Uchaguzi 2020 Kwanini huu ndio Uchaguzi Mgumu zaidi kwa CCM?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Amani iwe nanyi wadau

Kama mada inavyojieleza hapo juu, hizi ndo sababu za Kwa nini Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu ndo uchaguzi Mgumu zaidi kwa CCM?

1. Mwaka 2015 Chadema walikuwa na mgombea aliyependwa na watu Lowassa Ila hakuwa mgombea makini
CCM waliweza kumchafua sana Lowassa kutokana na kashfa zakena madhaifu yake. Mwaka huu Chadema hawajarudia makosa 2020. Wana mgombea makini sana Tundu Antiphas Lissu mwenye akili sana na uwezo mkubwa sana kama mwanasiasa. Wengikwa uwezo wake wa akili na kujenga hoja wanamfananisha na Mwl Nyerere pamoja na Oscar Kambona ambao ndo wanachukuliwa kama wanasiasa bora zaidi kuwai kutokea Tanzania.

2. Mgombea wa CCM kuyaumiza makundi mengi isivyo kawaida katika kipindi chake cha miaka 5
Ni ukweli ulio dhahili kuwa kila kundi katika nchi hii limeguswa vibaya sana kwenye awamu ya tano, hali ya uchumi na kodi mbaya za TRA zimeathili sana wafanyabiashara, wafanyakazi kutopandishwa mishahara kwa miaka 5, Wakulima wa mazao kama korosho, mbaazi, tumbaku, kahawa na mahindi kuharibiwa masoko yao kwa amri za serikali pamoja na kundi kubwa la vijana kukosa ajira kutokana na uchumi kutokuwa vizuri. Kufunguliwa makesi kwa wanaharakati na watu wanaompinga magufuli pia

3. Awamu ya Tano kutokuwa na mahusiano mazuri na wadau wa maendeleo wa Tanzania wa miaka yote
Hili hata mtu asiye na akili ameliona. Katika awamu ya tano ndo Tanzania imesemwa vibaya zaidi kimataifa na hata kutolewa matamko mbalimbali yasio mazuri na ya tahadhari na balozi za hapa nchini. Hiki ni kiashiria kuwa hata wadau wa kimataifa wamemchoka Magufuli

4. Lissu kuwa Mhanga wa Jaribio la Mauaji
Hii kete ingawa CCM wanaidharau ila hili ni moja ya jambo linalombeba sana Lissu. Watu wengi wanamuona Lissu kama muujiza unaotembea. Shambulio dhidi yake tena kwenye awamu ya Tano linamfanya awe rahisi kueleweka kwa watu na hata watu kumpenda zaidi.

5. Hali ya uchumi
Hali ya uchumi ya Tanzania imekuwa mbaya sana hasa kwa watanzania. Wengi maisha yao yamezidi kuwa magumu zaidi ukiangalia kama wakulima, wafanyakazi na vijana. Hawaoni ahueni mbele na wengi wanaona ni ngumu hali hii Kubadirika kwa aina ya utawala wa magufuli

Nimalize kwa kusema, katika survey yangu Kuna jambo kuu nimeliona. Kuna uwezekano mkubwa sana Watanzania wakaandika historia kuu mwaka huu. Tundu Antiphas Lissu anaenda kuishangaza dunia mwaka huu.

Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020-2025 ni Tundu Antiphas Lissu.
 
Uliyoyaandika na kutabiri ni kweli kabisa, nilitegemea ngome ya Geita na CHato jamaa asingekuwa na ufuasi mkubwa, ila kwa niliyoyaona hizo sehemu ni wazi kuwa Lissu hana mpinzani.

Magufuli atamshinda Lissu mikoa michache sana (Dodoma, Tabora, Pwani), mikoa kama Mwanza, Geita, Shinyanga watagawana 50/50, ila kwa mikoa iliyobakia pamoja na znz sioni wa kumshinda Lissu.
 
6. Wateule wake wamekuwa waliotumbuliwa kila siku hivyo wanaona akiteuliwa tena kazi ya kuwatumbua iko pale pale,hawampi ushirikiano
Na Hii ni moja ya nguzo kuu ya kuanguka kwa Magufuli mwaka huu

Magufuli ana weakness ya kutokuwa loyal kwa wateule wake Ila yeye anataka wawe loyal kwake.

Kuanzia kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hadi kwingine korte hakuna mwenye uhakika na ajira yake hivyo hata wao hawataona shida kumgeuka mwishoni.
 
Amani iwe nanyi wadau

Kama mada inavyojieleza hapo juu, hizi ndo sababu za Kwa nini Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu ndo uchaguzi Mgumu zaidi kwa CCM?...

Kama una akili timamu ukafanya survey na umekuja na hili hitimisho

Hakuna namna umefanikiwa kwa lolote katika maisha yako, you are average person na haupendi ukweli

TL ataweka platform nzuri na mwaka 2025 CCM itakuwa na wakati mgumu sana kuliko kawaida

Mwaka huu hakuna miujiza ndugu

Pole
 
Kama ingekuwa hivyo kwenye eneo hilo wanasaccos wako wengi vijana hao wasingebeba mabango na kuzomea hivyo. Haitaji akili ya chuo kuelewa hicho. Endelea kujichekesha kama zuzu lakini tarehe 28/10/2020 ndiyo utajua ukweli na hali halisi ya mambo kuliko propaganda zenu na kucheza na video clips zenu.
Nimekwambia next time andaaa hata camera nyingi. Alafu mbona ukichukua vijana wachache sana??? Hukupewa mpunga wa kutosha na polepole nini???!

Maana hao wahuni wasiozidi 20 huwezi fananisha na maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Geita waliompokea shujaa wao Tundu Antiphas Lissu kwa bashasha kubwa!!
 
Kama una akili timamu ukafanya survey na umekuja na hili hitimisho

Hakuna namna umefanikiwa kwa lolote katika maisha yako, you are average person na haupendi ukweli...
CCM ina wakati mgumu mwaka huu kwa sababu ya aina ya mgombea wao ( Ubabe, uzandiki na ufedhuli)
CCM wakiwa na mgonjwa aina ya January Makamba hoja za Tundu Lissu za uhuru na haki haziwezi pata nguvu sana kama zinavyopata nguvu dhidi ya Magufuli.

Magufuli sio mtu wa haki Ndo mana ni rahisi sana kuwatoa CCM mwaka huu kuliko kipindi chochote kile
 
Huu sio uchaguzi mgumu kwa CCM bali uchaguzi muhimu sana kwa CCM, haswa upande wa ubunge kuna kura zinahitajika za kutosha bungeni tuna jambo letu muhimu, moja hio

Pili, huu ni uchaguzi wa aibu sana kuwahi kutoka CHADEMA, Lowasa aliingia na asilimia 18% ya wapiga kura CHADEMA, kutokuepo kwake basi ni kutokuepo kwa asilimia 18 ya matokeo pia! na sio maneno yangu amesema mwenyewe mgombea



kama mwaka 2015, mlipata 42%, mkiwa na nyongeza ya asilimia 18 ya lowasa, mnategemea kura ngap saahv lowasa akiwa hayupo? toa apo muungano wa vyama vilivowaboost, unapata < 20%, act wazalendo wamekua na attention sana, nccr mageuzi imejaza wanachama wapya wa kutosha, cdm imepoteza wanachama wengi toka mwaka uanze, hesabu za haraka haraka apo utajua mnatoka na ngap
 
Yaani mahaba ni hatari. Yaani Mwanza na Geita wagawane 50 50,hauko serious. Ila una haki kuamini unachokiamini. Subiri tarehe 28/10/2020 uone mambo yatakavyokuwa. Ila nakutaarifu uchaguzi huu kwa JPM ni rahisi sana kuliko wa 2015.
Uliyoyaandika na kutabiri ni kweli kabisa, nilitegemea ngome ya Geita na CHato jamaa asingekuwa na ufuasi mkubwa, ila kwa niliyoyaona hizo sehemu ni wazi kuwa Lissu hana mpinzani. Magufuli atamshinda Lissu mikoa michache sana (Dodoma, Tabora, Pwani), mikoa kama Mwanza, Geita, Shinyanga watagawana 50/50, ila kwa mikoa iliyobakia pamoja na znz sioni wa kumshinda Lissu.
 
huu sio uchaguzi mgumu kwa ccm bali uchaguzi muhimu sana kwa ccm, haswa upande wa ubunge kuna kura zinahitajika za kutosha bungeni tuna jambo letu muhimu, moja hio...
Amini amini nakwambia. Mshindi wa uchaguzi huu wa mwaka huu na Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020- 2025 ni Tundu Antiphas Lissu!

Hilo jambo lenu mnalotaka kulifanya bungeni la kubadiri katiba na kumuongezea muda wa kuongoza magufuli ndo limewashtua watu wengi hadi wana CCM wenye akili ambao wameamua mwaka huu lolote na liwe Magufuli harudi tena ikulu.

Hakuna wa kumbeba magufuli mwaka huu. Mwambie aandanze tu kupaki vitu vyake hapo chamwino
 
Wanaccm wenyewe wanajuta sijui walipata wapi huyo mgombea wao. Hali ya maisha kea watanzania ni ngumu kuliko mwaka 1974.


umesoma ukaelewa lakini? tunajuta ama tunataka kura za kutosha bunge jipya linaloanza? hujui anatakiwa kua raisi wa milele? uchaguzi mdogo sana huu, lakini umuhimu wake ni kura za kupitish mswada mpya, isingekua ivo basi hata kampeni hakuna haja ya kufanya
 
Amini amini nakwambia. Mshindi wa uchaguzi huu wa mwaka huu na Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020- 2025 ni Tundu Antiphas Lissu!...
wewe endelea kusema amini uchaguzi huu raisi ni huyo shoga wenu statistics huna, unadhan kura za 2015 ztajiongeza eeh! sasa subiria izo kura zenu <20, inaonekana hujui statistics we endelea na izo kauli zenu za amini nakwambia 😂 😂 😂
 
umesoma ukaelewa lakini? tunajuta ama tunataka kura za kutosha bunge jipya linaloanza? hujui anatakiwa kua raisi wa milele? uchaguzi mdogo sana huu, lakini umuhimu wake ni kura za kupitish mswada mpya, isingekua ivo basi hata kampeni hakuna haja ya kufanya
Watanzania wenye majengo ya kibiashara dar,wanalia kisa kukimbia makao makuu ya nchi dodoma. Dar majengo yamebakia magofu. Na huwezi kuhamisha majengo. Huyu mtu ameleya shida kubwa kuliko .
 
Back
Top Bottom