Kwanini kusini mwa Jangwa la Sahara kuna..................

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Umaskini uliokithiri....na matokeo yake kuna...
Maambukizi ya kutisha ya HIV na Ugonjwa wa UKIMWI.....MALARIA, magonjwa mengineya tropiki, utapiamlo.....elimu duni.....na mengineyo.Tukiangalia kwa undani tunapata kwamba nchi nyingi kusini mwa jangwa hili zina utajiri wa kutisha wa maliasili - ardhi yenye rutuba, hali nzuri ya hewa, madini ya kila aina, misitu , wanyama na ndege wa kila aina, maji ( mito, maziwa,bahari),mvua za kutosha.......na mengineyo mengi!
TATIZO NI NINI??????
 
africa inaitwa the last frontier........

time yetu bado.......
 
Huku ndiko kwenye neema zote za dunia hii.
Wazungu wanataka kutumaliza kisha waje kurithi nchi
Umaskini uliokithiri....na matokeo yake kuna...
Maambukizi ya kutisha ya HIV na Ugonjwa wa UKIMWI.....MALARIA, magonjwa mengineya tropiki, utapiamlo.....elimu duni.....na mengineyo.Tukiangalia kwa undani tunapata kwamba nchi nyingi kusini mwa jangwa hili zina utajiri wa kutisha wa maliasili - ardhi yenye rutuba, hali nzuri ya hewa, madini ya kila aina, misitu , wanyama na ndege wa kila aina, maji ( mito, maziwa,bahari),mvua za kutosha.......na mengineyo mengi!
TATIZO NI NINI??????
 
Ni uongozi - Good Governance

Viongozi wetu hawajaamua kuwa wazalendo wa kweli. Ila siku wakiamua kila kitu kitabadilika.
Bado tuna stand chances za kuondokana na huu umasikini uliokithiri kama viongozi wetu wataamua kufuata njia sahihi ya utawala bora.

Believe me, wanajua wanatakiwa wafanye nini ila hawataki kufanya kwa makusudi kwasababu ya maslahi binafsi. Wanaiba mpaka vitu vingine wanasahau kama ni vyao kwao na bado wanahitaji na vingine...

Ni ulafi uliopitiliza.

Mungu awasaidie siku moja wauone Mwanga na wajirudi kusaidia jamaa zao.
 
Among other things, people out there aren't smart compared to other people from the rest of the world... let us keep on watching the dynamic world
 
Hahahahaaa....tatizo ni nini? Tatizo hatuna akili. Wewe angalia Afrika Kusini ilivyoendelea. Au Afrika Kusini haipo kusini mwa jangwa la Sahara?

Licha ya utawala dhalimu dhidi ya weusi kwa miaka mingi, yale mazungu yameijenga ile nchi bana. Kuna atakayebisha kuwa kusingekuwa na wazungu Afrika Kusini ingekuwa hapo ilipo?

Ukweli wa mambo, mkubali au mkatae, Miafrika Ndivyo Tulivyo. Najua mtanipinga sana tena sana tu, lakini mtaishia kunipinga kwa maneno tu. Na tayari tunajua maneno matupu hayaleti maendeleo wala kubadilisha hali tuliyonayo.

Ni mpaka hapo tutakapoanza kuvumbua vitu na mambo ndio tutakapoendelea. Na mpaka sasa huo uwezo hatuna.
 
Matatizo ya kusini mwa Sahara yanainzia kwenye nyanja zifuatazo ;
Uongozi usio wajibika kwa wananchi
Viongozi wengi wa kusini mwa Sahara hawana tabia ya kuwajibika kwa wananchi wao, nikiorodhesha mambo machache tu kwa kuangazia hususani nchi yangu na nchi jirani,
Ufisadi, rushwa, na idhalimu wa kila namna vimeshamili na wakati mwingine vinashangiliwa na kuonekana kua ni vitendo vya kishujaa
Pia nchi nyingi zinaendwshwa kwa mfumo wa bora liende, ( ufafanuzi kwa maana ya bora liende inamaanisha unaendesha nchi na unagundua mambo fulani yanafanyika kimakosa huchukui hatua yoyote kuzuia na kurekebisha, mfano mitaala ya elimu tunayo itumia Tanzania haiendani na mazingira halisi ya maisha ya Mtanzania na hailengi kumuandaa mwanafunzi kuyatumia mazingira yake katika kuzalisha na kutoa huduma mbali mbali pindi anapo hitimu, lakini hakuna hatua zinazo chukuliwa.
UZEMBE WA WANANCHI
Wananchi wengi katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ni wazembe na hawana tabia ya kufanya kazi na kuuthamini mda wao. Kutofanya kazi na kukaa kijiweni kwa wananchi wengi wa kusini mwa jangwa la Sahara kunaonekana kua jambo la kawaida sana. Kauli ya kukosa mtaji kimekua kichaka halali kwa wao kutofanya kazi na kukaa bijiweni mda wote.
 
Tuache kuwachapa watoto wetu, waafrika wanaoishi chini ya Jangwa la Sahara IQ zao ndogo kwasababu ya kupewa adhabu kali hasa za kuchapwa utotoni
 
Back
Top Bottom