Kwanini huwa wanaonyesha hotuba za nyerere alizotoa baada ya kustaafu tu?

ngwendu

JF-Expert Member
Jun 7, 2010
1,964
174
mwl. nyerere ametawala Tanzania kwa takriban miaka 24, lakini nimekuwa nikijiuliza, hivi ni kwa nini vyombo vya habari huwa vinatuonyesha hotuba alizotoa baada ya kung'atuka kutoka madarakani pekee? kwani nini hawatuonyeshi na zile akiwa madarakani? Msaada tafadhali. (Note; if you have no data/information you have no right to say, please nasisitiza)
 
Ndizo nasaha zenyewe huwezikutoa nasaha ukiwa bado kiongozi.sawa na baba unaposafiri la zima uache utaratibu wa kuishi hapo nyumban wakati we haupo.
 
Ni kwa sababu wakati wa uongozi wake uozo ulikuwa mkubwa, hakuwa na jipya lkn alipata nguvu kwa kukosoa ya wenzake tu. Kati ya madudu mengi yanayoliandama taifa hili mpka leo yaliasisiwa na yeye-tazama rushwa, udini (al;ikemea mdomoni moyoni ukakita kwa katoliki-soma kitabu cha padri John C. Sivalon), ufisahidi -tazama mafisadi wengi ni zao lake mwenyewe, umangimeza(alikemea mdomoni lkn yeye ikulu ilikuwa ni chaka la wazanaki, nk). Ni kawaida ya binadamu (kama nyani) kuliona la mwenzie lkn lake haliooni japo linatapisha:director:
 
Ni kwa sababu wakati wa uongozi wake uozo ulikuwa mkubwa, hakuwa na jipya lkn alipata nguvu kwa kukosoa ya wenzake tu. Kati ya madudu mengi yanayoliandama taifa hili mpka leo yaliasisiwa na yeye-tazama rushwa, udini (al;ikemea mdomoni moyoni ukakita kwa katoliki-soma kitabu cha padri John C. Sivalon), ufisahidi -tazama mafisadi wengi ni zao lake mwenyewe, umangimeza(alikemea mdomoni lkn yeye ikulu ilikuwa ni chaka la wazanaki, nk). Ni kawaida ya binadamu (kama nyani) kuliona la mwenzie lkn lake haliooni japo linatapisha:director:
asante mkuu kwa mchango. lakini unamaanisha hakuna hata hotuba moja ambayo wangekuwa wanairusha? kwani sasa hivi watuonyesha ile aliyohutubia kule uwanja wa sokoine mbeya tu na ile ya south Africa.
 
Ndizo nasaha zenyewe huwezikutoa nasaha ukiwa bado kiongozi.sawa na baba unaposafiri la zima uache utaratibu wa kuishi hapo nyumban wakati we haupo.
mkuu na maanisha hotuba alizokuwa akitoa kama mtendaji na si muangiliaji akiwa nje ya mamlaka kama tulivyo sisi. kwani sasa hivi inatupa tabu sana wengine kuamini kwani kama ni tuhuma na malalamiko mtu yeyote anaweza kuzitoa. hata kama ni mimi au wewe.
 
Siyo kwamba hotuba zake za zamani zimehodhiwa na TBCCM?! Hizi tunazoona na kusikia ni kwa sababu zilidakwa na vyombo binafsi vya habari, vinginevyo hakuna ambaye angezisikia kama zingekuwa hakimiliki ya Tbccm pekee. Nani atataka kutangaza mambo yatakayomuumbua mwenyewe?! Na kwa kiwango cha wivu na uovu wa watawala wenu, si ajabu ukakuta hotuba kibao za Nyerere zilishaaharibiwa/potezwa/tupwa kutoka maktaba ya tbccm!
 
Mi nadhani ni kutokuwa na record za video kipindi hicho, ila radio tanzania kipindi hicho ilikuwa ikitoa hotuba zake akiwa kiongozi
 
Zipo nyingi tu sema TBC wanazibania... Nimekumbuka Kitira Mkumbo alisema kuwa Television ya Taifa ni Vitendo na Si Jina pekee.... Waweke vitu wanavyohitaji kutizamwa na Watanzania sio ubabaishaji kama uliopo.... Hata Vurugu za Waislam Mbagala Kova, Mkuu wa Mkoa na Sheik Alhadi wa Dsm Walienda ITV kutoa Taarifa na Maonyo wa wanaoleta fujo waacha na wale walioathirika wasije chukua Jazba Polisi wata handle issue yote... TBC hawana uwezo wa kukatisha Muziki wa Diamond hata kukiwa na Janga la kitaifa limetokea
 
Back
Top Bottom