- Thread starter
- #81
Ulaya ata kujenga nyumba watu awajengi
Ushawai kumsikia mzungu anasema yupo site.
Kule kuna ma engineer
Ulaya ata kujenga nyumba watu awajengi
Ushawai kumsikia mzungu anasema yupo site.
Kwakweli huyo ni mvivu..mkiwa wawili raha sana..mi nakumbuka nilileta hosuegal baada ya miaka 2..napo nilitafuta nikiwa na mimba ya miezi 8...sababu nilikua lzm nipate mtu wa kunisaidia..isingekua mimba aaaah ningebaki na mr mpkaaa....
Raha sana mkiwa wasela
Sheria na haki za wafanyakaz wa ndani hakuna ilo uchangia kla mtu kuajiri mfanyakaz wandan ata km hana uwezo wa kumlipa na kumiliki
Umasikini ili ni ttzo sana familia nying ni maskin na kaz isiyoitaj taaluma au utaaram ni kaz za ndan kwaiyo iyo nayo usababisha kla mtu kuajiri mfanyakaz wa ndan au garden
Tanzania ni nchi pekee ambayo mfanyakaz tena wa mshahara wa kima cha chini na yy anajiri mfanyakazi wa ndan sjui anamlipa kias gan wakat yy mwenyewe ni kima cha chini
Bongo unakuta mtu amepanga chuma kimoja na sebure na yy kaajiri mfanyakaz masihara aya
Vyombo - Wash disher ipo...
Nguo - Washing mashine ipo...
Sakafu na carpert - Vacum cleaner ipo...
Garden - lawn mower ipo...
Sokini / kazini / shuleni - Private trasport ipo...
Chakula - Rice cooker, na vipikia vyote vipo...
Mdada wa kazi wa nini?
Wanaume wa kia africa wamelelewa kishenzi sana yaan hawana hurumahata kidogo na wenza wao unakuta anamfanyisha mkewe mikazi ye amekaa tu wala hajali na bado analalama juu vitu vinachelewa!
Huyo ndugu yako ni mimi, muda wa kupika pika kila saa unautoa wapi km sio mama wa nyumbani ni kazi sana! Hao ndugu wa mume km wanamuonea huruna sana ndugu yao wawe wanamletea fresh food...yaan Africa tuna upuuz mwingi sana wao maisha ya watu hata sijui yanawahusu nini!
Hujakua bado ukikua utaelewa
Ulaya na Marekani wanafuata sheria sana.Unapomuajiri housegirl unatakiwa umpe mkataba ndani ya mkataba umuwekee NSSF yake matibabu na mambo mengi tu sawa na mtu aliyeko kwenye ajira.Sasa kutokana na hili ndo maana ulaya wanakuwa na kigugumizi sana kuajiri mfanya kazi wa ndani maana ni gharama sana ila kinachofanyika kama una mtoto mdogo unampeleka home day care centre unakwenda job jioni unampitia.Huku kwetu kuna chama cha watu wanaofanya kazi za majumbani lakini hakina nguvu wala meno ya kung'ata kwasababu kwanza housegirl wenyewe hawana elimu hivyo hawajui haki zao.Pili serikali yenyewe inafumbia macho sababu hata hao wakubwa wa serikalini ambao ingekuwa wapitishe sheria hii ya kuwalinda nao wana ma housegirl hivo wanajua na wenyewe mtego utawanasa.Nimekuwa nikitafakari kwa muda sasa.
Kwanini familia za waafrika bila dada wa kazi au housegirl mambo hayaendi?
Mke atalalamika, nyumba itakuwa chafu, chakula hakitaiva kwa wakati yaani mambo yote yatakuwa vurumai.
Lakini ukiangalia wenzetu walioendelea familia nyingi ni baba, mama na watoto na wote wanajituma katika majukumu yao.
Ni familia chache za matajiri sana wenye mansions ndio utakuta kuna maids.
Je ni uvivu?
Je ni kwasababu wanapatikana kwa bei chee?
Ni tabia zetu tu kupenda ubwanyenye?