Kwanini kuna Covid za aina nyingi duniani? Na kwanini muda huu?

stakehigh

JF-Expert Member
Aug 9, 2019
6,377
3,491
Yawezekana kuna sababu kwanini kuna covid za aina nyingi ila mimi sijui, South Africa wana covid tafauti na iliopo duniani, Tanzania pia juzi kuna watu walikutwa na aina ingine ya covid!

Kwa wale mnaolewewa hizi variants zinatoka wapi , na kwanini zimekuja muda huu pia mtueleze?
 
Yawezekana kuna sababu kwanini kuna covid za aina nyingi ila mimi sijui, South Africa wana covid tafauti na iliopo duniani, Tanzania pia juzi kuna watu walikutwa na aina ingine ya covid!

Kwa wale mnaolewewa hizi variants zinatoka wapi , na kwanini zimekuja muda huu pia mtueleze?

Siamini hata kidogo kama kuna covid tofauti na hii iliyopo, navyojua covid ni hiyo hiyo isipokuwa imekuja kwa kasi zaidi, kwa maana watu wengi huugua na wengine kufa kabisa
 
Yawezekana kuna sababu kwanini kuna covid za aina nyingi ila mimi sijui, South Africa wana covid tafauti na iliopo duniani, Tanzania pia juzi kuna watu walikutwa na aina ingine ya covid!

Kwa wale mnaolewewa hizi variants zinatoka wapi , na kwanini zimekuja muda huu pia mtueleze?
Myth tu hizo na mizungu inatumia huo mwanya kuwachanganya
 
si ndo media zetu znavosema? hata ivo imefika hatua south africa wanauza dozi zao zote za astrazeneca kwa sababu hazitibu covid iliopo kwao

Au itakua laana hiyo ya mauwaji ya wageni ndio maana imegonga mwamba 🤣 haiwezekani covid iwe imekuja kivingine 🤣 haimake sense kwakweli
 
Nlisikia BBC Swahili wakielezea kuhusu virus mutation.

Wanasema Kirusi kinatabia ya kujibadilisha kikikaa mwilini muda mrefu. Utakuta mgonjwa alikuwa na Ile Covid ya China akakaa na Kirusi mwilini muda mrefu labda haoneshi dalili ama ama alichelewa kupona, Kirusi kinajibadilisha na kuunda aina nyingine. Sasa yeye akiambukiza kirusi anambukiza Aina ambayo yeye ameiunda.

That's why Kuna Brazil Mutation, South Africa, India, UK na saivi Naskia Tanzania Mutation inaamana mtu wa huko kirusi kilibadilisha mutation mwilini mwake na yeye akaambukiza wengine

Hata wagonjwa wa Ukimwi waanambiwaga hata Kama unavirusi usifanye Ngono zembe, Unaweza kwenda kupata Kirusi kingine tofauti na chako, Kikakupelekesha zaidi.

Nimejaribu kuelezea kwa nlivyo elewa labda wataalamu wa Afya watakuja kuelezea vizuri.
 
Back
Top Bottom