Kwanini China iwe ajenda ya siri mkutano wa wafanyabiashara kati ya Marekani na Afrika?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
VCG41N923010210.jpg


Viongozi wa kisiasa na biashara wa Marekani na nchi za Afrika walifanya mkutano wa kilele kati yao kwa njia ya video kuanzia tarehe 27 – 29 Julai, ukiwa na kauli mbiu ya “njia mpya za kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na Afrika”. Kwa Marekani mkutano huu ni moja ya hatua za Rais Joe Biden wa Marekani kujaribu kuboresha uhusiano kati ya Afrika na Marekani, ulioharibiwa vibaya kutokana na lugha za matusi na dharau za mtangulizi wake Bw. Donald Trump. Kwa nchi za Afrika, mkutano huu ni fursa nyingine ya kuangalia vyanzo vya uwekezaji na mitaji, hasa baada ya uchumi wa nchi nyingi za Afrika kuathiriwa na janga la COVID-19.

Katika hali ya kawaida mkutano huu ulitakiwa kuwa ni wa pande mbili, lakini ajabu ni kuwa umegubikwa na ukakasi kiasi, kwani kwa mara nyingine baadhi ya watu wanatumia mkutano huo kama jukwaa la kukosoa uwepo wa China barani Afrika. Baadhi ya wanahabari wa nchi za magharibi wamefikia hata hatua ya kusema mkutano huu ni fursa kwa Marekani kukabiliana na uwepo na ushawishi wa China barani Afrika. Ingawa hili ni jambo la kusikitisha, lakini linaonesha kuendelea kuwepo kwa mawazo ya vita baridi, na kuichukulia Afrika kama ni uwanja wa mapambano ya kiitikadi kati ya nchi kubwa. Lakini pia inafichua zaidi tabia za baadhi ya nchi inapokuja kwenye uhusiano kati yake na nchi za Afrika.

Kumekuwa na imani potofu ya baadhi ya watu wanaoamini kuwa kutokana na Marekani kuwa na idadi kubwa watu wengi wenye asili ya Afrika, au kuwa na mfumo wa kisiasa unaofanana na ule unaofuatwa na nchi nyingi za Afrika, basi Marekani itakuwa rafiki mkubwa wa Afrika. Na wengine hata walifikiri kuwa kutokana na Marekani kuwahi kuwa na rais mwenye asili ya Afrika, basi uhusiano ungekuwa mzuri zaidi wakati ule, lakini takwimu na hali halisi vinaonyesha tofauti kabisa.
dfsgdsgdsg.png

Kwanza, hakuna sera madhubuti ya kitaifa ya Marekani inayohimiza ushirikiano wa kiuchumi na nchi za Afrika. Katika kumbukumbu za hivi karibuni uliongezeka kiasi mwishoni wa utawala wa Rais George Bush. Baada ya hapo katika kipindi chote cha utawala wa Barack Obama kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka 2017 na kuendelea hadi sasa, uwekezaji umekuwa ukipungua mwaka hadi mwaka, uliongezeka kidogo tu katika mwaka wake wa mwisho na kuendelea kupungua. Kwa hiyo kisera, si chini ya chama cha Republican au Democrats, na sio chini rais mzungu au mwenye asili ya Afrika, mtazamo wa Marekani kwa Afrika ni ule ule.

Pili, tunaona kuwa mambo yanayofanya Marekani barani Afrika na sera zake ni ya mhemko (reactionary). Tukiangalia mkutano wa biashara kati ya China na Marekani uliofanyika mwaka 2019 mjini Maputo, Shirika la Maendeleo ya kifedha la Marekani lilipanga kutenga dola za kimarekani bilioni 60. Fedha hizo kimsingi hazikuwa mpango wa kuzisaidia nchi za Afrika, bali zilikuwa (reaction) na lengo la kukabiliana na ongezeko la ushawishi wa China kiuchumi barani Afrika, na hivyo kuwa na manufaa kwa nchi za Afrika. Hii ni tofauti na dola bilioni 60 alizotangaza (proactive) Rais Xi mwaka 2018 kwa ajili ya kuendeleza miundo mbinu barani Afrika, na kuboresha maisha ya watu wa Afrika na kuwawezesha kushirikiana kiuchumi.

Lakini tukiangalia China kwa upande mwingine, takwimu na hali halisi vinajieleza wazi. China imekuwa inashirikiana na nchi za Afrika kwa miaka mingi, na ushirikiano wake na nchi za Afrika umekuwa tulivu. Tangu enzi za mapambano ya kujipatia uhuru ya nchi za Afrika, ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika haujawahi kuwa wa kuilenga nchi fulani, na haujawahi kuathiriwa na mabadiliko ya rais wa China. Kama kuna kudorora kidogo kwa uwekezaji wa China barani Afrika, sababu ni msukosuko wa fedha kama ilivyokuwa mwaka 2008, au janga la COVID-19 kama ilivyokuwa mwaka 2020. Takwimu kutoka China-Africa research Initiative zinaweza kuthibitisha hali hii.

Hata hivi ni bora ikumbukwe kuwa tunaishi katika zama mpya, nchi za Afrika ziko huru kushirikiana na nchi yoyote. Kama nchi moja ikizipuuza nchi Afrika, basi zinaweza kuchagua nchi zinazopenda kushirikiana na nazo. Mara nyingi viongozi wa nchi za Afrika wamekuwa wanaziuliza nchi za magharibi, mlikuwa wapi wakati ushawishi wa China unaongezeka barani Afrika? Jibu ni kwamba baada ya ukoloni zilizitelekeza nchi za Afrika. Lakini China imekuwa ikitekeleza kauli yake kivitendo, kwamba ushirikiano kati yake na Afrika utaendelea kuwepo bila kujali China iko au itakuwa katika hatua gani ya maendeleo.

Mkutano wa biashara kati ya wafanyabiashara wa Afrika na Marekani ni jambo nzuri, kwani bila shaka nguvu ya Marekani, ikiwa mdau wa maendeleo ya Afrika kama ilivyo nchi nyingine, inaweza kuwa mchango muhimu kwa maendeleo Afrika. Kwa hiyo hili ni jambo jema la kukaribishwa.

Lakini pia kama ni kweli China imeweza kurudisha ufuatiliaji wa Marekani na nchi nyingine za magharibi kwa Afrika, basi China inapaswa kupongezwa. Inawezekana kuwa hii ni neema inayoletwa na China barani Afrika bila kutarajia.
 
CHINA ndio mbabe wa uchumi duniani. Afrika na Marekani wakikaa pamoja lazima Mwafrika amuulize USA, utanifanyia nini wewe, tayari Mchina ananipa hiki na kile
 
Mmarekani anakuja Afrika analeta maneno. Mchina anatumia gharama kubwa sana kuiwin Afrika kitu ambacho mmarekni na ulaya hawawezi fanya. China itaendelea kujieneza Afrika na duniani kote.

Anataka ajenge barabara inayotoka China hadi Ulaya, wanambania bania.
 
CHINA ndio mbabe wa uchumi duniani. Afrika na Marekani wakikaa pamoja lazima Mwafrika amuulize USA, utanifanyia nini wewe, tayari Mchina ananipa hiki na kile
Toa takwimu sio ushabiki,maana bado rekodi iko wazi kuwa USA ndio kinara.

Kama unayo hiyo mpya kuwa China ndio kinara, lete takwimu
 
Mmarekani anakuja Afrika analeta maneno. Mchina anatumia gharama kubwa sana kuiwin Afrika kitu ambacho mmarekni na ulaya hawawezi fanya. China itaendelea kujieneza Afrika na duniani kote.

Anataka ajenge barabara inayotoka China hadi Ulaya, wanambania bania.
Watalegeza tu hakuna ujanja
 
Mmarekani anakuja Afrika analeta maneno. Mchina anatumia gharama kubwa sana kuiwin Afrika kitu ambacho mmarekni na ulaya hawawezi fanya. China itaendelea kujieneza Afrika na duniani kote.

Anataka ajenge barabara inayotoka China hadi Ulaya, wanambania bania.
Hamuoni aibu kukaa kusifia yanayofanywa na nchi nyingine
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom