Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,410
- 119,111
Kwanza naomba kudiklea interest mimi nimeshawahi kufanya kazi ya Customer care...Habari wanajamvi!
Hapa nimetoka kuongea na customer care wa offisi Fulani hivi(Naomba nisiitaje)
Kuhusu malalamiko ya account Yangu kutowezesha pesa kutoka .
Nilipiga simu Mara ya kwanza akapokea Mdada na mazungumzo yalikuwa hivi?
Customer care : Haloow...unaongea na ......naongea na nani Tafadhali!?
Me: Unaongea na ,,...............Niko......
Customer care: oky naomba nikusaidie.
Me: Ninashida hapa kidogo account Yangu imeshindwa kutoa pesa tangu Jana Sijui tatizo nini?
Customer care: kwanini zisindwe kutoka kuna mahali utakuwa umekosea .
Me: hapana Mi sijaanza Leo kutoa pesa Ni mzoefu ndio maana nakwambia hvyo.
Customer care: hiyo pesa itakuwa haipo Kwenye account yako!.
Naomba account number yako!.
Me!....############678
Customer care: Nimesharekebisha hapa jaribu kufanya mihamala tena!.nakutakia siku njema.
Baaada ya hapo ikashindikana nikapiga tena simu akapokea Jamaa saivi. Na maongezi yalikuwa hivi.
Customer care: halow unaongea na .....naongea na nan Tafadhali!...?
Me: unaongea na .......Niko..,.....
Customer care : Naomba nikusaidie Tafadhali!...
Me: Oky! Nimepiga simu mda sio mrefu hapo nilikuwa na shida .......1.2.3.
Lakini naona bado tatizo liko pale pale.
Customer care: Oky naomba account number yako Ndugu mteja...
Me: 2334444#####
Customer care: Naomba usubir kidogo usikate simu.
Me. Oky.
Customer care: Sawa sasa kulikuwa na shida kidogo ya kimtandao kwa watumiaji wa account za
### kuanzia Jana jion hivi hii inatokana na .....1.2.3. Mafundi wanashughurikia tatizo na muda mfupi tatizo litakaa sawa nimechukua namba yako pembeni nitakutaarifu kwa SMS tatizo likimalizika pole kwa usumbufu Ndugu.......
Me: asante sana kiongozi..
Customer Care: ulikuwa na tatizo lingine nikusaidie:
Me: hapana.
Customer care: nakutakia siku njema asante kwa kutumia Huduma zetu.
Hizo zilikuwa Ni conversation kati Yangu na customer care na mpaka saivi problem solved .
Sasa swali langu customer care wa kike huwa wanakuwa na stress za nini mpaka wanatoa majibu ambayo hayamshawishi mteja.
Customer
Sio kwamba namtetea huyo wa kwanza ila najaribu kuelewa situation yake, matatizo ya miamala huwa yanajitokeza mara nyingi hata kwenye mitandao ya simu, tatizo linaweza kuwa lako binafsi, linaweza kuwa ni la wateja wote au ni errors tu ndogondogo ambazo zinajitokeza hapa na pale.
Linapokuwa limetokea tatizo ambalo linawaface wateja wengi mtu wa customer care hawezi kutoa conlusion kuwa kuna tatizo kisa amepokea wateja wawili watatu wenye tatizo moja, ni lazima atoe report juu ya tatizo, lifanyiwe uchunguzi na aletewe majibu kuwa hili ni tatizo X, msaidie mteja kwa njia hii au mwambie asubirie tatizo linashughulikiwa kwa ujumla wake.
Inawezekana ulipokuwa unapiga mara ya kwanza tatizo lilikuwa lipo ila halijatolewa official statement na ulipopiga mara ya pili ikawa ufumbuzi umepatikana.
Ni kweli wapo ambao ni wavivu kufuatilia lakini pia anaweza akawa hana habari kuhusu tatizo husika kulingana na aina wateja aliohudumia siku hiyo