Kwanini Chadema haiwalipi hawa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
2008-07-02 09:46:16
Na Simon Mhina

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe, amedai kwamba kinachotokea sasa hivi ndani ya CHADEMA ni mpango maalum wa kukiua chama hicho ili kisionekane katika uchaguzi mkuu 2010 na sio ruzuku inayotolewa na Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini.

Akizungumza na Nipashe jijini jana, Mwenyekiti huyo alisema sio siri kwamba CHADEMA ni tishio kwa mafisadi, ambao wamejipanga vilivyo kutoa upinzani mkubwa kwenye uchaguzi huo.

Alisema kuna njama za kuidhoofisha CHADEMA kabla ya mwaka 2010.

``Wameshajua kwamba huenda janga la ufisadi likawa agenda kubwa sana katika Uchaguzi Mkuu ujao, na hakuna asiyejua kwamba CHADEMA ndio wameibua tatizo hilo na sisi na wabunge wetu ndio tumelishikia bango, sasa kuna njama inafanywa ya kufa na kupona kuhakikisha kwamba tunakosa nguvu,`` alisema.

Mwanasiasa huyo alisema sio siri kwamba tayari kuna watu ndani ya CCM hasa kundi la mafisadi, ambao tayari wameshaanza kupanga mikakati kwa ajili ya uchaguzi huo.

Alisema kwa madai haya hana maana ya kumtuhumu Makamu wake aliyesimamishwa kwamba anashirikiana na mafisadi hao, lakini ukweli kuhusu kila jambo, utafahamika.

``Na moja ya mkakati huo ni kuhakikisha kwamba kabla ya uchaguzi huo nguvu ya CHADEMA inapungua,`` alisema.

Hata hivyo, kiongozi huyo alionya kwamba hakuna mgawanyiko wowote ndani ya CHADEMA kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vinashabikia.

Alisema ruzuku ya chama hicho inatumika kwa mlingano sawa mikoani kwa mujibu wa mahitaji na bajeti ya chama.

Bw. Mbowe, alitoa ufafanuzi huo, kufuatia madai kwamba ruzuku ya CHADEMA inaishia makao makuu na kwamba wale wanaohoji na kutaka isambae zaidi ili kujenga chama chao wanaonekana nuksi.

Mwenyekiti huyo alisema kwa kiasi kikubwa shughuli za makao makuu ya chama hicho, zinaendeshwa kwa kujitolea.

Alisema viongozi wa juu wa CHADEMA, akiwemo yeye, Katibu Mkuu na Naibu wake, wanafanya kazi kwa kujitolea.

``Mimi siku zote sijawahi kupokea mshahara wala posho kutoka CHADEMA, gari ninalotumia ni langu binafsi, dereva namlipa mimi kila kitu najihudumia mwenyewe. Vilevile Katibu Mkuu na hawa akina Zitto hawapokei malipo yoyote kutoka CHADEMA,`` alisema.


Bw. Mbowe, alisema yeye amekuwa akitoa fedha zake binafsi kwa ajili ya kukisaidia chama na wakati mwingine kukikopesha bila riba wala masharti yoyote, pale ambapo kinapungukiwa.

Aliwataka wanachama wa CHADEMA na wale wa kambi ya upinzani na viongozi wake, wasisononeke kutokana na kuchafuka kwa hali ya siasa ndani ya chama hicho, kwa vile hapakuwa na njia nyingine ya kusawazisha mambo.

Alisema hatarajii kwamba hatua ya Kamati Kuu kumsimamisha uongozi Makamu Mwenyekiti, Bw. Chacha Wangwe itazua mtafaruku wowote.

Alisema hatarajii hali hiyo kwa vile Bw. Wangwe, alishirikishwa katika hatua hiyo muhimu.

Bw. Mbowe, alisema hali ya CHADEMA imetulia na kuna mshikamano wa hali ya juu kati ya viongozi wote, vikao vya chama na wanachama.

Alisema wamelazimika kuchukua hatua hiyo, ili kusawazisha mambo ndani ya chama kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

``Tulikuwa na wasiwasi na baadaye tumethibitisha kwamba kilichokuwa kinaendelea ndani ya chama lengo lake ni kudhoofisha CHADEMA katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010,`` alisema.

Hata hivyo, Bw. Mbowe, alisema njama zozote za kusambaratisha chama chake hazitawezekana, kwa vile umma wa Watanzania umeshajua vita iliyopo mbele yao ya ufisadi, ambayo kwa kiasi kikubwa imeshikiwa bango na CHADEMA.

Makamu Mwenyekiti aliyesimamishwa, Bw. Chacha Wangwe, amekuwa akidai kwamba mbali na ruzuku, sababu nyingine ya kutoelewana na wenzake ni yeye kuhoji chama chao kutokuwa na sura ya kitaifa kutokana na nafasi nyeti kupeana watu wa mkoa mmoja.

My Take:
- Kwanini Chadema isiwalipe viongozi wake? Hicho chama siyo taasisi ya dini au NGO, huu mtindo wa kulipa fedha za wao wenyewe na wengine kutolipwa ni mtindo mbaya. Hata mtindo wa Mbowe kutoa fedha yake mfukoni kwa ajili ya Chadema siyo mtindo mzuri kwani unamfanya aonekane kama ana maslahi zaidi ya mtu mwingine. Chama kiendeshwe kama Chama. Hata kama chama hakiwezi kuwalipa inavyopaswa ni muhimu kuwa na token payment hata kama Shs. 10,000 kwa mwezi kwa viongozi lazima walipwe, wasifanye kazi za chama bure.

- Kama Bajeti ya Chama ni ndogo kuliko mahitaji yake, ni lazima wajifunze kufanya mambo ndani ya bajeti. Kama ni kuanzisha miradi n.k wafanye hivyo lakini wasifanye vitu ambavyo hawana uwezo wa kuvigharimia. Katika hili wanaweza kuanzisha miradi ya Chama. Hili linawezekana kwa kuanzisha kampuni ya Chama (Holding Company) na wanaweza kuangalia ni jinsi gani chama kinaweza kumiliki kitega uchumi. Kama mnapata karibu milioni 66 kila mwezi na fedha zote zinaishia kwenye matumizi na hazizalishi basi kuna tatizo la kiuwekezaji.

- Uongozi mkuu wa chama ujitoe kwenye kusimamia fedha na badala yake waajiri watu ambao wana weledi wa mambo ya fedha. Mhasibu Mkuu, Mkaguzi wa ndani, watunza fedha n.k na wataalamu wa Boharia. Wanasiasa wabakie kufanya maamuzi ya kisiasa. Na watumishi hawa walipwe kwa kiwango cha fani zao, na wasiwe na uhusiano wowote ule wa karibu na kiongozi yeyote wa juu wa chama hicho. Kabila, mkoa, rangi, au dini na jinsia don't count.

- Ruzuku ya Chama isipokelewe na kiongozi wa kisiasa, period. Fedha za ruzuku au fedha nyingine yoyote inaenda moja kwa moja kwenye akaunti ya chama na hesabu zake zinaeleweka na zinasimamiwa ipasavyo. Lazima waweke mfumo mzuri wa usimamizi wa fedha ili saa ya yoyote ijulikane wana fedha kiasi gani, ziko wapi, na zimetumika vipi.

- Viongozi wa kisiasa warudi kwenye kuimarisha chama, kwa kupika makada wa kisiasa, kufungua matawi ya chama n.k. Sikumbuki mara ya mwisho kusikia Zitto, Slaa, au Mbowe amefungua tawi la Chadema mahali popote ilikuwa lini. Chama hakijengwi kwa hotuba za Bungeni, au maneno ya magazetini, bali kwa kushawishi watu kukikubali na kuzielewa sera zake. Na njia pekee ya kuonesha kuwa watu wanawakubali ni watu kujiunga na chama hicho.

Madai kuwa watu wanaelewa kuwa Chadema inapigia kelele ufisadi zaidi n.k ni madai tu lakini ushahidi wa watu kuelewa unaonekana kwa watu kujiunga. Je tangia mambo ya ufisadi yaanze na tangia sakata la Zitto Chadema imejipatia wanachama wangapi, na kiasi cha watu kujiunga kina tofauti gani na kabla ya hapo. Kama hakuna tofauti kubwa na inayoonekana basi kuna tatizo mahali fulani.

Mengine.. nitawaandikia in private katika kulinda "heshima ya chama" chenu.
 
2008-07-02 09:46:16
...Hata mtindo wa Mbowe kutoa fedha yake mfukoni kwa ajili ya Chadema siyo mtindo mzuri kwani unamfanya aonekane kama ana maslahi zaidi ya mtu mwingine.


Mara nyingi hii inafanya chama kionekane kinahodhiwa na wale walio na uwezo wakujitolea zaidi (wenye uwezo mkubwa kifedha). Kwa watu wenye uwezo mdogo kipesa (ambao ndio walio wengi) inakuwa ngumu kuona ni namna gani watapokelewa au kusisika ndani ya chama, kwani mchango wao ni mdogo. huu ndio mwanzo wa watu kuanza kusema chama kile ni cha watu wachache. nakubaliana na MMK wanachama wapya ndio kipimo halisi cha kukubalika na ndio watakao kitegemeza chama, ikiwa ni pamoja na uwekezaji
 
CHADEMA haiko tayari kuongoza nchi na kuna dalili kuwa haijaanzishwa kwa lengo la kuongoza nchi.
Mambo aliyoeleza mwanakijiji ni muhimu na ya ukweli mtupu.Hata hivyo ifahamike kuwa Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA wana sources nyingi sana ya kujifunza jinsi ya kusimamia mapato ya chama na mgawanyo wake. Kinachotokea hivi sasa ndani ya CHADEMA hakisababishwi na ukosefu wa maarifa ya kusimamia mapato au kuzalisha bali ni matokeo ya maamuzi ya makusudi ya viongozi walioamua kuweka muundo utakaowawezesha kufanya maamuzi kwa malengo wanayoyajua wao.
Nionavyo mimi, kuwashauri watu wanaojua mengi lakini hawako willing to change is a waste of time.
 
naona hajamtaja makamo mwenyekiti viiiipi yeye alikuwa akilipwa ? au ndio chuki hata kumtaja hataki ?
 
...Mambo aliyoeleza mwanakijiji ni muhimu na ya ukweli mtupu.Hata hivyo ifahamike kuwa Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA wana sources nyingi sana ya kujifunza jinsi ya kusimamia mapato ya chama na mgawanyo wake. Kinachotokea hivi sasa ndani ya CHADEMA hakisababishwi na ukosefu wa maarifa ya kusimamia mapato au kuzalisha bali ni matokeo ya maamuzi ya makusudi ya viongozi walioamua kuweka muundo utakaowawezesha kufanya maamuzi kwa malengo wanayoyajua wao.
Nionavyo mimi, kuwashauri watu wanaojua mengi lakini hawako willing to change is a waste of time.

kama ni hivyo, haya je ni danyanya toto, maana naona kama wameweka mfumo na malengo yanayoongela hata ya MMk hapo juu. ingawa sijaelewa huko kuwekeza bila kufanya biashara

source: http://www.chadema.net/mikakati/makao.php
Mpango Mkakati wa Saba kwa 2006 -2010

Kupanua na kujenga ofisi ya Makao Makuu ya chama kwa kuongeza vifaa na uwajibikaji ili kuongeza hadhi, ufanisi, tija na utekelezaji wa shughuli na maamuzi ya vikao vya chama:

Idara ya raslimali itahusika na kutambua, kubuni, kusimamia na kupata raslimali za chama mathalani fedha, miradi, vifaa, muda, mawazo na nyenzo nyingine toka kwa wanachama, wapenzi wa chama na wadau wengine wa maendeleo.


Kuwekeza katika uzalishaji (bila kukifanya chama kifanye biashara). Kuendesha michango ya umma (local fundraising) kwa kutumia shughuli za namna mbalimbali.


Idara ya Fedha itahusika na usimamizi wa matumizi ya fedha kwa pamoja na mambo mengine kuandaa kanuni za mapato na matumizi ya raslimali/fedha na kuhakikisha zinafuatwa katika ngazi mbalimbali za chama.
 
Kwa kweli Chadema inahitaji msaada mkubwa.Ni lazima tukubali kuwa kwa staili hii haitaweza kuongoza nchi.Mabadiliko makubwa yanahitajika.Kwa hali ya sasa inaonekana kama Chadema ni mali ya Mwenyekiti.Kama ni kweli yeye ndiye anayetoa fedha nyingi namna hiyo basi ni wazi kuwa hakuna mwenye kauli yoyote juu yake.Na hii ni hatari kwa chama hasa inapofika wakati wa kufanya maaamuzi magumu na mazito kwa faida ya chama na wananchi.

Najua mwanzo ni mgumu ila chonde chonde Chadema suala la fedha,umaarufu na jeuri ya baadhi ya viongozi inaweza kuwa ni chanzo cha mparaganyiko wa chama.


-Wembemkali.
 
Maandishi ya Mbowe kwenye hili saga yamenitisha kweli kweli. Inaelekea anajua mno ku spin.

Alipoamua kuwataja watu ambao hawalipwi na wanajitolea ilitakiwa aongelee na suala la Wangwe. Ilitakiwa ataje kama Wangwe analipwa au halipwi. Hii kuchagua habari ya kuitoa kiujanja ni njama ya kuwadanganya wananchi na ndivyo vitu ambavyo wengine tunavipinga. Kuwa straight forward, kama hulipwi au uongozi wote wa juu wa CHADEMA hauilipwi basi sema hivyo.

Nakubaliana na Mwanakijiji kwamba vyama vyetu kutegemea fadhila za wenye fedha wachache ndio mwanzo wa matatizo. Tajiri hatumbukizi pesa zake kwenye chama bila interests, ni muhimu kwa vyama kutumia pesa za wananchama, hata kama hazitoshi.

Kama viongozi hawalipwi basi kuwe na utaratibu ambao unajulikana ukielezea nani halipwi na kwasababu zipi. Kwa mfano wabunge wanaweza wasilipwe kwasababu wana mishahara bungeni.
 
Haya mahojiano ya Mbowe na mwandishi wa Nipashe yamenistua.

Mbowe alikuwa ana nia ya kujenga Chama (kinachoelekea kuyumba katika kipindi hiki cha mpito kuelekea 2010), lakini sithani kama inahitaji kipaji kuona kuwa ameshindwa kutimiza lengo lake. Hii habari imeharibu hadhi ya Chama hasa machoni mwa wasomi.... Hainiingii akilini kwa nini Chadema mpaka leo hasa viongozi bado wanafanya kazi kwa kujitolea; I mean mudo wote ambao Mbowe anatumia kuendesha Chama ni kwamba anajitolea.!!! Kwa nini ajitolee..???

Namuunga mkono Zemarcopolo anaposema...

Kinachotokea hivi sasa ndani ya CHADEMA hakisababishwi na ukosefu wa maarifa ya kusimamia mapato au kuzalisha bali ni matokeo ya maamuzi ya makusudi ya viongozi walioamua kuweka muundo utakaowawezesha kufanya maamuzi kwa malengo wanayoyajua wao.


Huo ni ukweli unasikitisha na kukatisha tamaa, Chadema need to get their house in order la sivyo wale wasomi wachache walianza kuwa na matumaini ya mabadiliko ya kweli watarudisha nyuma imani yao. Mapendekezo ya Mzee Mwanakijiji ni muhimu yafanyiwe kazi ndani ya Chadema tena kuwepo na juhudi za makusudi za kuwapa taarifa wa Wananchi kuhusu progress yake.

Chadema tayari inaumizwa sana na hisia za ukabila; kama alivyosema Mtanzania huko nyuma kuwa "hisia" kwenye siasa ni kitu kibaya sana. Juhudi za dhati ni lazima zifanyike kufuta hizi hisia kwa wananchi...nikisema juhudi za dhati na za wazi nina maanisha wafikirie nje ya box kabisa hata ikibidi kuweka "positive descrimination" kwenye utaratibu wao wa kuchagua viongozi. Doa la matumizi mabaya ya fedha za chama na ukabila ni sumu kubwa sana kwa jumuiya yoyote ile inayo jinadi kuwajibika kwa wananchi.

Chadema nawatakia kila la kheri...tafadhalini sana juhudi za kusafisha sifa mbaya za chama zisiwe siri. Watanzania sio wajinga wanaelewa na nyie mkiwa wa wazi na wakweli mtaeleweka na kujenga heshima ya chama.
 
naona hajamtaja makamo mwenyekiti viiiipi yeye alikuwa akilipwa ? au ndio chuki hata kumtaja hataki ?

Maandishi ya Mbowe kwenye hili saga yamenitisha kweli kweli. Inaelekea anajua mno ku spin.

Alipoamua kuwataja watu ambao hawalipwi na wanajitolea ilitakiwa aongelee na suala la Wangwe. Ilitakiwa ataje kama Wangwe analipwa au halipwi. Hii kuchagua habari ya kuitoa kiujanja ni njama ya kuwadanganya wananchi na ndivyo vitu ambavyo wengine tunavipinga. Kuwa straight forward, kama hulipwi au uongozi wote wa juu wa CHADEMA hauilipwi basi sema hivyo.


Wakuu

Nashindwa kuelewa kwa nini mlitegemea Mwenyekiti Mbowe amtaje Chacha Wangwe wakati ambapo ameshasimamishwa uongozi/cheo/kazi ya Umakamu Mwenyekiti na kikao halali cha chama??

Sioni kama kuna haja ya kuchambia kila neno, sentensi, nukta na koma katika kauli ya Mwenyekiti wa Chadema. Tuchukue hoja kubwa aliyoiweka wazi kuwa hao viongozi hawalipwi na sio mbona hajataja jina fulani.
 
Kuelekea ukombozi ni lazima wachache ama wengi wawe tayari kuumizwa kwa faida ya wengi.

Hii ni vita ya kuelekea ukombozi ,na ijulikane kuwa wafanayabiashara na wenye pesa hawakichangii CHADEMA kwani wanaogopa CCM.

vitu vingine tuwe tayari kusema ukweli mbona hata hapa JF inaendeshwa kwa kuchangiwa na wanachama wake wenye uwezo wa kuchangia?

Mbona hapa hamlalamiki kuwa waache kuchangia?

Nani anamlipa Invisible na JF Crew yote hapa ?mbona wao wanajitolea na kufanya bure?

Ama kujitolea CHADEMA ndio dhambi na kosa?
 
Kuelekea ukombozi ni lazima wachache ama wengi wawe tayari kuumizwa kwa faida ya wengi.

Hii ni vita ya kuelekea ukombozi ,na ijulikane kuwa wafanayabiashara na wenye pesa hawakichangii CHADEMA kwani wanaogopa CCM.

vitu vingine tuwe tayari kusema ukweli mbona hata hapa JF inaendeshwa kwa kuchangiwa na wanachama wake wenye uwezo wa kuchangia?

Mbona hapa hamlalamiki kuwa waache kuchangia?

Nani anamlipa Invisible na JF Crew yote hapa ?mbona wao wanajitolea na kufanya bure?

Ama kujitolea CHADEMA ndio dhambi na kosa?

Naona kujitolea ni dhambi kwa vile kasema Mbowe.

Hata hivo wazo la chama kujitegemea ni zuri sana, lakini tusikimbilie kuwalaumu CHADEMA, kwani kumbuka CCM ilichukua mali zote zilizokuwa chini ya mfumo wa chama kimoja ambazo tulikuwa tumezichangia watanzania wote, na bado ikahakikisha utaratibu wa ruzuku ya chama kulingana na idadi ya wab unge ikijua kwamba yenyewe itaendelea pata lion's share, bado tu hazija watosha waka kwapua na za EPA!

My take:
Vyama vya ushindani vinacheza katika unfair ground, zile mali za chama kimoja ingebidi zirudishwe serikalini baada ya vyama vingi ili vyote vianze square one!

Kwa mtaji huu, bila kujitolea Chama hakiwezi kusonga mbele kwani havikuwezeshwa kuanza na bado mfumo wa ruzuku ni wa kibaguzi, bora hiyo ruzuku ingekuwa inagawiwa sawa kwa vyama vyote bila kujali idadi ya wabunge walau hiyo ingesaidia kuviinua hata vyama vidogo!
 
Kuelekea ukombozi ni lazima wachache ama wengi wawe tayari kuumizwa kwa faida ya wengi.

Hii ni vita ya kuelekea ukombozi ,na ijulikane kuwa wafanayabiashara na wenye pesa hawakichangii CHADEMA kwani wanaogopa CCM.

vitu vingine tuwe tayari kusema ukweli mbona hata hapa JF inaendeshwa kwa kuchangiwa na wanachama wake wenye uwezo wa kuchangia?

Mbona hapa hamlalamiki kuwa waache kuchangia?

Nani anamlipa Invisible na JF Crew yote hapa ?mbona wao wanajitolea na kufanya bure?

Ama kujitolea CHADEMA ndio dhambi na kosa?

MK,
JF sio chama cha siasa na haina dhumuni la kushika madaraka ya kuongoza watanzania milioni 40, CHADEMA on the other hand is.
Ndio maana Mwanakijiji akasema haipaswi kuendeshwa kama shirika la kidini au NGO.
Kuna wanachadema wameshanukuliwa hapa wakisema kuwa kabla Mbowe hajawa mwenyekiti CHADEMA ilikuwa inaendeshwa kama NGO, habari hii tuliyopata leo inatueleza kuwa CHADEMA bado inaendeshwa kama NGO.
 
MK,
JF sio chama cha siasa na haina dhumuni la kushika madaraka ya kuongoza watanzania milioni 40, CHADEMA on the other hand is.
Ndio maana Mwanakijiji akasema haipaswi kuendeshwa kama shirika la kidini au NGO.
Kuna wanachadema wameshanukuliwa hapa wakisema kuwa kabla Mbowe hajawa mwenyekiti CHADEMA ilikuwa inaendeshwa kama NGO, habari hii tuliyopata leo inatueleza kuwa CHADEMA bado inaendeshwa kama NGO.

JF ni jukwaa la mapambano ya ukombozi, CHADEMA ni chama cha kuutafuta ukombozi.

Mnakumbuka TANU ilichangiwa na watu gani? si walikuwa wanatafuta ukombozi ?

Sasa tatizo ni kuwa CHADEMA nayo inaelekea njia hiyo hiyo ya kikombozi ila isichangiwe.

Kumlipa Mbowe na viongozi wa CHADEMA si ndio kusema ruzuku ibakie makao makuu badala ya kwenda mikoani? Utamlipa ngapi Lissu?Slaa, wakurugenzi wa makao makuu?

Tukubaliane kuwa hizi ni harakati za ukombozi na ukombozi daima una hatua , sasa ni hatua za harakati.

Naamini kuwa kuna siku haya maneno yatakubaliwa .

Jukwaa lolote la ukombozi hupitia hatua za kujitolea .....
 
Hata NGOs haziendeshwi kwa staili hii ya Mbowe na CHADEMA. Tuwasaidie jamaa hawa ili Chama hiki kiweze KUJITEGEMEA angalau kwa 50%. Watupatie akaunti yao tuchangie kulingana na uwezo wa kila mmoja wetu halafu UONGOZI utajua namna kuzizalisha pesa hizo. Vinginevyo tunaongopeana hapa kumpenda Dr. Slaa, Mh. Zito, Mh. Wangwe....Bila CHADEMA, CCM itatufanya vibaya zaidi ya haya ya EPA, RICHMOND,...
 
MMK
Nakushukuru sana kwa ushauri kuhusu uendeshaji wa fedha kwenye vyama vya siasa. Hata hivyo, Chadema ni chama kinachofanya kazi yake kwa uwazi. Hatuna la kuficha napenda kueleza ifuatavyo:
i) Uamuzi wa viongozi wakuu, tena wanaotumia muda wao wote kwa shughuli za chama, za kisiasa na uendeshaji, ni uamuzi uliofanyika kwa hiari na kupitia vikao halali vya chama. Kwa bahati mbaya maamuzi mengine hayafiki hadharani. Chadema haioni cha ajabu katika hatua hii. Mwalimu Nyerere asingejitolea enzi za uhuru, na kuchangiwa na wapenzi wachache waliokuwa na uwezo leo tusingelikuwa na Uhuru. Nadhani wenye mapenzi mema na nchi hii wataelewa kuwa mapambano tuliyonayo ni mapambano yanayohitaji kujitolea kwa kiwango kikubwa. Viongozi wakuu wa Chadema kwa kutambua hili, waliamua kwa hiari yao, kujitolea ili ruzuku kidogo iliyoko itumike kwa shughuli za uenezi. Bendera, Kadi, nyaraka mbalimbali,ujenzi wa Ofisi stahiki Makao Makuu ya Chama kama sura ya Chama, kuwekeza kwenye miradi ya muda mrefu ya kuitegemeza chama( kazi hiyo imekwisha kufanyika siyo nadharia na kwa yeyote mwenye nia ya kutaka kujua tunaweza kumpa taarifa za kina), ziara za uenezi na kadhalika.
2) Viongozi wa juu wa Chadema ni Wabunge, ukimwacha Mwenyekiti. Mishahara wanayopata ikitumika kuendeleza Chama kuna dhara gani, Chama hujengwa na wenye moyo. Hili halina maana ya wenye kuchangia chama ndio waamuzi katika maamuzi ya chama. Chama kinaendeshwa kwa Katiba, Kanuni, Maadili, na Itifaki ya Chama. Maamuzi yanapofanywa kwa imla hofu hizo hutokea. Kwa Chadema, ambayo maamuzi yake hufanyika yote na vikao halali, mipango huenda kwa kadiri ya Strategic Plan, ambayo nayo si siri, ipo wazi kwenye Mtandao wa Chama, na kila mwenye nia njema anaweza kuipata bila tatizo. iwapo kuna mwenye kuhitaji maelezo ya ziada tuko tayari kuyatoa wakati wowote, vitabu vya Hesabu ya Chama ni mali ya Wanachama na wakati wowote Mwanachama anaweza kuomba taarifa atapewa, na au anaweza kufika Makao Makuu ya Chama akaona vitabu hivyo bila gharama yeyote. Taarifa zote za fedha hutolewa kwenye vikao vya Kamati Kuu, na sijawahi kuona Taarifa ya Fedha ikikataliwa kwa ubadhirifu au kwa sababu yeyote ile. Wajumbe wa Kamati Kuu ni mashahidi. Taarifa ya Fedha hutolewa pia kwenye Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuendana na Ratiba ya Kikatiba ya Vikao hivyo.
3: Fedha za Chadema hukaguliwa na Wakaguzi wanaotambulika kisheria, na huwasilishwa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.
4: Ili kuepuka Wachache wenye uwezo kufanya chama kuwa mali yao, Chadema inaoutaratibu ambao sina hakika vyama vingapi unao, wa kutathmini na kutambu mchango wa kila mwanachama kwa maana ya fedha zake anazochangia kwenye chama, muda wake anaotumia kwa ajili ya shughuli za Chama ( hatua hii inafanyika kwa sasa Makao Makuu tu kwa vile Instruments za kufanya Tathmini hii kwenye mikoa na Wilaya bado inafanyiwa kazi na hata ya Makao Makuu bado inaendelea kufanyiwa kazi. Mathalan muda wa mtumishi wa Chama anayefanya kazi baada ya saa rasmi za kazi hutathminiwa na kupewa thamani ya fedha kama mchango wake kwa ujenzi wa chama. Inahitajiwa fikra mpya ili ukombozi tunaoendelea nao uweze kufanikiwa. Lakini kutegemea fedha tu hakutatufikisha mahali.

Hivyo, Tafsiri sahihi ya Kauli ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chadema, inaweza kuhojiwa katika misingi hii. Nimeona nieleze hili kwa misingi ya uwazi kwa vile Chadema hatuna cha kuficha, chama ni cha wote wenye nia njema, na hata wasiokitakia mema kama wapo ni vema wakajua Chadema inaendeshaje shughuli zake ili wasiohoji kwa nadharia na kwa hisia. Mwenye kuhitaji Taarifa zaidi, Dr. Slaa, anapatikana kwa Simu na +255 784 666995 au +255 754 366 995 au kupitia E mail zangu slaa@chadema.net, wslaa@hotmail.com. Nafurahi kwa wote waliochangia kwa angle yeyote ile kwani licha ya kuwa kila mmoja ana uhuru wa kutoa maoni yake, pia kila mwanademokrasia halisi hutambua mchango wa kila mmoja na pia anaweza kuokoteza mawazo mazuri katika michango hiyo. Hakuna mchango uko mbovu tu, hata uliombovu sana unajambo zuri, japo dogo la kuweza kujifunzia. Naomba radhi si nia yangu kutoa mhadhara, lakini kila inapohitajika katika mada yeyote ile nitafanya hivyo kwa maslahi ya nchi yetu, wanachama wetu na wote wenye mapenzi mema.
 
Mnajua Chama siku zote hakiendeshwi bila pesa hiyo tusidanganyane.
Angalieni vyama ambavyo havina pesa vilivyo choka kuna vyama vingine vinajulikana Dar tu ukiona mikoani havijulikani kabisa.
Kama Mbowe anatoa pesa zake mwenyewe mfukoni kwa ajili ya chama ni jambo la kumpongeza kwa kuonyesha uzalendo wa hali ya juu.Sasa mkianza kuuliza kama Wangwe analipwa au lah hapo sasa mjadala mwingine yeye si anakula posho za Ubunge bungeni kwa kupitia chama chake.
Kuendesha chama kuna hitaji sana fedha na wafadhili wengi wa kujitolea sasa miongoni mwao wanaweza wakawa na masrahi binafsi wengine ni ungwana tu.
 
mkuu hebu tuingie kwenye ile mada ya makamo mwenyekiti wenu nnaomba utupatie mawazo yako kuhusu suala hili kwa nn mliamua kumnyonga hadharani kweupee kama saddam ?
 
Dr. Slaa,

Kwanza nikukaribishe mzee wetu!

Ama kweli JF imenifanya walau nimsome mtu ambaye nilitamani kuona ameandika online. Na nimekubali kuwa mzee wetu hauko nyuma katika issue ya teknolojia wakati wenzako wengi wakiiponda njia hii ya mawasiliano.

Mzee nimekuwa impressed na statement yako hapo juu pamoja na kujiunga nasi hapa. Ninachoweza kukuomba ni kuwa mvumilivu kwani penye wengi tambua pana mengi. Wengi wetu tunatumia pen names lakini wengine ni watu ambao unatufahamu tukikutana face to face. Nakuomba kuwa mwenye subira pale unapoona mambo yanakuwa ndivyo sivyo. Nakuomba usiwe kama Mwenyekiti wenu Mbowe ambaye alipoulizwa maswali mengi hapa hakutia mguu tena. Kaa nasi na pindi tukihitaji kupata kauli yako tujibu kiungwana japo twaweza kuuliza kipuuzi tu. Ni kweli kuwa si kila swali lazima lijibiwe. Upatapo nafasi basi jaribu kutupa moyo katika harakati hizi.

Back to the issue, nashukuru kwa comment yako ngoja niwape muda wadau kuona wana yepi ya kuongeza.

Kibakuli
 
MMK
Mwenye kuhitaji Taarifa zaidi, Dr. Slaa, anapatikana kwa Simu na +255 784 666995 au +255 754 366 995 au kupitia E mail zangu slaa@chadema.net, wslaa@hotmail.com. i

Mkuu Slaa.
Sote tunatambua sana mchango wako wakupigana na mafisadi nchini.
Lakini tunasikitika sana kuona unatumia mtandao wa simu wa FISADI aliye kubuhu Rostam Aziz na hapa imewahi tolewa thread watu kususia huduma zote za mafisadi kama huyu.
Kwa hiyo mkuu kuendelea kutumia line ya simu ya VODA maanake unamuunga mkono RA anaye tuibia nchi yetu kwa kuwekeza kwenye hii kampuni ya VODA.
Tunaomba ubadilishe hii line ya VODA tupo tayari kukuchangia ununue TIGO au ZANTEL.
Ahsanteni.
 
Kuelekea ukombozi ni lazima wachache ama wengi wawe tayari kuumizwa kwa faida ya wengi.

Hii ni vita ya kuelekea ukombozi ,na ijulikane kuwa wafanayabiashara na wenye pesa hawakichangii CHADEMA kwani wanaogopa CCM.

vitu vingine tuwe tayari kusema ukweli mbona hata hapa JF inaendeshwa kwa kuchangiwa na wanachama wake wenye uwezo wa kuchangia?

Mbona hapa hamlalamiki kuwa waache kuchangia?

Nani anamlipa Invisible na JF Crew yote hapa ?mbona wao wanajitolea na kufanya bure?

Ama kujitolea CHADEMA ndio dhambi na kosa?

unachoshindwa kujua ni kwamba JF sio chama cha siasa chenye malengo ya kuongoza nchi siku moja kama chadema, Hii ni forums ambayo watu wachache wamejitolea kwa moyo mmoja na hata wewe hujakatazwa kufanya hivyo, lakini Chadema ni chama cha siasa na kina katiba na dhumini la kuongoza nchi yetu kama ikibahatika,we unategeme siku Mbowe akisema anataka kulipwa pesa zake zote alizo jitolea wakati wako IKulu si watauza nchi yetu , kuwa makini ndugu yangu
 
Back
Top Bottom