunzo JKT?

Mimi binafsi natamani kama VETA wangeanzisha program ya kufundisha kozi fupi za namna ya kutengeneza out board injini za boti,marekebisho ya fiber boat, usukaji wa zana za uvuvi hii program ikifanyika mikoa yenye maziwa,mabwawa,mito mikubwa na bahari ingesaidia sana kuwapa skills vijana wengi na wangejiajiri.

Mpaka sasa Tanzania hakuna chuo au taasisi yoyote inayofundisha ufundi wa injini ndogo za petrol za boti. Mafundi wengi wanatumia uzoefu na wengine wamiliki wanarekebisha wenyewe.
Nadhani FETA Mbegani wanatoa haya mafunzo
 
Nadhani FETA Mbegani wanatoa haya mafunzo
FETA iwe Mbegani au Nyegezi wao hutoa mafunzo ya uvuvi kuanzia ngazi ya cheti.

Nazungumzia kuhusu kutolewa short course za hivyo vitu. Maana ukiangalia syllabus ya FETA wao wana Kozi ya Master Fisherman, Marine engineering ila ndani kuna module wanafundisha diesel engine na kurekebisha injini za boti ila tambua mtu anayetoka hapo outboard engine kasoma nadharia.
 
Kwa msisitizo tu ni kwamba kijana yoyote ambae ni raia wa kuzaliwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambae amemaliza kidato cha sita anapaswa kujiunga JKT kwa mujibu wa sheria.

Hiyo haijalishi umemaliza Mzizima, Al Haramain au Feza boys au Girls.

Iwe ni kwa mujibu kwa sheria ya JMT.

Na hata iwe kwa sababu mbalimbali kijana huyo hakuweza kujiunga huo basi iwe ni deni na atumukie kwa muda utakaofaa.

Nchi kama Israeli, Korea Kusini, Kazakhstan na zingine wanafanya hivyo.

Hii yaondoa matatizo kama kutokuwa mzalendo, uzembe wa kufikiri na ushawishi wa kujiunga na makundi kama yale ya kule Kibiti.

Enzi zetu sisi kaka na dada zenu tulikuwa tukikutana pamoja JKT na bila kujali tajiri au maskini au mtoto wa mkulima wote tulinyoa nywele na kuwa na madenge sawa.

JKT ndipo ndipo misingi ya umoja, amani na upendo baina ya wana wa nchi inapojengwa.

Wengine wanaobadilika kama tunaowaona leo hii na wamepitia JKT ni kwa kudanganywa na vijienti vya hapa na pale.
Huko jkt kuna pesa au ndio mlango wa ajira?!

Nchi hii hakuna HAKI na hilo ndilo tatizo kubwa, sio kutokwenda JKT.
Unampeleka mtu JKT akitoka huko hana kazi miaka 10 yuko mtaani, halafu unataka awe mzalendo, sawa hatuhamasishi ujambazi, wala uasi.

Tuambie kijana kasoma kamaliza chuo ana dgree moja, hana ajira, ana deni la mkopo, ana ndoto za maisha anayotaka yeye, hiyo JKT inamsaidia nini?! Au inamsaidiaje aishi?!

Mnataka akalime sijui, mara ajiajiri huo ni upuuzi tu, frustration zinataka solution siyo panadol.
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya J.K.T?

View attachment 1610352


Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, inafahamika vema na watanzania wengi ya kuwa lengo la kuwapeleka hawa wadogo wetu JKT ni kuwajengea uzalendo, ukakamavu pamoja na mentality ya kujitegemea.

Ninafahamu fika ya kuwa serikali haiwezi kupeleka graduates wote wa kidato cha sita kwenda mafunzo ya JKT kutokana na ufinyu wa budget, lakini inapaswa kukumbuka pia kwa kutokufanya hivyo inakuwa imetengeneza kundi lingine kuwa la vijana waliokosa fursa adhimu ya kupata mafunzo ya ukakamavu na uzalendo huko vyuoni na mtaani.

View attachment 1610365

Kuna mtoto mmoja wa mama yangu mdogo yeye hakubahatika kupata nafasi ya kuchaguliwa kwenda huko sasa kwa namna anavyogombana na baba yake kila siku ilikuwa mpaka kero.

Kijana mdogo wa kiume yeye akilala usiku kuja kuamka kesho yake basi ni saa nne au tano asubuhi. Mtoto hajui kufagia uwanja wala kufuta madirisha ya nyumbani kwao mpaka huwa ninajiuliza sasa watoto kama hao ambao ndio tunategemea watakuja kuwa taifa la kesho ndio wanakuwa lelemama kiasi hiki sijui Tanzania ya mwaka 2050 itakuwa na watu wazima wa aina gani?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu. Hakika umasikini ni m-baya.

View attachment 1610364

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya mdau
=====
Barikiwa
 
Huko jkt kuna pesa au ndio mlango wa ajira?!
Nchi hii hakuna HAKI na hilo ndilo tatizo kubwa, sio kutokwenda JKT.
Mkuu, usilazimishe ideologies zako ndio ziwe imani ya kila mtu. Wewe unaona nchi hii hakuna haki ila wapo wanaona haki ipo na inatendeka...
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya J.K.T?

View attachment 1610352


Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, inafahamika vema na watanzania wengi ya kuwa lengo la kuwapeleka hawa wadogo wetu JKT ni kuwajengea uzalendo, ukakamavu pamoja na mentality ya kujitegemea.

Ninafahamu fika ya kuwa serikali haiwezi kupeleka graduates wote wa kidato cha sita kwenda mafunzo ya JKT kutokana na ufinyu wa budget, lakini inapaswa kukumbuka pia kwa kutokufanya hivyo inakuwa imetengeneza kundi lingine kuwa la vijana waliokosa fursa adhimu ya kupata mafunzo ya ukakamavu na uzalendo huko vyuoni na mtaani.

View attachment 1610365

Kuna mtoto mmoja wa mama yangu mdogo yeye hakubahatika kupata nafasi ya kuchaguliwa kwenda huko sasa kwa namna anavyogombana na baba yake kila siku ilikuwa mpaka kero.

Kijana mdogo wa kiume yeye akilala usiku kuja kuamka kesho yake basi ni saa nne au tano asubuhi. Mtoto hajui kufagia uwanja wala kufuta madirisha ya nyumbani kwao mpaka huwa ninajiuliza sasa watoto kama hao ambao ndio tunategemea watakuja kuwa taifa la kesho ndio wanakuwa lelemama kiasi hiki sijui Tanzania ya mwaka 2050 itakuwa na watu wazima wa aina gani?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu. Hakika umasikini ni m-baya.

View attachment 1610364

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya mdau
=====
Mgambo iwe compulsory? Vijana wetu wakasote kuwa jeshi la akiba?
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya J.K.T?

View attachment 1610352


Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, inafahamika vema na watanzania wengi ya kuwa lengo la kuwapeleka hawa wadogo wetu JKT ni kuwajengea uzalendo, ukakamavu pamoja na mentality ya kujitegemea.

Ninafahamu fika ya kuwa serikali haiwezi kupeleka graduates wote wa kidato cha sita kwenda mafunzo ya JKT kutokana na ufinyu wa budget, lakini inapaswa kukumbuka pia kwa kutokufanya hivyo inakuwa imetengeneza kundi lingine kuwa la vijana waliokosa fursa adhimu ya kupata mafunzo ya ukakamavu na uzalendo huko vyuoni na mtaani.

View attachment 1610365

Kuna mtoto mmoja wa mama yangu mdogo yeye hakubahatika kupata nafasi ya kuchaguliwa kwenda huko sasa kwa namna anavyogombana na baba yake kila siku ilikuwa mpaka kero.

Kijana mdogo wa kiume yeye akilala usiku kuja kuamka kesho yake basi ni saa nne au tano asubuhi. Mtoto hajui kufagia uwanja wala kufuta madirisha ya nyumbani kwao mpaka huwa ninajiuliza sasa watoto kama hao ambao ndio tunategemea watakuja kuwa taifa la kesho ndio wanakuwa lelemama kiasi hiki sijui Tanzania ya mwaka 2050 itakuwa na watu wazima wa aina gani?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu. Hakika umasikini ni m-baya.

View attachment 1610364

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

Maoni ya mdau
=====
Hakuna kubahatika kuingia jkt kwa aliemaliza f6. Kubahatika ni kupata ulichokihitaji sana bila kutarajia. Ni wachache waitwao kwa mujibu na kwenda kwa furaha. Wanakwenda tu kwa kuwa ni sheria.
 
Mfumo wa ufundishaji ulioushauri una walakini. Hao wauza magari wanaokuja kutoa mafunzo wamethibitishwa na nani? Mwisho wa masomo yoyote uthibitisho ni cheti cha kuhitimu, kitatolewa na nani? Kuna VETA ndio watoa mafunzo kwa level za chini, washauri vijana waende huko.
 
Mkuu, usilazimishe ideologies zako ndio ziwe imani ya kila mtu. Wewe unaona nchi hii hakuna haki ila wapo wanaona haki ipo na inatendeka...
Hahaha hivyo nikubali ideology zako za kupeleka watu jkt na mgambo?!

Mawazo yangu ni yangu na yako ni yako.
Huyapendi yangu yaache, nami nisipopenda yako Natayaacha.

Jukwaa huru hili.

Usisahau kumpigia kura Tundu Lisu na CHADEMA kwa Haki, Usawa, Amani na maendeleo ya Tanzania.
 
Unampeleka mtu JKT akitoka huko hana kazi miaka 10 yuko mtaani, halafu unataka awe mzalendo, sawa hatuhamasishi ujambazi, wala uasi.

Tuambie kihana kasoma kamaliza chuo ana degree moja, hana ajira, ana deni la mkopo, ana ndoto za maisha anayotaka yeye, hiyo JKT inamsaidia nini?! Au inamsaidiaje aishi?!

Mnataka akalime sijui, mara ajiajiri huo ni upuuzi tu, frustration zinataka solution siyo panadol.
Mhhh
 
Back
Top Bottom