Kwanini kila ndoa inayovunjika lawama anatupiwa mwanamke!!!!!

Karina

Member
Jun 17, 2011
51
16
Jamani wana MMU kuna ndoa zomevunjika nimezishuhudia zaidi ya 3 na zote ukizisikiliza kesi zao nimwanaume kutokuwa mwaminifu yaani kuwa na nyumba ndogo au kutoka na wanawake tofauti tofauti nje ya ndoa lakini cha kushangaza jamii inawahukumu hao wanawake walioachwa kuwa wameshindwa kuipalilia ndoa mara wawaambie mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake mwenyewe. sasa mimi huwa najiuliza WHY??? mwanamke tu jamani??
 
mwanamke huwa ndo nguzo ya nyumba na ndo huleta maelewano au kuharibu ... lawama zinakuwa kwa vile kashindwa kuitunza nyumba yake
 
Jamani wana MMU kuna ndoa zomevunjika nimezishuhudia zaidi ya 3 na zote ukizisikiliza kesi zao nimwanaume kutokuwa mwaminifu yaani kuwa na nyumba ndogo au kutoka na wanawake tofauti tofauti nje ya ndoa lakini cha kushangaza jamii inawahukumu hao wanawake walioachwa kuwa wameshindwa kuipalilia ndoa mara wawaambie mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake mwenyewe. sasa mimi huwa najiuliza WHY??? mwanamke tu jamani??

sababu mwanamke ndiye anayeolewa kwa kutolewa mali,hivyo ana jukumu la kuilinda,..sema jingine
 
Mfume dume Karina,malezi yetu yanamtaka mama azae na alee watoto,hivyo ikitokea kutokuelewana jamii inatarajia wazazi (hasa mama) kuweka maslahi ya watoto kwanza above everything including her personal happiness,health and welfare. Too sad Karina lakini hayo ndo mazingira tuliyokulia.
 
Mfumo dume tuliourithi na unaendelea kututafuna
Angalia hata maandiko yanasema wazi kabisa "mwanamke mwerevu huijenga nyumba kw amikono yake ila mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake" hapo haimtaji mwanaume japo mwanaume hapo anaweza kuwa ndiye mkosaji
 
Mfumo dume tuliourithi na unaendelea kututafuna
Angalia hata maandiko yanasema wazi kabisa "mwanamke mwerevu huijenga nyumba kw amikono yake ila mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake" hapo haimtaji mwanaume japo mwanaume hapo anaweza kuwa ndiye mkosaji
100% umefinalize mjadala
 
Mfume dume Karina,malezi yetu yanamtaka mama azae na alee watoto,hivyo ikitokea kutokuelewana jamii inatarajia wazazi (hasa mama) kuweka maslahi ya watoto kwanza above everything including her personal happiness,health and welfare. Too sad Karina lakini hayo ndo mazingira tuliyokulia.

Mfumo dume tuliourithi na unaendelea kututafuna
Angalia hata maandiko yanasema wazi kabisa "mwanamke mwerevu huijenga nyumba kw amikono yake ila mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake" hapo haimtaji mwanaume japo mwanaume hapo anaweza kuwa ndiye mkosaji
Sina cha kuongeza
 
Mfume dume Karina,malezi yetu yanamtaka mama azae na alee watoto,hivyo ikitokea kutokuelewana jamii inatarajia wazazi (hasa mama) kuweka maslahi ya watoto kwanza above everything including her personal happiness,health and welfare. Too sad Karina lakini hayo ndo mazingira tuliyokulia.

bad hapo majukumu ya kuitunza ndoa na nyumba yako kwa mwanamke maana wanaume kukiwa na tatizo hupenda kuzikimbia nyumba au kukimbia tatizo ... na furaha ya nyumba ni mwanamke
 
Kweli jamani, lawama zimezidi kwa wanawake.
Ndoa hadi kuvunjika unakuta mwanamke kashavumilia mengi ila bado wanatulaumu.
Waone vile!!
 
bad hapo majukumu ya kuitunza ndoa na nyumba yako kwa mwanamke maana wanaume kukiwa na tatizo hupenda kuzikimbia nyumba au kukimbia tatizo ... na furaha ya nyumba ni mwanamke

Inatokea kwamba sisi wanaume ndio tunasababisha mengi ila ni wepesi sana kukimbia majukumu maana lolote litakaloharibika ndani ya nyumba lawama zinakuwa kwa wake zetu hata kama sisi ndi wasababishi
 
Inatokea kwamba sisi wanaume ndio tunasababisha mengi ila ni wepesi sana kukimbia majukumu maana lolote litakaloharibika ndani ya nyumba lawama zinakuwa kwa wake zetu hata kama sisi ndi wasababishi

lakini sisi wanaume tunaweza kuwa ni tatizo , au wanawake ni tatizo au wote ni matatizo ... ila zigo la lawama linamwendea mwanamke kwa vile ndo mlezi
 
lakini sisi wanaume tunaweza kuwa ni tatizo , au wanawake ni tatizo au wote ni matatizo ... ila zigo la lawama linamwendea mwanamke kwa vile ndo mlezi

Kwa asilimia kubwa sisi wanaume tuna matatizo tena ndo waanzilishi wa mengi ndani ya familia ila ni wepesi sana kukwepa lawama
na vile vile ni wagumu sana kukiri madhaifu yetu na kukubali kukaa chini na kuyajadili kwenye ngazi ya familia
So wenzetu wanapovumilia wakichoka huwa wanaamua lolote na liwe au tunaporealize kuwa tuna makosa inakuwa too late wenzetu washachoka
 
Kwa asilimia kubwa sisi wanaume tuna matatizo tena ndo waanzilishi wa mengi ndani ya familia ila ni wepesi sana kukwepa lawama
na vile vile ni wagumu sana kukiri madhaifu yetu na kukubali kukaa chini na kuyajadili kwenye ngazi ya familia
So wenzetu wanapovumilia wakichoka huwa wanaamua lolote na liwe au tunaporealize kuwa tuna makosa inakuwa too late wenzetu washachoka

lakini kama ni mlezi hata mtoto akikosea huwezi kumchoka .. utatumia kila mbinu ila wengi wa wanawake hukumbilia kulaumu tu
 
lakini kama ni mlezi hata mtoto akikosea huwezi kumchoka .. utatumia kila mbinu ila wengi wa wanawake hukumbilia kulaumu tu
Mkuu nakubali uvumilivu ni muhimu sana kwenye masuala ya ndoa
Ila kuna mengine kwa kweli hayavumiliki
kuna sehem nao hawa wenzetu wanafika wanasema enough is enough wacha litokee la kutokea aondoke maana inakuwa sasa mambo anayofanyiwa yamezidi kipimo
 
Mkuu nakubali uvumilivu ni muhimu sana kwenye masuala ya ndoa
Ila kuna mengine kwa kweli hayavumiliki
kuna sehem nao hawa wenzetu wanafika wanasema enough is enough wacha litokee la kutokea aondoke maana inakuwa sasa mambo anayofanyiwa yamezidi kipimo

tatizo ni pale wanapoanza kutoa mambo nje ndo wanakutana na ushauri usiofaa .... hasa yey anapoanza kukuelezea ni lazima aonyeshe kwamba wewe ni tatizo
 
tatizo ni pale wanapoanza kutoa mambo nje ndo wanakutana na ushauri usiofaa .... hasa yey anapoanza kukuelezea ni lazima aonyeshe kwamba wewe ni tatizo

Mkuu ushawahi kukutana na situation unapofikia pooint of no return yaani kama ni ushauri ushatoa mpaka basi na kama ni kuyaongea mmeshayaongea sana ikiwamo na vikao vya ndugu na wazazi na ijapofikia hapo mhusika anakuwa hana other option zaidi ya kuamua liwalo na liwe
 
Jamani wana MMU kuna ndoa zomevunjika nimezishuhudia zaidi ya 3 na zote ukizisikiliza kesi zao nimwanaume kutokuwa mwaminifu yaani kuwa na nyumba ndogo au kutoka na wanawake tofauti tofauti nje ya ndoa lakini cha kushangaza jamii inawahukumu hao wanawake walioachwa kuwa wameshindwa kuipalilia ndoa mara wawaambie mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake mwenyewe. sasa mimi huwa najiuliza WHY??? mwanamke tu jamani??

Huo ndio mfumo DUME. kimsingi Ndoa ikivunjika wote (yaani Mume na Mke) mmechangia, lakini jamii ni mara nyingi inamhukumu mke kwa sababu kwa mujibu wa mafundisho ya mapokeo kutoka kizazi hadi kizazi, mke hutakiwa kumvumilia mume hata kama atakuwa na matatizo kiasi gani...................... Huo ndio ujinga wa ndoa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom