Kwanini hatujadili kwa uwazi swala la mahakama ya kadhi na Madai ya waislam

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
1,657
2,252
Mahakama ya kadhi inawahusu waislam tu tena maswala ya mirathi na ndoa. Nduguzetu wanataka iendeshwe kwa kodi zetu. Kwanini wasijichange wao wakaianzisha kwa sadaka na zaka zao. Kwani wao ni wengi kuliko sisi. Je wakristo na wao wakitaka mabalaza yao ya usuluhisho wa ndoa yagaramiwe na selikali. Yani yajengewe ofisi, Walipwe wajumbe na nk. We unazani itakuwaje?

Kuna tena swala la kujua idadi yao wanataka sensa ya kitaifa ihesabu idadiyao kwanini wao wasijihesabu wao wajue watajenga nyumba za ibada ngapi? Na shule zao ngapi.

Kuna hizi shule zilizokuwa za wakristu. Kama Nsumba, Minaki, Kahororo, Ngaza, Ihungo na Ndanda Zilikuwa na makanisa hapo ya dhehebu ililokuwa inazimiliki eti wanataka na selekali iwajengee na nyumba zao za ibada. NA KILA DHEHEBU WAKITAKA WAJENGEWE NYUMBA ZAO HAPO ITAKUWAJE. Kumbuka wakristo wote hawaingiliani kuna wasabato, walokole, RC,

kuna jambo najiuliza bajeti yetu inategemea kodi za pombe na sigara. Je pesa za pombe na sigara zitujengee misikiti au makanisa?

Pili bajeti yetu 50% ni mikopo na misaada kutoka ulaya je watakubali haya?

Pole JK aliyekupandisha ndie atakaekushusha.
 
Back
Top Bottom