GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,523
- 108,810
Nami najipanga sasa kwenda Uchina ( China ) ili pia nikapate matibabu kwani nasikia Wachina huwa hawashindwi Kitu kabisa. Nina tatizo langu la Pumu la muda mrefu sana na nimejaribu kupata Tiba mbalimbali katika Hospitali za Tanzania hadi nikawa naambiwa sasa kuwa GENTAMYCINE nisipende sana Kupanda Ndege au Treni ila nitumie sana Uber au Gari tu kama ni safari za karibu kama labda za kwenda Uganda au Rwanda hapo.
Ila kwa kuwa mwakani 2020 nami GENTAMYCINE nataka Kugombea Kiti cha Ubunge nimeshauriwa sasa kutokana na aina za Kampeni ambazo nitakuwa nazifanya ambazo nitakuwa nahojiwa mno na Kupingwa sana na itanibidi pia nitembelee Vijiji vyote basi yanipasa hivi karibuni tu au mwaka huu niweze kwenda ( kufanya ) ziara ya nchi za mbali ( tena Mashariki ya mbali ) kabisa huko Uchina ( China ) ili nikatibiwe vyema hii Pumu ( Asthma ) yangu isije Kuniua bure japo pia nitatumia nafasi hiyo hiyo Kusalimiana na Kiongozi ( Rais ) wa China na Viongozi wa Chama cha Kikongwe cha huko ambacho pia ni Rafiki na Chama changu hapa Nyumbani.
Sijapanga bado tarehe ya kwenda huko Uchina ( China ) ila naomba mkisikia tu kuwa nimesafiri huko ikiwa ni mara yangu ya Kwanza kupanda Ndege za mbali mniombee kabisa ( tena ikibidi fungeni kabisa ) ili GENTAMYCINE niweze Kufika salama na nipatiwe Tiba nzuri kabisa kwani kama kuna Watu ambao huwa hawashindwi Kutibu Ugonjwa wowote basi ni Wachina na nasikia pia kuwa hata Magonjwa ya Hatari nayo wanatibu bila kusahau Moyo hivyo naamini nikirudi huko nitakuwa niko ' Fiti ' kabisa kuliko sasa ambapo Pumu yangu hii inanifanya niishi kwa wasiwasi na nisipende Kusafiri mara kwa mara hadi Ndugu zangu, Majirani na Marafiki wananishangaa.
Nawasilisha.
Ila kwa kuwa mwakani 2020 nami GENTAMYCINE nataka Kugombea Kiti cha Ubunge nimeshauriwa sasa kutokana na aina za Kampeni ambazo nitakuwa nazifanya ambazo nitakuwa nahojiwa mno na Kupingwa sana na itanibidi pia nitembelee Vijiji vyote basi yanipasa hivi karibuni tu au mwaka huu niweze kwenda ( kufanya ) ziara ya nchi za mbali ( tena Mashariki ya mbali ) kabisa huko Uchina ( China ) ili nikatibiwe vyema hii Pumu ( Asthma ) yangu isije Kuniua bure japo pia nitatumia nafasi hiyo hiyo Kusalimiana na Kiongozi ( Rais ) wa China na Viongozi wa Chama cha Kikongwe cha huko ambacho pia ni Rafiki na Chama changu hapa Nyumbani.
Sijapanga bado tarehe ya kwenda huko Uchina ( China ) ila naomba mkisikia tu kuwa nimesafiri huko ikiwa ni mara yangu ya Kwanza kupanda Ndege za mbali mniombee kabisa ( tena ikibidi fungeni kabisa ) ili GENTAMYCINE niweze Kufika salama na nipatiwe Tiba nzuri kabisa kwani kama kuna Watu ambao huwa hawashindwi Kutibu Ugonjwa wowote basi ni Wachina na nasikia pia kuwa hata Magonjwa ya Hatari nayo wanatibu bila kusahau Moyo hivyo naamini nikirudi huko nitakuwa niko ' Fiti ' kabisa kuliko sasa ambapo Pumu yangu hii inanifanya niishi kwa wasiwasi na nisipende Kusafiri mara kwa mara hadi Ndugu zangu, Majirani na Marafiki wananishangaa.
Nawasilisha.