Kwanini hatufuniki macho kujikinga na Corona wakati virusi vinaweza kuingia kupitia hapo

pandagichiza

JF-Expert Member
Jul 9, 2013
4,644
3,020
Corona inaingilia machoni, puani na mdomoni.

Tunafunika mdomo na pua kujikinga na corona. KWANINI HATUFUNIKI MACHO KUJIKINGA NA CORONA?

Nawasilisha.
 
Nyongeza,kwanini hatufuniki masikio kujizuia nakorona maana wanatuambia tusishike uso lakini masikioni tushike ata kuingiza vidole ivi ni salama kweli?
 
Logic ni kwamba ushijishike uso!! Inatakiwa uvae hata miwani kuzuia "FUTA" aka Corona isiingie kwa kupitia macho.
 
Korona inaambukizwa kwa kupitia viungo vya mfumo Wa upumuani ambayo mainly ni (pua & mdomo) that is why wanaziba hizo sehemu.
 
Ninavyofahamu ni kwamba macho yanaweza kuwa contaminated...

Ni kutokana na hilo ndo maana tunashauriwa kuepuka kujishika usoni kwa sababu, kama macho yamekuwa contaminated, or infected with the virus, ina maana utahamishia virus mikononi na hivyo kuleta uwezekano wa ama wewe mwenyewe kujiambukiza au kuambukiza watu wengine!

Lakini kwavile hiki ni kirusi, pia kina uwezekano ya kuathiri macho, but I doubt kama itakuwa ni COVID-19 ambayo ni respiratory disease.
 
Mkuu mimi kwa sasa nimenunua miuani navaa. Sijajua serikali yetu inasahau kutuambia au vp! Ikumbukwe hata barakoa mwanzo walisema msivae labda tu kama umeambukizwa.
 
Back
Top Bottom