S V Surovikin
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 13,614
- 32,710
Habari
Kila mmoja wetu ni shahidi kwamba tangu alipoingia madarakani bwana John Joseph pombe magufuli kauli zake na vitendo vyake ilikuwa ni kuua upinzani hasa CHADEMA.
Tumekuja mpaka 2020 kwenye uchaguzi mkuu tukashuhudia ambayo kila mmoja wetu anajua pamoja na kauli tata kwamba wapinzani ndio wanachelewesha maendeleo ya watanzania.
Hatimaye Uchaguzi ukaisha na CCM wakaibuka kidedea kwa mbinu wanazojua wao. Ndugu zetu upande wa pili/CHADEMA wakaamua kujiweka pembeni ili serikali ya CCM iweze kuharakisha maendeleo kwa wananchi, ila cha ajabu kuna kilio kikubwa kutoka CCM kuhusiana na jambo hili.
Yani viongozi wetu pamoja na sisi wafuasi wa chadema tumejiweka pembeni kuhusiana na jambo hili ila ccm wanahangaika sana kulikoni?
Naombeni mnisaidie nipate kuelewa nini kiko nyuma ya kilio hiki cha CCM wakati mahubiri yao siku zote ni kwamba wapinzani hawafai, wapinzani wanachelewesha maendeleo ya wananchi, wapinzani wanashirikiana na mabeberu, upinzani umekufa na maneno mengi ya namna hiyo.
Hata hapa jamiiforums tunaona vijana wa CCM wakijitahidi kuanzisha mada za kuwaomba viongozi wetu wakubali kupeleka wabunge wa viti maalum, wamefika mbali hadi kuleta nukuu za makada wa CCM wakitaka CHADEMA wakubali kupeleka wabunge wa viti maalum.
Je, kuna nini nyuma ya pazia?
Kila mmoja wetu ni shahidi kwamba tangu alipoingia madarakani bwana John Joseph pombe magufuli kauli zake na vitendo vyake ilikuwa ni kuua upinzani hasa CHADEMA.
Tumekuja mpaka 2020 kwenye uchaguzi mkuu tukashuhudia ambayo kila mmoja wetu anajua pamoja na kauli tata kwamba wapinzani ndio wanachelewesha maendeleo ya watanzania.
Hatimaye Uchaguzi ukaisha na CCM wakaibuka kidedea kwa mbinu wanazojua wao. Ndugu zetu upande wa pili/CHADEMA wakaamua kujiweka pembeni ili serikali ya CCM iweze kuharakisha maendeleo kwa wananchi, ila cha ajabu kuna kilio kikubwa kutoka CCM kuhusiana na jambo hili.
Yani viongozi wetu pamoja na sisi wafuasi wa chadema tumejiweka pembeni kuhusiana na jambo hili ila ccm wanahangaika sana kulikoni?
Naombeni mnisaidie nipate kuelewa nini kiko nyuma ya kilio hiki cha CCM wakati mahubiri yao siku zote ni kwamba wapinzani hawafai, wapinzani wanachelewesha maendeleo ya wananchi, wapinzani wanashirikiana na mabeberu, upinzani umekufa na maneno mengi ya namna hiyo.
Hata hapa jamiiforums tunaona vijana wa CCM wakijitahidi kuanzisha mada za kuwaomba viongozi wetu wakubali kupeleka wabunge wa viti maalum, wamefika mbali hadi kuleta nukuu za makada wa CCM wakitaka CHADEMA wakubali kupeleka wabunge wa viti maalum.
Je, kuna nini nyuma ya pazia?