Kwanini Kuku alivuka barabara?

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Katika mgongano wa kifikra swali jepesi kama hilo laeza kusababisha maoni mengi na ya ajabu sana. Tangia miaka ya enzi na enzi swali hilo limekuwa likipatiwa majibu tofauti kufuatana na ni nani anayetoa jibu hilo. Ukienda kwenye blogu ya michuzi utaona jinsi watu wanavyofikiri ni jinsi gani watu mashuhuru wamejaribu kulijibu swali hilo au ni jinsi gani wangejaribu kulijibu swali hilo. Swali hili lina falsafa iliyofichika na linahusu haki, uhuru, maono, mwelekeo na mtazamo.

Wewe ukiulizwa swali hilo, unafikiri ni kwanini "kuku aliamua kuvuka barabara"?
 
- Ni wazi kuwa kuku alivuka barabara ili kwenda kutetea haki yake ya kwenda kokote na wakati wowote bila ya kuulizwa kwanini alivuka barabara!
 
Wewe ukiulizwa swali hilo, unafikiri ni kwanini "kuku aliamua kuvuka barabara"?

...kwakuwa alikuwa anatumia 'uhuru wake' wa 'kujiamulia mambo yake', ...uhuru wa 'kwenda popote' kwa 'wakati wake' bila 'kushawishiwa na yeyote', tena 'bila wasiwasi au kufikiria athari yeyote!'!
 
- Kama kuku aliona wadudu wazuri upande wa pili au alichoshwa na upande aliokuwa sisi inatuhusu nini? Yawezekana aliamua kuvuka barabara kwa sababu alikuwa ameboeka upande aliokuwapo na hivyo akaamua kufuata wadudu wazuri upande ule mwingine. Hatuna haki ya kuhoji!

Asanteni.
 
Naomba nijue swali lenyewe maana nisije jiingiza katika kuchangia wakati kiini chake hasa sikijui
 
Kuku alivuka barabara kumkimbia mwewe. Na mwewe akimfuata atavuka tena kurudi alikotoka, na kuendelea!
 
Katika mgongano wa kifikra swali jepesi kama hilo laeza kusababisha maoni mengi na ya ajabu sana. Tangia miaka ya enzi na enzi swali hilo limekuwa likipatiwa majibu tofauti kufuatana na ni nani anayetoa jibu hilo. Ukienda kwenye blogu ya michuzi utaona jinsi watu wanavyofikiri ni jinsi gani watu mashuhuru wamejaribu kulijibu swali hilo au ni jinsi gani wangejaribu kulijibu swali hilo. Swali hili lina falsafa iliyofichika na linahusu haki, uhuru, maono, mwelekeo na mtazamo ambapo "kuku" ni picha tu!! na barabara ni methali tu..

Wewe ukiulizwa swali hilo, unafikiri ni kwanini "kuku aliamua kuvuka barabara"?

Kama ndio hivyo basi bwana ngoja tuangalie ufundi wake kwa mbali.
 
Mwanakijiji, Unaposema kuku ni picha tu hapo kidogo umeondoa tamu ya msemo huu kwani itaniuwia vigumu kuiweka picha hiyo ktk character ya kuku.
Hata hivyo kuku ni ndege ambaye maisha yake yote hutazama vitu hivi:- Chakula, Usalama na ngono!
Hivyo basi inawezekana kabisa majibu yote hapo juu yakawa sawa maadam moja kati ya linapatikana upande wa pili!
 
Mie nafikiria nini kilimfika huyu kuku, kama alipigwa mzinga wakati wa kuvuka...basi alikuwa na haki ya kuangalia shoto na kulia. Kama alivuka salama, je alipata alichokitaka??. Kama hapo ni yes, je ili hitaji hiyo trouble yote?. Ni vigumu sana kujiweka kwenye position ya huyu "kuku" na maswali ni mengi kuliko majibu.
 
suala lako linategemea tunalitazama kwa kipindi cha miaka mingapi.

ikuwa kwa time frame ya miaka milioni kadhaa, kuku inawezekana akawa hajavuka barabara, ila mazingira yamebadilika kiasi cha kuwa kuku anaonekana kavuka barabara.
 
...kwa mvuto wa 'panzi' kwenye nyasi zionekanazo kijani zaidi upande wa pili (wa barabara)!
 
Alikuwa ana kiu na upande wa pili kulikuwa na maji kwenye dimbwi akavuka apate kutuliza kiu yake
 
Hao ni kuku wa mjini penye barabara.

Wa kijijini kwetu wanapopelekwa mjini, hata barabara yenyewe wanaiogopa.
 
Moja, hakuwa na upofu wa macho. Mbili, dhamira ya kutaka kubadilisha maeneo ya kutanua ilimsukuma kufanya hivyo. Tatu, hakuna aliyekuwa tayari kumsaidia kuvuka hiyo barabara.
 
kwa sababu ya ujinga wake tu, badala ya "kupaa" ambayo ni salama zaidi yeye anaamua kujikongoja tena kiuvivu uvivu wakati mbawa za "kupaa" anazo. atagongwa bure!
 
Inawezekana kuku huyu alivuka barabara kuiwahi ndege ya E.L. ambayo ilikuwa imekaa mkao waku-take off. Kitu ambacho hakujua ni kuwa mkao wa ndege hiyo ulikuwa mtego wa kumnasa kwa ajili ya mgawanyo kama alivyofanyiwa bwana sungura.
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom