Kwanini kambi ya upinzani ilikuwa imenuna wakati bajeti inasomwa bungeni?

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Bunge letu lina wabunge wa kambi ya upinzani kutoka vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.

Ikumbukwe kuwa CCM ina wabunge 276, CHADEMA ina wabunge 72, CUF 42, NCCR-Mageuzi 1 na ACT-Wazalendo 1.

Wakati hotuba ya bajeti inasomwa bungeni, mbunge wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alikuwa nje ya nchi.

Kilichonishangaza zaidi, wabunge wa upinzani hawakupiga hata makofi(meza) wakati Maboresho ya Mfumo wa Kodi, Ada na Tozo Mbalimbali zilipokuwa zinasomwa.

Ikumbukwe kuwa maboresho hayo yametokana kwa kiasi kikubwa na hoja za hao hao wapinzani ambao walizitoa mwaka jana na pia mwaka huu katika hotuba na mijadala kwa Wizara ya fedha na mipango.

Kwa mfano, mwaka jana wapinzani walipiga kelele sana kuhusu Kodi ya Ongezeko la Thamani katika huduma zinazotolewa kwenye usafirishaji wa bidhaa/mizigo nje ya nchi (ancillary transport services). Katiba bajeti hii, kodi hiyo imeondolewa.

Kodi nyingine iliyokuwa inalalamikiwa sana na wapinzani ni kodi ya Mwaka ya Leseni ya Magari (Annual Motor Vehicle Licence Fee) iliyokuwa inalipwa hata kwa magari ambayo hayatumiki. Kwa sasa kodi hiyo imefutwa na badala yake hiyo itatozwa kwa magari yanayotembea tu na italipwa mara moja tu pale gari linaposajiliwa. Mbunge Msigwa wakati akiungana na baadhi ya wabunge wa CCM kutoa mapendekezo haya ya kuitaka serikali ihamishie kwenye mafuta alishangiliwa sana na kambi ya upinzani.

Sehemu nyingine iliyokuwa inalalamikiwa sana ni serikali kutokufahamu vizuri kiasi gani cha madini kinasafiriswa nje ya nchi. Kwa sasa serikali imeamua kutoruhusu usafirishaji wa madini kutoka migodini na kupeleka moja kwa moja nje ya nchi. Aidha, Serikali itaanzisha maeneo maalum (clearing houses) katika viwanja vya kimataifa, migodini, na kadhalika ambapo madini hayo yatathibitishwa na kupewa kibali cha kusafirisha madini hayo ambacho kitatozwa ada ya asilimia moja (clearing fee) ya thamani ya madini hayo.

Kitu kingine kilichoanzishwa na serikali kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye bidhaa za mtaji (capital goods) ili kupunguza gharama za ununuzi/uagizaji wa mashine na mitambo ya kuzalishia.

Serikali imeamua pia kupunguza kiwango cha kodi ya Mapato ya Makampuni (Corporate Income Tax) kutoka asilimia 30 mpaka asilimia 10 kwa miaka mitano kuanzia mwaka mwekezaji atakapoanza uzalishaji, kwa waunganishaji (assemblers) wa magari, matrekta na boti za uvuvi.

Kutotozwa pia ushuru kwa mtu anayesafirisha mazao yake kutoka Halmashauri moja kwenda nyingine yasiyozidi tani moja (1) na pia kupunguzwa kwa ushuru wa mazao (produce cess) kwa sasa yatatozwa asilimia 2

Haya yote wakati yanasomwa na Waziri wa Fedha na Mipango, wabunge wa kambi ya upinzani walikuwa wamenuna huku nyuso zao zikionekana kusononeka.

Mimi kama mwananchi wa kawaida nikajiuliza, hawa wabunge wa upinzani hawakuona hata jema moja katika hii bajeti hasa ikichukuliwa kuwa baadhi ya yale waliyokuwa wanayapigia kelele yamefanyiwa kazi?

Kwa nini wanaonekana kusononeka wakati hata baadhi ya madai yao yamekubaliwa?

Kwa vielelezo msikilize kwenye video Mbunge Peter Msigwa alivyosema na kushangiliwa na wabunge wa upinzani kuhusu kodi ya mwaka ya leseni ya magari.

Kwa wenye bando dogo anzia kuangalia video dakika ya 8:30.

VIDEO:
 
Bunge letu lina wabunge wa kambi ya upinzani kutoka vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.

Ikumbukwe kuwa CCM ina wabunge 276, CHADEMA ina wabunge 72, CUF 42, NCCR-Mageuzi 1 na ACT-Wazalendo 1.

Wakati hotuba ya bajeti inasomwa bungeni, mbunge wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alikuwa nje ya nchi.

Kilichonishangaza zaidi, wabunge wa upinzani hawakupiga hata makofi(meza) wakati Maboresho ya Mfumo wa Kodi, Ada na Tozo Mbalimbali zilipokuwa zinasomwa.

Ikumbukwe kuwa maboresho hayo yametokana kwa kiasi kikubwa na hoja za hao hao wapinzani ambao walizitoa mwaka jana katika hotuba ya bajeti.

Kwa mfano, mwaka jana wapinzani walipiga kelele sana kuhusu Kodi ya Ongezeko la Thamani katika huduma zinazotolewa kwenye usafirishaji wa bidhaa/mizigo nje ya nchi (ancillary transport services). Katiba bajeti hii, kodi hiyo imeondolewa.

Kodi nyingine iliyokuwa inalalamikiwa sana na wapinzani ni kodi ya Mwaka ya Leseni ya Magari (Annual Motor Vehicle Licence Fee) iliyokuwa inalipwa hata kwa magari ambayo hayatumiki. Kwa sasa kodi hiyo imefutwa na badala yake hiyo itatozwa kwa magari yanayotembea tu na italipwa mara moja tu pale gari linaposajiliwa.

Sehemu nyingine iliyokuwa inalalamikiwa sana ni serikali kutokufahamu vizuri kiasi gani cha madini kinasafiriswa nje ya nchi. Kwa sasa serikali imeamua kutoruhusu usafirishaji wa madini kutoka migodini na kupeleka moja kwa moja nje ya nchi. Aidha, Serikali itaanzisha maeneo maalum (clearing houses) katika viwanja vya kimataifa, migodini, na kadhalika ambapo madini hayo yatathibitishwa na kupewa kibali cha kusafirisha madini hayo ambacho kitatozwa ada ya asilimia moja (clearing fee) ya thamani ya madini hayo.

Kitu kingine kilichoanzishwa na serikali kusamehe Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye bidhaa za mtaji (capital goods) ili kupunguza gharama za ununuzi/uagizaji wa mashine na mitambo ya kuzalishia.

Serikali imeamua pia kupunguza kiwango cha kodi ya Mapato ya Makampuni (Corporate Income Tax) kutoka asilimia 30 mpaka asilimia 10 kwa miaka mitano kuanzia mwaka mwekezaji atakapoanza uzalishaji, kwa waunganishaji (assemblers) wa magari, matrekta na boti za uvuvi.

Haya yote wakati yanasomwa na Waziri wa Fedha na Mipango, wabunge wa kambi ya upinzani walikuwa wamenuna huku nyuso zao zikionekana kusononeka.

Mimi kama mwananchi wa kawaida nikajiuliza, hawa wabunge wa upinzani hawakuona hata jema moja katika hii bajeti hasa ikichukuliwa kuwa baadhi ya yale waliyokuwa wanayapigia kelele yamefanyiwa kazi?

Kwa nini wanaonekana kusononeka wakati hata baadhi ya madai yao yamekubaliwa?
Ile bajeti iliyopitishwa mwaka jana imetekelezwa kwa asilimia ngapi?
Je hii bajeti mpya itatekelezwa kwa asilimia ngapi?

Hili la kusononeka au kufurahi kwa wapinzani sio "issue".

Je bajeti hii mpya inaimarishaje uchumi wa mlalahoi? Kwa sababu ile bajeti inayoisha imewatumbua walalahoi kweri kweri.
Mshauri Mkulu aitishe uchaguzi mkuu kwa haraka kama yule mama wa UK ili wapinzani wazidi kusononeka! ;):D
 
Bongo upinzani utabaki upinzani tu. Wabunge wa kambi ya upinzani hawataki kabisa kuonesha wanafurahishwa na utendaji wa serikali hata chembe kidogo. Kwa tanzania kambi ya upinzani na kambi ya chama tawala ni kama paka na panya.

ikitokea kambi ya chama tawala au serikali kwa ujumla inafanya vizuri na wananchi wanakubali kinachofanyika wapinzani wao kama sio kutafuta vijisababu chokonozi ii kutibua mchakato thabiti basi wataamua kukaa kimya tu, kama sio kutoka nje ya ukumbi wa bunge. Kwao wanaamini upinzani ni kupinga kila kitu kinachofanywa na chama tawala.

Kwa kifupi wabunge wa kambi ya upinzani siku zote wanaiombea mabaya serikali. Wanadhani serikali ikiboronga ni ahueni kwao. La hasha. Kuboronga kwa serikali ni kadhia kubwa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Nchi ikishaenda mlama ni aibu kwa wanasiasa wote, wa chama tawala na upinzani. Mantiki yangu hapa ni kwamba kufeli kwa serikali ni kufeli kwa kambi ya upinzani, kwani kazi kubwa ya chama cha upinzani ni kukosoa serikali pale inapokosea, kutoa maoni ya kipi kilicho bora kifanyike na kupongeza pale panapostahili.

Kwa huu mtindo wa kambi ya upinzani kususia susia ni kudidimiza maendeleo ya nchi, kidemokrasia na kiuchumi. Mpinzani anaposusa na kuishia kulalamika kwa kila lifanyikalo pasipo kujenga hoja endelevu ni sawa na kuwa na upinzani usio na meno, kiasi cha kukifanya chama tawala kufanya kitakacho, eidha kwa kukomoa upinzani au kwa kuamini upinzani hauna hoja endelevu.

kambi ya upinzani ibadilike sasa -ikue kidemokrasia. Demokrasia ni kujenga hoja na kama malumbano yanatokea basi yawe marumbano ya hoja, sio malumbano ya hulka na kejeli.
 
Ile bajeti iliyopitishwa mwaka jana imetekelezwa kwa asilimia ngapi?
Je hii bajeti mpya itatekelezwa kwa asilimia ngapi?

Hili la kusononeka au kufurahi kwa wapinzani sio "issue".

Je bajeti hii mpya inaimarishaje uchumi wa mlalahoi? Kwa sababu ile bajeti inayoisha imewatumbua walalahoi kweri kweri.
Mshauri Mkulu aitishe uchaguzi mkuu kwa haraka kama yule mama wa UK ili wapinzani wazidi kusononeka! ;):D
Mkuu nimeainisha mapendekezo yaliyosomwa na Waziri ambayo utekelezaji wake unaanza mara moja.

Hoja ya kuuliza mwaka jana serikali imetekeleza mangapi ni hoja ambayo haina mashiko katika maeneo niliyoainisha.
 
.Unashangilia bajeti isiyoendana na unacho kusanya.Deni la taifa linazidi kukua ila bajeti haionyeshi ni mkakati upi waliona kupunguza madeni.Hiyo misamaha unayoshingili mingi hamgusi mwananchi wakaida moja kwa moja ila mafuta yanayogusa watu moja kwa moja wamekaba wewe kwako sio tatizo.
 
Ni mtu wa ajabu tu ndie anaweza kushangilia baada ya kusomwa "...mwaka ujao wa fedha tunaondoa motor vehicle license na badala yake ushuru huo utapatikana kwenye mafuta ambapo, petroli itapanda kutoka Sh. X to Sh. X+n, diesel from Sh. Y to Y+n na mafuta ya taa from Sh. Z to Z+n!"

Ni yeye tu ndie anaweza kushangilia jambo kama hilo!!!!

Kwanini motor vehicle license iwe replaced na kupanda kwa kodi ya mafuta?! Au wanashangilia kwa sababu ni wao ndio walikuwa wanalipa hiyo motor vehicles licence kwa sababu ndio wanaomiliki magari lakini hivi sasa wanajua kama ni mafuta basi hata mkulima wa kijijini nae atalazimika kulipia in other way round?!

Yale yale ya JK!! Uchakachuaji wa petrol ukawa treated na kupandisha kodi kwenye mafuta ya taa!! Yaani uzembe wa serikali kushindwa kuwadhibiti wachakachuaji wa petrol zigo lake wakaenda kuwabebesha maskini wanaotegemea mafuta ya taa!

Mbunge yeyote anayetetea maslahi ya wananchi walio wengi katu asingepiga makofi kwa jambo kama hilo!!!!
 
Ni zuzu tu ndie anaweza kushangilia baada ya kusomwa "...mwaka ujao wa fedha tunaondoa motor vehicle license na badala yake ushuru huo utapatikana kwenye mafuta ambapo, petroli itapanda kutoka Sh. X to Sh. X+n, diesel from Sh. Y to Y+n na mafuta ya taa from Sh. Z to Z+n!"

Ni zuzu tu ndie anaweza kushangilia jambo kama hilo!!!!

Kwanini motor vehicle license iwe replaced na kupanda kwa kodi ya mafuta?! Au wanashangilia kwa sababu ni wao ndio walikuwa wanalipa hiyo motor vehicles licence kwa sababu ndio wanaomiliki magari lakini hivi sasa wanajua kama ni mafuta basi hata mkulima wa kijijini nae atalazimika kulipia in other way round?!

Yale yale ya JK!! Uchakachuaji wa petrol ukawa treated na kupandisha kodi kwenye mafuta ya taa!! Yaani uzembe wa serikali kushindwa kuwadhibiti wachakachuaji wa petrol zigo lake wakaenda kuwabebesha maskini wanaotegemea mafuta ya taa!

Mbunge yeyote anayetetea maslahi ya wananchi walio wengi katu asingepiga makofi kwa jambo kama hilo!!!!

Mkulima wa kijijini hatumii usafiri?
 
Bongo upinzani utabaki upinzani tu. Wabunge wa kambi ya upinzani hawataki kabisa kuonesha wanafurahishwa na utendaji wa serikali hata chembe kidogo. Kwa tanzania kambi ya upinzani na kambi ya chama tawala ni kama paka na panya. ikitokea kambi ya chama tawala au serikali kwa ujumla inafanya vizuri na wananchi wanakubali kinachofanyika wapinzani wao kama sio kutafuta vijisababu chokonozi ii kutibua mchakato thabiti basi wataamua kukaa kimya tu, kama sio kutoka nje ya ukumbi wa bunge. Kwao wanaamini upinzani ni kupinga kila kitu kinachofanywa na chama tawala.
Kwa kifupi wabunge wa kambi ya upinzani siku zote wanaiombea mabaya serikali. Wanadhani serikali ikiboronga ni ahueni kwao. La hasha. Kuboronga kwa serikali ni kadhia kubwa kwa wananchi na taifa kwa ujumla. Nchi ikishaenda mlama ni aibu kwa wanasiasa wote, wa chama tawala na upinzani. Mantiki yangu hapa ni kwamba kufeli kwa serikali ni kufeli kwa kambi ya upinzani, kwani kazi kubwa ya chama cha upinzani ni kukosoa serikali pale inapokosea, kutoa maoni ya kipi kilicho bora kifanyike na kupongeza pale panapostahili.
Kwa huu mtindo wa kambi ya upinzani kususia susia ni kudidimiza maendeleo ya nchi, kidemokrasia na kiuchumi. Mpinzani anaposusa na kuishia kulalamika kwa kila lifanyikalo pasipo kujenga hoja endelevu ni sawa na kuwa na upinzani usio na meno, kiasi cha kukifanya chama tawala kufanya kitakacho, eidha kwa kukomoa upinzani au kwa kuamini upinzani hauna hoja endelevu.
kambi ya upinzani ibadilike sasa -ikue kidemokrasia. Demokrasia ni kujenga hoja na kama malumbano yanatokea basi yawe marumbano ya hoja, sio malumbano ya hulka na kejeli.
Siasa za Tanzania zinashangaza kweli.

Ni kama wapinzani wanatoa mapendekezo ya kinafiki kama walivyofanya kwa CCM kuhusu Lowassa halafu baada ya CCM kumtosa wakamkimbilia haraka haraka na kuwa mgombea wao wa Urais wa Tanzania.

Wapinzani walisema Lowassa hafai hata kuchukua fomu za kugombea Urais achilia mbali kuwa kwenye mchujo wa wagombea Urais wa Tanzania.
 
Mkuu ninashangaa unaandika kama vile unanifahamu wakati hunifahamu.

Hivyo vikao unavyovisema ulivianzisha wewe? Kama hukuanzisha, umejuaje kama kuna vikao?

Kwani kuna sheria au taratibu hapa Jamiiforums zinazonitaka kutokusemea hapa?
Mkuu wasikutie roho joto hao.
 
wa
Siasa za Tanzania zinashangaza kweli.

Ni kama wapinzani wanatoa mapendekezo ya kinafiki kama walivyofanya kwa CCM kuhusu Lowassa halafu baada ya CCM kumtosa wakamkimbilia haraka haraka na kuwa mgombea wao wa Urais wa Tanzania.

Wapinzani walisema Lowassa hafai hata kuchukua fomu za kugombea Urais achilia mbali kuwa kwenye mchujo wa wagombea Urais wa Tanzania.
Wanaamini kila wakisemacho na kukifanya ni sahihi na wanalazimisha wananchi waamini kila kitokacho kwao ni bora.
Kwa kweli kwenye issue ya Lowassa walitia aibu ya karne. ilionesha ni jinsi gani kambini kwao hawana kamanda wa kusimama kwenye uwanja wa mapambano
 
Walikuwa Bado wana majozi ya msiba
Mmmh! Sidhani kama ni kweli.

Mbona niliwaona kwenye msiba wa Marehemu Philemon Ndesamburo walikuwa wanatoa 'mapovu'' baada ya bunge kupitisha azimio la kuwazuia Mdee na Bulaya kuhudhuria kwenye vikao vya bunge.
 
Mtu mwelewa hawezi ifurahia budget inayopeleka maumivu kwa wananchi kwa kupandisha bei ya mafuta. Wanajua shubiri iliyomo japo kwa juu imepakwa asali. Walinuna kwa sababu ya kuwahurumia wananchi wanaobebeshwa mzigo mkubwa kupita uwezo wao.
 
Mtu mwelewa hawezi ifurahia budget inayopeleka maumivu kwa wananchi kwa kupandisha bei ya mafuta. Wanajua shubiri iliyomo japo kwa juu imepakwa asali. Walinuna kwa sababu ya kuwahurumia wananchi wanaobebeshwa mzigo mkubwa kupita uwezo wao.
Pengine ungesoma vizuri mada iliyo mezani. hao hao walionuna walipendekeza yafanyika haya mwaka jana
 
Back
Top Bottom