Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,036
- 20,337
Chato kuwa mkoa haijakaa vyema. Hii ilipaswa kuachwa kama wilaya ndani ya mkoa wa Geita.
Kwanini chato iwe mkoa kutoka kwenye mkoa mchanga wa Geita?
Ikumbukwe Geita ilitengwa kua Mkoa mwaka 2010 kipindi cha Jakaya tena iweje mkoa mchanga utoe mkoa mwingine wa Chato? Soma Kikwete atangaza mikoa, wilaya mpya
Serikali ingepaswa kuangalia mikoa mingine mikubwa ndio iweze kuikata kuzaa mikoa mingine, mfano mikoa inayostahili inaweza kua Tabora, Morogoro, Tanga, Singida, Ruvuma, n.k
Kuna haja gani ya kuunda mkoa Mpya wa Chato? Serikali iliangalie hili lasivyo kutakua na utitiRi wa mikoa kwa kila Rais ajae.
_______________________________
Rejea Taarifa hizi
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.
Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:
1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.
2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.
3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.
4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.
Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.
Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.
Nini maoni yako kwenye hili?
Kwanini chato iwe mkoa kutoka kwenye mkoa mchanga wa Geita?
Ikumbukwe Geita ilitengwa kua Mkoa mwaka 2010 kipindi cha Jakaya tena iweje mkoa mchanga utoe mkoa mwingine wa Chato? Soma Kikwete atangaza mikoa, wilaya mpya
Serikali ingepaswa kuangalia mikoa mingine mikubwa ndio iweze kuikata kuzaa mikoa mingine, mfano mikoa inayostahili inaweza kua Tabora, Morogoro, Tanga, Singida, Ruvuma, n.k
Kuna haja gani ya kuunda mkoa Mpya wa Chato? Serikali iliangalie hili lasivyo kutakua na utitiRi wa mikoa kwa kila Rais ajae.
_______________________________
Rejea Taarifa hizi
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.
Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:
1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.
2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.
3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.
4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.
Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.
Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.
Nini maoni yako kwenye hili?