MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Kama kuna Mechi ambayo kwa msiojua wengi wenu kwamba Simba SC imefanyiwa kila Hila na Kampeni ya Kimkoa na Kibunge ili iziache Alama ( Points ) Tatu ( 3 ) zote pale Makao Makuu ya nchi Mkoani Dodoma basi ni hii ya leo dhidi ya Dodoma Jiji FC.
Tokea Siku ya Jumatano mpaka Alfajiri ya leo Viongozi Waandamizi wa Dodoma Jiji FC ( ambao pia ni Maseneta ndani ya Yanga SC ) bila kuwasahau Wafanyakazi baadhi wa Serikali na Manispaa pamoja na Msaidizi wa Mganga wa Yanga SC anayetawala ( trend ) mno Mitandaoni wamefanya Ushirikina ( Unyangindo ) wa kila aina katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma mpaka Kuzuia Watu wa Simba SC wasiingie ( Kasoro Jana tu ) ili wafungwe. I
Na Mkakati huu haukuishia kwa Kuroga ( Ushirikina ) zaidi bali ulihamia mpaka kwa Waamuzi ambapo kwa bahati waliyekuwa wakidhani ndiyo atakuwa Mwamuzi leo ( waliyemalizana nae ) akaishia kuwa Kamisaa huku Yule ambaye hawakuzungumza nae ( Kumshirikisha ) ndiyo akawa Mwamuzi ( Referee ) na akachezesha kwa Kujitahidi kidogo japo alikuwa akiingiliwa mno Kimaamuzi na Kamisaa ambaye alishapewa Mzigo mapema tu.
Shukran nyingi hasa ziende kwa Kocha mwenye Uchungu na Simba SC Selemani Matola pamoja na Meneja anayeipenda Simba kuliko hata Mkoa wake wa Kagera ( Bukoba ) Patrick Rweymamu ambao Kipindi cha Pili waliamua Kumshauri Kinguvu Kocha Mkuu Gomez kuwa amuingize Mshambuliaji Meddie Kagere ili Simba SC iwe na Washambuliaji Watatu wakiamini kuwa Nguvu za Kagere na Uchezaji wake ungeleta Mafanikio na kweli ikawa hivyo.
Asanteni sana Wachezaji wa Simba SC!!!
Tokea Siku ya Jumatano mpaka Alfajiri ya leo Viongozi Waandamizi wa Dodoma Jiji FC ( ambao pia ni Maseneta ndani ya Yanga SC ) bila kuwasahau Wafanyakazi baadhi wa Serikali na Manispaa pamoja na Msaidizi wa Mganga wa Yanga SC anayetawala ( trend ) mno Mitandaoni wamefanya Ushirikina ( Unyangindo ) wa kila aina katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma mpaka Kuzuia Watu wa Simba SC wasiingie ( Kasoro Jana tu ) ili wafungwe. I
Na Mkakati huu haukuishia kwa Kuroga ( Ushirikina ) zaidi bali ulihamia mpaka kwa Waamuzi ambapo kwa bahati waliyekuwa wakidhani ndiyo atakuwa Mwamuzi leo ( waliyemalizana nae ) akaishia kuwa Kamisaa huku Yule ambaye hawakuzungumza nae ( Kumshirikisha ) ndiyo akawa Mwamuzi ( Referee ) na akachezesha kwa Kujitahidi kidogo japo alikuwa akiingiliwa mno Kimaamuzi na Kamisaa ambaye alishapewa Mzigo mapema tu.
Shukran nyingi hasa ziende kwa Kocha mwenye Uchungu na Simba SC Selemani Matola pamoja na Meneja anayeipenda Simba kuliko hata Mkoa wake wa Kagera ( Bukoba ) Patrick Rweymamu ambao Kipindi cha Pili waliamua Kumshauri Kinguvu Kocha Mkuu Gomez kuwa amuingize Mshambuliaji Meddie Kagere ili Simba SC iwe na Washambuliaji Watatu wakiamini kuwa Nguvu za Kagere na Uchezaji wake ungeleta Mafanikio na kweli ikawa hivyo.
Asanteni sana Wachezaji wa Simba SC!!!