Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,236
Huwa sielewi ni kwa nini Viongozi na wanachama wa CCM huwa wanasisimuliwa sana na maneno na matendo ya kiugandamizaji.
Kwa mfano huwezi kuamini inakuwaje wabunge wa CCM wengi wao wanakuwa kinyume na Mbunge Mwenzao Tundu Lissu wakati wanajua kabisa alishambuliwa nusura auawe. Ukiwasikiliza Wabunge wa CCM baadhi yao utaona ni kama vile wanafurahia kushambuliwa kwa Lissu.
Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao wengi wao kama siyo wote ni wana CCM, mara nyingi sana matamko yao huwa ni yenye kuashiria kutumia nguvu ndiyo sura halisi ya dola dhidi ya wananchi.
Mitaani wafuasi na wananchama wa CCM wao huwa wanaona sawa tu kutumia nguvu dhidi ya nguvu za hoja za wapinzani wao. Kule Zanzibar kuna watu hadi wamepachikwa jina la "Zombie" na ni watu wenye matendo mabaya sana dhidi ya wale wasio wana-CCM wenzao.
Hata kufananisha uongozi na viongozi wa CCM ni rahisi sana kulinganisha viongozi wao na viongozi wale wasiofuata kanuni za kuheshimu haki za binadamu.
Wao utasikia wakisema "China iliendelea kwa kutoendekeza haki za binadamu" ama "watu kama nyie mngekuwa Korea kaskazini mngeshatwangwa risasi".
Kwa nini CCM huwa wanasisimuliwa sana na mambo yanayosadifu ugandamizaji?
Kwa mfano huwezi kuamini inakuwaje wabunge wa CCM wengi wao wanakuwa kinyume na Mbunge Mwenzao Tundu Lissu wakati wanajua kabisa alishambuliwa nusura auawe. Ukiwasikiliza Wabunge wa CCM baadhi yao utaona ni kama vile wanafurahia kushambuliwa kwa Lissu.
Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao wengi wao kama siyo wote ni wana CCM, mara nyingi sana matamko yao huwa ni yenye kuashiria kutumia nguvu ndiyo sura halisi ya dola dhidi ya wananchi.
Mitaani wafuasi na wananchama wa CCM wao huwa wanaona sawa tu kutumia nguvu dhidi ya nguvu za hoja za wapinzani wao. Kule Zanzibar kuna watu hadi wamepachikwa jina la "Zombie" na ni watu wenye matendo mabaya sana dhidi ya wale wasio wana-CCM wenzao.
Hata kufananisha uongozi na viongozi wa CCM ni rahisi sana kulinganisha viongozi wao na viongozi wale wasiofuata kanuni za kuheshimu haki za binadamu.
Wao utasikia wakisema "China iliendelea kwa kutoendekeza haki za binadamu" ama "watu kama nyie mngekuwa Korea kaskazini mngeshatwangwa risasi".
Kwa nini CCM huwa wanasisimuliwa sana na mambo yanayosadifu ugandamizaji?