Kwanini Kikwete anawakwepa vijana na kukumbatia wazee?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
JK alionekana ni tumaini kubwa kwa vijana wan chi hii wakati anajitayarisha kuingia madarakani. Mapema mwezi May 2005 aliporudi Dar kutoka Dodoma baada ya CCM kumteuwa kugombea urais msafara wake wa kutoka Dar Airport kuja mjini ulikuwa na umati mkubwa wengi wao wakiwa vijana.

Wengine walilala barabarani kwa furaha na matumaini na wengine hata kudandia gari lake wakipiga kelele ‘Ajira!" Wazee hawakuonekana kabisa kufanya hivyo.

Na vivyo hivyo ilivyokuwa mikoani alipokwenda kujitambulisha, na pia wakati wa kampeni za 2005.

Leo hii JK anawakwepa vijana, anaona ni bora awakumbatie wazee. Na leo haikuwa mara ya kwanza kukutana na wazee, maana akiwa miongoni mwao anajisikia anafuraha kwani wazee hawana madai ya msingi kwake ukilinganisha na vijana.

Pia anajua akiwa miongoni mwa wazee ambao wengi wao ni wa CCM, watampigia makofi, vigelegele kwa lolote atakalolisema. Narudia, kwa lolote atakalolisema – na leo tumeona!


Vijana ambao ndiyo twaambiwa ni taifa la kesho na ndiyo wenye matatizo lukuki, JK anawaono si lolote si chochote. Hata hiyo katiba aliyozungumzia, itawahusu vijana zaidi.

Kwa nini JK sasa anawaogopa vijana na hali ndiyo walimpa kura nyingi kumwingiza madarakani.
 
Anajua wazi kwamba vijana ni bomu ambalo katika mpangilio wa sera zake, litampasukia tu kabla ya kuondoka madarakani.

Pia nakubaliana nawe alikuwa anatafuta kupigiwa makofi na shangwe, na mahali ambapo ana uhakika wa kuipata hiyo ni miongoni na wazee wa CCM tui.
 
JK ana mambo ya kiswahili tu na anafuata ushauri wa mswahili mwenzake Alhaji Mwinyi. nakumbuka wakati wa urais wa Mwinyi alipokuwa anainadi ile sera yake ya kuchangia elimu ya juu, alikutana na wazee kuwatangazia sera hiyo nao wazee hao mara moja walimpigia makofi.

Leo hii watoto wa wazeen hao wanahaha na kusaga meno kupata elimu ya juu kwa kukosa hela. Imekula kwao.
 
wale wazee weng wao kwasasa hawana lolote wanalojua na badala yake wanaangalia posho.
 
Lakini ni aibu kwa JK kutaka comfort kutoka kwa wazee -- wazee wetu hapa Tz nu muflis kabisa kimawazo. Mie nadhani angekuwa anakutana na vijana wangempa mawazo mazuri sana.
 
Wazee wengi wanamatatizo ya kumbukumbu, kwahiyo anatumia weakness hiyo maana anajua hakuna kati yao atakayetoka hapo na kukumbuka kitu.

Pia anaogopa reaction na kuzomewa, ndio maana anachukua wazee-kama uliangalia tbc wakati anahutubia, kuna mzee alionyeshwa kama mfano tu-akiwa anasinzia-fikiria huko back bench waliokuwa mbali na camera hali ilikuwaje
 
Vijana hawatabiriki. Hujawahi kusikia 'ujana maji ya moto?' Hata J.K Nyerere alitumain sana kwa wazee.

Tatizo J.K amewapa uhuru uliopitiliza.N

AOMBA AJARIBU UDIKITETA WALAU KWA WIKI 1. TAFADHAL J.K NAKUOMBA SANA.
 
Sababu ni vijana hawadanganyiki na pilau,

Ni-log off au ni stay on line? Nishauri pls.
 
Wazee wa CCM Dar hawana tofauti na wabunge wa CCM walioko mjengoni Dodoma,kwa maana ingine wabunge wa CCM ni kama wazee wa CCM wa mkoa wa Dari lisilo Salama,wote wana sifa zinazofanya,kushangilia ujinga,kusahau yaliyosemwa,kujifanya wako dunia ingine(Sintojua),wanajifanya wanampenda sana mkulu na mkulu ni wao peke yao,wote wanampaka mafuta ya mgongo mkulu kwa kumsifia ''suti ''aliyovaa.

Hebu angalia wabunge wa CCM wanavyojadili mambo ya katiba,je wanatofauti gani na hawa wazee ngumbaro wa Dar,ambao uwezo wao wa kufikiri ni kufikiri watapata wapi kahawa na kashata
 
Mh nimekwazwa na mkutano wa jana, Hivi ulikuwa wa Rais na wazee wote au wazee wa CCM? Sasa kauli za CCM HOYEE,na CCM, CCM zilikuwa za nini Rais wangu? Hawa wazee wajifunze utaifa pale rais anaposimama kama Rais na sio mwenyekiti wa Chama.

Pili lini Rais atakutana na VIJANA PIA mbona kila mara Wazee wazee tu tena wanaoonyesha unafiki wa hali ya juu? Tukumbuke wazee hawa ndio waliotufikisha hapa tulipo.

Tatu mbona wazee wa Dar es salaam tu naomba akutane pia na wazee wa MBEYA, MWANZA, ARUSHA, MOSHI etc kama kweli anaheshimu Taifa hili. NAWASILISHA.
 
Mwoga na siku zote wanawachukua wazee ambao hawawezi kumchallenge, wale wazee nina wasiwasi watakuwa wametoka mikoani huko na kazi yao ni kushangilia CCM tu pale ioneshe kwamba wazee wanamkubali mkuu wa nchi kwa mgongo wa chama, ni kosa lile, haitakiwi kufanya, Rais asimame kama Rais!
 
Nimefuatilia Hotuba ya Ndg Mr. president Kikwete nimegundua kuwa yeye na washauri wake ikiwa pia na chama chake wemeshindwa kumshauri ni wapi aongelee mambo ta Kitaifa na ni kundi gani linaguswa na jambo husika.

Katiba hii tutakayopambana kufa au kupona ili iwe inayokidhi matakwa ya Watanzania ( VIJANA) na sio wazee wa CCM na tena wale wa Dar tu kama tulivyowaona wanasinzia wakati wa hutuba ya Mr.President.Yawezaka pia kuwa wazee hao wanafikili kuwa bado Tanzania ni CCM tu kwani walikuwa wanasikika wakiimba CCM kila Mr. President waliposema neno na kusahau kuwa CCM ITAKUFA kabisa baada ya uchaguzi 2015. Nionavyo mimi wale wazee wa Dar anaowatumia Mr. President kutokana na Umri wao miaka minne iliyobaki ya kikwete na hata kabla ya kupatikana kwa katiba mpya Umri wao kwa mjibu wa maandiko matakatifu hautawaruhusu kuwa na nguvu ya hata kutembea bila mikongoja ( sitaki niwatabilie uwepo wao duniani). kwa Ufupi katiba ijayo ni ya VIJANA na kamwe si wazee tena kama CCM wanavyojidanganya.

Hata hivyo Mr. President na serkali yake wanajua walivyolisahau kundi kubwa hili la vijana na kuendelea na kundi la wazee ambao wanajua muda wao ni mchache sana.

Vijana KUWENI macho na hili na msikubali kabisa na kwa wenye hakili za utambuzi wa mambo ya political Kipropaganda utagundua tu kuwa hizi ni mbinu zilizopitwa na wakati za kungangania wazee na kuwaacha VIJANA wakitaabika...

Hii inaitwa political Miscalculation na matokeo yake yataonekana ni swala la Muda tu Ndg Mr. President.
 
pale Nkrumah hall alipaweza hayati mwalimu tu..iwapo hoja za mbali hazijibiki je zile zapapo kwa papo si itakuwa shuhuli?
 
kakusanya wazee wa watu maskini......wanasinzia tu.
angekuwa anawahurumia wazee hao, angewalipa
madai yao wale wastaafu wa EAC.
 
Swali langu ni kutaka kuja kama Rais wetu anatutendea haki sisi vijana wa Tanzania.?
1- Kwanini Rais anapenda tu kuongea na wazee na siyo vijana.?
2- Je kwenye hotuba zake sijawahii sikia akitaja mkakati wa kusaidia vijana hapa nchini.?
 
Haya ndiyo yaliyomkatisha tamaa..!!!!!!!!!! IMG_4545.jpg ..............................:croc:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom