Kwanini haifikiriki kabisa askari wetu wa FFU wenye uwezo mkubwa kutuliza maandamano na ghasia kuisaidia Ufaransa kuzima maandamono yenye ghasia

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Jiulize - askari wetu wa FFU, pamoja na Raisi wetu Magufuli, wanaona kwamba wana uwezo mkubwa sana wa kuzuia maandamano na ghasia nchini. Wanajisifia kwa hilo.

Sasa angalia kwamba askari wa Ufaransa kwa wiki nzima wamekuwa wakipambana na waandamaji wenye ghasia bila kuwa na mafanikio kwa kiasi cha kutosha.

Unaweza kuwaza - ina maana FFU wa Tanzania wana ujuzi zaidi ya askari wa Ufaransa katika kutuliza maandamano na ghasia mitaani? Je unaweza kuwazia kwamba Raisi Macron wa Ufaransa anampigia simu Rais Magufuli na kumwambia "Raisi Magufuli, naona askari wako wa FFU wana uwezo sana wa kutuliza maandamano na ghasia, naomba unisaidie waje huku Ufaransa"

Haiwezekani. Kwa nini? Sio tu kwa sababu si kawaida kwamba majeshi ya polisi kuvuka mpaka wa nchi yao kwenda kutuliza nchi nyingine,

Kwa nini haiwezekani basi? Ni kwa sababu mafanikio ya FFU kutuliza mandamoano au ghasia nchini hayatokani na ujuzi wao zaidi ya askari wa Ufaransa - yanatokana na wao kutumia njia za kinyama na kikatili ambazo nchi kama Ufaransa haiwezi hata kufikiria kuzitumia kwa wananchi wake.

Kwa hiyo kama FFU au Rais Magufuli watajisifu juu ya uwezo wa askari Tanzania kutuliza maandamano na ghasia si kwa kuwa FFU Tanzania wana uwezo zaidi ya aksri wa Ufaransa, bali ni kwa kuwa FFU Tanzania wanatumia njia za kinyama na ukatili ambazo askari wa Ufaransa kamwe hawawezi kuzikubali zitumike katika nchi yao. Huo ndio ukweli.
 
Unaweza kuwazia FFU wakiwafanyia raia wa Ufaransa mambo kama haya kumsaidia Macron kutuliza maandamano na ghasia?

1544372477757.png
1544372835816.png
 
Jiulize - askari wetu wa FFU, pamoja na Raisi wetu Magufuli, wanaona kwamba wana uwezo mkubwa sana wa kuzuia maandamano na ghasia nchini. Wanajisifia kwa hilo.

Sasa angalia kwamba askari wa Ufaransa kwa wiki nzima wamekuwa wakipambana na waandamaji wenye ghasia bila kuwa na mafanikio kwa kiasi cha kutosha.

Unaweza kuwaza - ina maana FFU wa Tanzania wana ujuzi zaidi ya askari wa Ufaransa katika kutuliza maandamano na ghasia mitaani? Je unaweza kuwazia kwamba Raisi Macron wa Ufaransa anampigia simu Rais Magufuli na kumwambia "Raisi Magufuli, naona askari wako wa FFU wana uwezo sana wa kutuliza maandamano na ghasia, naomba unisaidie waje huku Ufaransa"

Haiwezekani. Kwa nini? Sio tu kwa sababu si kawaida kwamba majeshi ya polisi kuvuka mpaka wa nchi yao kwenda kutuliza nchi nyingine,

Kwa nini haiwezekani basi? Ni kwa sababu mafanikio ya FFU kutuliza mandamoano au ghasia nchini hayatokani na ujuzi wao zaidi ya askari wa Ufaransa - yanatokana na wao kutumia njia za kinyama na kikatili ambazo nchi kama Ufaransa haiwezi hata kufikiria kuzitumia kwa wananchi wake.

Kwa hiyo kama FFU au Rais Magufuli watajisifu juu ya uwezo wa askari Tanzania kutuliza maandamano na ghasia si kwa kuwa FFU Tanzania wana uwezo zaidi ya aksri wa Ufaransa, bali ni kwa kuwa FFU Tanzania wanatumia njia za kinyama na ukatili ambazo askari wa Ufaransa kamwe hawawezi kuzikubali zitumike katika nchi yao. Huo ndio ukweli.
Sema waandamaji wa kitanzania ni waoga. Waandamanaji wa ufaransa wanajielewa.
Halaf wana udhubutu..
Ffu watanzani wapeleke kule wakutane na raia wenye udhubutu tuone perfomance yao.

sema polisi wanatumia uoga wa wananchi wenyewe kufanya yao
 
Sema waandamaji wa kitanzania ni waoga. Waandamanaji wa ufaransa wanajielewa.
Halaf wana udhubutu..
Ffu watanzani wapeleke kule wakutane na raia wenye udhubutu tuone perfomance yao.

sema polisi wanatumia uoga wa wananchi wenyewe kufanya yao
Hapana Mkuu. Suala la woga Ufaransa haliingii kwa kuwa askari wa Ufaransa wanapewa maagizo kabisa kwamba "do not harm the demonstrators"

Sasa niambi Tanzania hapa ikiwa waandamanaji wakiambiwa Polisi wameambiwa "do not harm the demonstrators" kama watashindwa kutoka.

Kumbuka hata vilema walipigwa, na waziri mkuu anaambiwa hata shangazi zako tutawapiga.
 
Tatizo kubwa la watanzania, na hasa vijana wa leo, ni uoga. Wakati tukiwa chuo kikuu pale UDSM, tukiamua kuandamana tuliandamana.

Hata vile vifaa vya kisasa vya FFU vilinunuliwa wakati wetu lakini bado hawakuweza kuzuia maandamano.

Vijana wa leo ni tepetepe, bomu la machozi linapigwa Kimara, wa Mbagala wanaingia uvunguni kwa hofu na woga.

Watawala nao wamewajua vizuri vijana wa Tanzania. Hakuna ushujaa wa kwenye keyboard.
 
Hapana Mkuu. Suala la woga Ufaransa haliingii kwa kuwa askari wa Ufaransa wanapewa maagizo kabisa kwamba "do not harm the demonstrators"

Sasa niambi Tanzania hapa ikiwa waandamanaji wakiambiwa Polisi wameambiwa "do not harm the demonstrators" kama watashindwa kutoka.

Kumbuka hata vilema walipigwa, na waziri mkuu anaambiwa hata shangazi zako tutawapiga.
Usifikirii wamefika hapo kwa ujasiri wa kwenye keyboard? Kufika hapo kulikuwa na kujitolea hasa. Na watawala wanajua kuwa polisi wakiua waandamanaji, na wao utawala ndiyo mwisho.
 
Usifikirii wamefika hapo kwa ujasiri wa kwenye keyboard? Kufika hapo kulikuwa na kujitolea hasa. Na watawala wanajua kuwa polisi wakiua waandamanaji, na wao utawala ndiyo mwisho.

Nakubali. Lakini ona huku kwetu, unaweza kuwazia kuwa Polisi wakiua waandamanaji utawala wa CCM na Magufuli ndio mwisho? Wameshaua mara nyingi tu.
 
Hata waandamanaji wa hizo nchi za ulaya wanajitambua sio kama waandamanaji wa huku africa.
Huku wanatumia hiyo fursa kufanya uporaji na kudhuru watu wengine.
 
Hata waandamanaji wa hizo nchi za ulaya wanajitambua sio kama waandamanaji wa huku africa.
Huku wanatumia hiyo fursa kufanya uporaji na kudhuru watu wengine.
MKuu, hata ulaya kuna uporaji sana,pindi hizo sio huku kwetu tu
 
Kaka ni suala la uwoga. Ffu ya tz haijakutana na waandamanaji wale konk wenyewe.
Unajua watanzania wameshajazwa dhana ya uwoga wakishaona bunduki wanajificha.

Riot police ya ufaranca wamekuwa trained na wanafuata guidlines walizowekewa. That why hawatumii live ammunition.
Kule wanafuata sheria.. hata viongozi wao wanafuata sheria.

Ffu ya tanzania wanafanya wanayofanya sababu wanabaraka za wakubwa. So even wakimuua mmoja, always kesi itapotezewa. So wapata viburi sababu wanalindwa na mabosi zao.

Ufaranca riot police akiua. Basi lazima awajibike
Hapana Mkuu. Suala la woga Ufaransa haliingii kwa kuwa askari wa Ufaransa wanapewa maagizo kabisa kwamba "do not harm the demonstrators"

Sasa niambi Tanzania hapa ikiwa waandamanaji wakiambiwa Polisi wameambiwa "do not harm the demonstrators" kama watashindwa kutoka.

Kumbuka hata vilema walipigwa, na waziri mkuu anaambiwa hata shangazi zako tutawapiga.
 
Kaka ni suala la uwoga. Ffu ya tz haijakutana na waandamanaji wale konk wenyewe.
Unajua watanzania wameshajazwa dhana ya uwoga wakishaona bunduki wanajificha.

Riot police ya ufaranca wamekuwa trained na wanafuata guidlines walizowekewa. That why hawatumii live ammunition.
Kule wanafuata sheria.. hata viongozi wao wanafuata sheria.

Ffu ya tanzania wanafanya wanayofanya sababu wanabaraka za wakubwa. So even wakimuua mmoja, always kesi itapotezewa. So wapata viburi sababu wanalindwa na mabosi zao.

Ufaranca riot police akiua. Basi lazima awajibike
Nakubali woga unachangia, lakini sidhani kama waandamanaji wa Ufaransa wanajitokeza kuandamana kwa kuwa hawana woga wa kupigwa na kuuwawa kama ilivyo Tanzania. Na sidhani kama huwa wanaenda kuamdamana wakijua wataoigwa au kuuwawa kama ilivyo Tanzania. Mabomu ya machozi - ndio. Maji ya baridi - ndio. Kumamatwa na kuwekwa ndani - ndio. Lakini kupigwa na kuuwawa kwa kosa la kuandamana Ufaransa?
 
Tatizo kubwa la watanzania, na hasa vijana wa leo, ni uoga. Wakati tukiwa chuo kikuu pale UDSM, tukiamua kuandamana tuliandamana.

Hata vile vifaa vya kisasa vya FFU vilinunuliwa wakati wetu lakini bado hawakuweza kuzuia maandamano.

Vijana wa leo ni tepetepe, bomu la machozi linapigwa Kimara, wa Mbagala wanaingia uvunguni kwa hofu na woga.

Watawala nao wamewajua vizuri vijana wa Tanzania. Hakuna ushujaa wa kwenye keyboard.
Zama zimebadirika baba,andamana Leo uone
 
Tatizo kubwa la watanzania, na hasa vijana wa leo, ni uoga. Wakati tukiwa chuo kikuu pale UDSM, tukiamua kuandamana tuliandamana.

Hata vile vifaa vya kisasa vya FFU vilinunuliwa wakati wetu lakini bado hawakuweza kuzuia maandamano.

Vijana wa leo ni tepetepe, bomu la machozi linapigwa Kimara, wa Mbagala wanaingia uvunguni kwa hofu na woga.

Watawala nao wamewajua vizuri vijana wa Tanzania. Hakuna ushujaa wa kwenye keyboard.
Udsm mlikuwa mnapigwa risasi za Moto kama aliyopigwa Akwilina?
 
Hao FFU wako wote wataozea jela.

Serikali za wazungu hazitaki mchezo.
 
Back
Top Bottom