Kwanini Ikulu yetu ya Tanzania (Magogoni) isiwe chanzo cha Utalii Kwa Dar kuliko kuwekwa kwa usiri mzito?

mahingah

Senior Member
Oct 4, 2016
199
275
Nina miaka miwili toka nifike hapa Dar kikazi,kitu ambacho nilikuwa na ndoto ya kuja kukiona na kupiga picha ni Ikulu ya Dar es salaam(white house), lakini nilicho kishuudia ni usiri wa hali ya juu hadi kuweka mabati usiweze kuona ndani wakati Kwa wenzetu Kama Marekani ikulu imekuwa Kama kivutio cha utalii. Watu hutoka sehemu mbalimbali kwenda kuona na kupiga picha, Mimi sijapenda coz Tanzania ni nchi ya amani

1519993861013.jpg
 
Yaani ikulu uigeuze sehemu ya kupunguzia stress zako? Nenda kwa hao "wenzako" unaowasifu.
 
Mwafrica mtu mweusi ni tofaut na mzungu aliye starabika miaka mingi.

Usifananishe mambo ya mbele na African, watu wataanza kukojoa, kutupa makopo hapo hapo Ikulu wakienda kupiga picha.
 
Mwafrica mtu mweusi ni tofaut na mzungu alie starabika miaka mingi,

Usifananishe mambo ya mbele na African, watu wataanza kukojoa, kutupa makopo hapohapo ikulu wakienda kupiga picha
Siku hzi tumestarabika sana.
 
Italii gani sasa apo. Cha msingi ifanywe tu hta gest house tuwe tunapata pesa. Au wafanye hostel ya CBE
 
Yah Bado ipo kupitia kule Kwa nyuma Obama road,haurusiwi kupita,mm nilitaka kupita hata nipige picha Kwa nyuma nikakutana na wazee wa kazi
Mambo yanabadilika, tuliwahi kukatiza hapo kipindi cha 2017 tukapunga upepo, wakati wa kugeuka kuna walinzi wa kule nje wakatusimamisha wakawa wanatupigisha stori kimtindo.
 
Mambo yanabadilika, tuliwahi kukatiza hapo kipindi cha 2017 tukapunga upepo, wakati wa kugeuka kuna walinzi wa kule nje wakatusimamisha wakawa wanatupigisha stori kimtindo.
Ww jamaa unbahati sana,ukuchukua hata picha za ukumbusho,nitumie
 
Afrika rais amegeuzwa kuwa nusu mungu ambaye wananchi either wanamwabudu au wanalazimishwa kumuabudu. lakini kwa wenzetu rais ni mtumishi wa wananchi.

Kufika ikulu Afrika sio rahisi ni sawa na kufika mbinguni maana ni makazi ya mungu wenu.
 
Yaani ikulu uigeuze sehemu ya kupunguzia stress zako? Nenda kwa hao "wenzako" unaowasifu.
Ikulu ni ofisi ya uma tatizo liko wapi ukienda hapo kupunguza stress.

Nikama enzi zetu tunasoma tulikua tukiona gari lolote la serikali hasa gari za polisi tulikua tunaomba lift hicho kitu miaka hii hakipo tena
 
Mkuu Ikulu yetu inaitwa 'State House' siyo 'White House'.
White house ni Ikulu ya Marekani.
 
Ikulu ni ofisi ya uma tatizo liko wapi ukienda hapo kupunguza stress.

Nikama enzi zetu tunasoma tulikua tukiona gari lolote la serikali hasa gari za polisi tulikua tunaomba lift hicho kitu miaka hii hakipo tena
Mwambie huyo, mimi mama yangu aliniambia miaka ya nyuma Yale mabati hayakuwekwa ulikuwa unapita kuangalia tena Kwa ukaribu tu
 
Mkuu Ikulu yetu inaitwa 'State House' siyo 'White House'.
White house ni Ikulu ya Marekani.
Asante Kwa kunijuza hilo,nilijua nayo ni white house kisa rangi yake,vp kuhusu jina la magogoni lipo sahii? Ndo jina lake?
 
Back
Top Bottom