KIBONGOMKUTI
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 1,425
- 605
Shughuli zangu zinanikutanisha na wasichana/wanawake wengi, baadhi yao nawachukulia kama dadaz/aunt zangu. Wengi wamekuwa wananiomba mkopo wa pesa kwa ahadi za kunilipa pesa, lakini cha ajabu au kushangaza wengi wao mara baada ya kukopa jina kaka huanza kutoka kwenye kamusi ya mawasiliano mara utasikia Baby/Honey/Sweet ikifuatiwa na samahani za kizushi kana kwamba kakosea. Funga kazi ni kila ninapodai pesa zangu naishiwa kuonyeshwa dalili za kulipwa huduma badala ya cash money. Naomba ushauri tafadhali me sitaki huduma nataka mpunga wangu full stop!