Kwanini Dkt. Emmanuel Nchimbi alijiuzulu Uwaziri wa Mambo ya ndani Desemba 2013?

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Dkt. Emmanuel John Nchimbi (24 December, 1971) alijiuzuru uwaziri wa mambo ya ndani Desemba 2013, ni sababu zipi zilipelekea kujiuzuru?

Dkt Nchimbi ni nani hasa?

Elimu yake ya Msingi aliianzia jijini Dar es Salaam katika Shule ya Msingi Oysterbay kati ya mwaka 1980 – 1986

Dkt. Nchimbi alijiunga na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Sekondari Uru kati ya mwaka 1987 – 1989 (kidato cha I – III) halafu akahamia Shule ya Sekondari Sangu na kukamilisha kidato cha nne mwaka 1989 – 1990.

Nchimbi alisoma Shule ya Sekondari ya Forest Hill, Mbeya masomo ya kidato cha V na VI mwaka 1991 – 1993. Alijiunga katika Chuo cha IDM Mzumbe (Morogoro) na kuhitimu Stashahada ya Juu ya Utawala (mwaka 1994 – 1997).

Wakati anahitimu IDM, pia alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na mwaka uliofuatia (1998), alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM).

Dk Nchimbi amewahi kuajiriwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kati ya mwaka 1998 – 2003.

Alisoma shahada ya uzamili ya usimamizi wa biashara Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2001 – 2003 akibobea kwenye maeneo ya (benki na fedha).

Dk Nchimbi aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda (mwaka 2003 – 2005) na (mwaka 2008 – 2011) alisoma na kufanikiwa kuhitimu shahada ya uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Amekuwa mbunge jimbo la Songea Mjini.

Mara tu baada ya kuwa mbunge, Rais Kikwete alimteua kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo (Januari 2006 - Oktoba 2006)

Naibu Waziri Wizara ya Kazi, Ajira na Vijana (Oktoba 2006 - Februari 2008)

Naibu Waziri Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa (Frbruary 2008 - Novemba 2010).

Baada ya Uchaguzi Mkuu 2010, Rais Kikwete alimpa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo akiwa Waziri kamili, alidumu hapo hadi Mei 2012 alipohamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kabla ya kujiuzulu Desemba 2013. (Kwanini?)

Mwaka 2016 aliteuliwa kuwa balozi huko Braziri
 
Huyu jamaa anafaa pia kuwa makamu wa Rais
Na PhD yake fake. Hafai huyu.Alimtesa sana Amina Chifupa kisa Amina alitaka kugombea uenyekiti umoja wa vijana. Ila huyu akirudi mbona Musiba ataipata,na Mwita waitara ndo asahau uwaziri. Maana Mwita aliondoka CCM sababu kubwa ni Nchimbi.
 
Dkt. Emmanuel John Nchimbi (24 December, 1971) alijiuzuru uwaziri wa mambo ya ndani Desemba 2013, ni sababu zipi zilipelekea kujiuzuru?

Dkt Nchimbi ni nani hasa?

Elimu yake ya Msingi aliianzia jijini Dar es Salaam katika Shule ya Msingi Oysterbay kati ya mwaka 1980 – 1986

Dkt. Nchimbi alijiunga na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Sekondari Uru kati ya mwaka 1987 – 1989 (kidato cha I – III) halafu akahamia Shule ya Sekondari Sangu na kukamilisha kidato cha nne mwaka 1989 – 1990.

Nchimbi alisoma Shule ya Sekondari ya Forest Hill, Mbeya masomo ya kidato cha V na VI mwaka 1991 – 1993. Alijiunga katika Chuo cha IDM Mzumbe (Morogoro) na kuhitimu Stashahada ya Juu ya Utawala (mwaka 1994 – 1997).

Wakati anahitimu IDM, pia alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na mwaka uliofuatia (1998), alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM).

Dk Nchimbi amewahi kuajiriwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kati ya mwaka 1998 – 2003.

Alisoma shahada ya uzamili ya usimamizi wa biashara Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2001 – 2003 akibobea kwenye maeneo ya (benki na fedha).

Dk Nchimbi aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda (mwaka 2003 – 2005) na (mwaka 2008 – 2011) alisoma na kufanikiwa kuhitimu shahada ya uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Amekuwa mbunge jimbo la Songea Mjini.

Mara tu baada ya kuwa mbunge, Rais Kikwete alimteua kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo (Januari 2006 - Oktoba 2006)

Naibu Waziri Wizara ya Kazi, Ajira na Vijana (Oktoba 2006 - Februari 2008)

Naibu Waziri Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa (Frbruary 2008 - Novemba 2010).

Baada ya Uchaguzi Mkuu 2010, Rais Kikwete alimpa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo akiwa Waziri kamili, alidumu hapo hadi Mei 2012 alipohamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kabla ya kujiuzulu Desemba 2013. (Kwanini?)

Mwaka 2016 aliteuliwa kuwa balozi huko Braziri
Katibu wa CCM ajaye kumpisha Dr Bashiru

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Naogopa Sana nchimbi kushika madaraka ya juu Sana, nadhani aling'oka na akina matayo David kipindi kile
 
Na PhD yake fake. Hafai huyu.Alimtesa sana Amina Chifupa kisa Amina alitaka kugombea uenyekiti umoja wa vijana. Ila huyu akirudi mbona Musiba ataipata,na Mwita waitara ndo asahau uwaziri. Maana Mwita aliondoka CCM sababu kubwa ni Nchimbi.
Kisa cha Mwita kumuogopa Ema.
 
Kote umekuja vizuri...
Umekosa kwenye kuuliza swali... Huwezi kujua yote hayo ukashidwa kujibu swali lako mwenyewe...
Ulipoandika Braziri ndo umedhihirisha kuwa wewe upo mataga timu gani na hustahili kijibiwa...
 
Na PhD yake fake. Hafai huyu.Alimtesa sana Amina Chifupa kisa Amina alitaka kugombea uenyekiti umoja wa vijana. Ila huyu akirudi mbona Musiba ataipata,na Mwita waitara ndo asahau uwaziri. Maana Mwita aliondoka CCM sababu kubwa ni Nchimbi.
Arudi tafadhali tuna mujitaji sana aje kushughulikia na washamba
 
Kisa cha Mwita kumuogopa Ema.
Mwita aliondoka CCM kisa Nchimbi. Ni chui na Paka. Nchimbi alikuwa akikuona unatishia nafasi yake UVCCM basi alikuwa anahakikisha anakuwekea vikwazo. Kwanza alimuhamishia Tanga huko. Kisha Makamba na Nchimbi wakaminyia asigombee Tarime baada ya kifo cha Chacha Wangwe. Baadae ndo Waitara akahama CCM.
 
Mwita aliondoka CCM kisa Nchimbi. Ni chui na Paka. Nchimbi alikuwa akikuona unatishia nafasi yake UVCCM basi alikuwa anahakikisha anakuwekea vikwazo. Kwanza alimuhamishia Tanga huko. Kisha Makamba na Nchimbi wakaminyia asigombee Tarime baada ya kifo cha Chacha Wangwe. Baadae ndo Waitara akahama CCM.
Asante Victoire kwa mchapo
 
Mwita aliondoka CCM kisa Nchimbi. Ni chui na Paka. Nchimbi alikuwa akikuona unatishia nafasi yake UVCCM basi alikuwa anahakikisha anakuwekea vikwazo. Kwanza alimuhamishia Tanga huko. Kisha Makamba na Nchimbi wakaminyia asigombee Tarime baada ya kifo cha Chacha Wangwe. Baadae ndo Waitara akahama CCM.
Naiona historia ya makundi ikijirudia tena 2025, unless kama mama ataplay neutral vinginevyo namuona magufuli mwingine akijipenyeza hapo katikati ya vifaru watakaokuwepo wakati huo wakiiwakilisha ccm asili na ccm mataga 😂
 
Dkt. Emmanuel John Nchimbi (24 December, 1971) alijiuzuru uwaziri wa mambo ya ndani Desemba 2013, ni sababu zipi zilipelekea kujiuzuru?

Dkt Nchimbi ni nani hasa?

Elimu yake ya Msingi aliianzia jijini Dar es Salaam katika Shule ya Msingi Oysterbay kati ya mwaka 1980 – 1986

Dkt. Nchimbi alijiunga na elimu ya sekondari kwenye Shule ya Sekondari Uru kati ya mwaka 1987 – 1989 (kidato cha I – III) halafu akahamia Shule ya Sekondari Sangu na kukamilisha kidato cha nne mwaka 1989 – 1990.

Nchimbi alisoma Shule ya Sekondari ya Forest Hill, Mbeya masomo ya kidato cha V na VI mwaka 1991 – 1993. Alijiunga katika Chuo cha IDM Mzumbe (Morogoro) na kuhitimu Stashahada ya Juu ya Utawala (mwaka 1994 – 1997).

Wakati anahitimu IDM, pia alichaguliwa kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na mwaka uliofuatia (1998), alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM).

Dk Nchimbi amewahi kuajiriwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kati ya mwaka 1998 – 2003.

Alisoma shahada ya uzamili ya usimamizi wa biashara Chuo Kikuu cha Mzumbe mwaka 2001 – 2003 akibobea kwenye maeneo ya (benki na fedha).

Dk Nchimbi aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda (mwaka 2003 – 2005) na (mwaka 2008 – 2011) alisoma na kufanikiwa kuhitimu shahada ya uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe.

Amekuwa mbunge jimbo la Songea Mjini.

Mara tu baada ya kuwa mbunge, Rais Kikwete alimteua kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo (Januari 2006 - Oktoba 2006)

Naibu Waziri Wizara ya Kazi, Ajira na Vijana (Oktoba 2006 - Februari 2008)

Naibu Waziri Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa (Frbruary 2008 - Novemba 2010).

Baada ya Uchaguzi Mkuu 2010, Rais Kikwete alimpa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo akiwa Waziri kamili, alidumu hapo hadi Mei 2012 alipohamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kabla ya kujiuzulu Desemba 2013. (Kwanini?)

Mwaka 2016 aliteuliwa kuwa balozi huko Braziri
Polee
 
Back
Top Bottom