nyabhingi
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 15,513
- 19,998
labda nikukumbushe tu kuwa na mimi nilikuwa brainwashed sunday school kama wewe mpaka nilipostukaendelea kuamini ivyo ila ukweli utaujua tuu
labda nikukumbushe tu kuwa na mimi nilikuwa brainwashed sunday school kama wewe mpaka nilipostukaendelea kuamini ivyo ila ukweli utaujua tuu
mi ni tofauti nawewe mi sijafundishwa sunday school sikuwa mwendaji kanisani mzuri nilikua nasubiria kuna visherehe vya mikaeli na watoto nikapige wali neema imenijia wakati najitambua...sikushangai nyie mlikua mnafundishwa lugha za kitoto ili mwelewe kwaio pole kwa kipindi icho na pole sasa kwa kipindi hikilabda nikukumbushe tu kuwa na mimi nilikuwa brainwashed sunday school kama wewe mpaka nilipostuka
nipe pole kwa kipindi kile na nipongeze kwa kipindi cha sasa(in fact ni miaka mingi sasa tokea nilipokataa utumwa wa mawazo wa wazungumi ni tofauti nawewe mi sijafundishwa sunday school sikuwa mwendaji kanisani mzuri nilikua nasubiria kuna visherehe vya mikaeli na watoto nikapige wali neema imenijia wakati najitambua...sikushangai nyie mlikua mnafundishwa lugha za kitoto ili mwelewe kwaio pole kwa kipindi icho na pole sasa kwa kipindi hiki
EIMEN nimeitikia kwa herufi kubwaHalafu kuna mpuuzi mmoja anataka kuleta ujinga kuifunga JF, nasema ashindwe na atakayepata wazo la kuifunga JF kufa na afe yeye hata na uzao wake wote
Mkuu we hatari sana kwa uchambuzi wa aina hii hadi nageuka mwanafunzi kwenye uzi wangu mwenyewe..... Tunakusubiri urudi umwage nondo zaidi maana uko deep si kitotoMada nzuri,kabla kuangalia kwann kanaan alilaaniwa inabidi tujue kanaan nani na hamu nani na zipi asili zao?
Je hamu alikuwa mtu wa aina gani?
Hamu alikuwa ni phoenician ambaye alipewa laana na baba yake nuhu baada kuona utupu wa nuhu mwanzo 9:22,lakini Hamu ni jina lenye asili ya kiebrania likiwa na maana blackened,burnt or hot
Je neno kanaan lina maana gani?
Jina kanaan limetokana na neno la kiebrania likiwa na maana low land embu jiulize unawezaje mwita mtoto aliyezaliwa leo jina kama hilo! Jibu jina kanaan si lake la kuzaliwa hili jina alipewa badae alipokuwa akiishi akitoka kutoka milimani kuja low land
Je lipi jina alilopewa kanaan baada ya kuzaliwa
Jina lake alipozaliwa ni Lebana ambalo asili yake ni kiebrania likiwa na maana nyeupe
itaendelea ....
Naomba niseme neno hapampendwa zitto junior
kwanza hongera sana kwa mada tamu na fikirishi namna hii nikuweke wazi tu kuwa mada zako zote nimezipata kupitia TAGS zako ahsante na ninakuomba usichoke kuniTAG tena na tena kila upandishapo nyuzi za aina hiyo kumbuka kuniTAG........ahsante sana kwa hilo
pili mpendwa zitto junior kwenye hii mada yako nimejaribu kuifatilia pamoja na nadharia ulizoziambatanisha na kugundua kuwa kuna vitu viwili vinahitaji majibu ya kina yasio ya kutumia nguvu nyingi wala kulazimisha na yasio na mashaka kabisa
1. kwanini Mungu alimlaani canaan badala ya ham (mwenye hatia)
2. kwa nini laana laana laana kizazi kimoja mpaka cha tatu au nne ?
mpendwa kimsingi hivo vitu ni maswali fikirishi sana na vinavoitaji majibu kwa faida ya wengi
kuna maelezo kadhaa nilitaka niyatoe lakini naona hayajitoshelezi na maswali ya msingi hasa la kwanza yatabaki palepale. hivyo ninaomba muda ili tuendelee kutafiti na kujifunza zaidi
pamoja sana na barkiwa sana mpendwa
mpendwa kuhusu iyo namba 1 TUPO PAMOJA,Naomba niseme neno hapa
1. Kuna siri kubwa kwenye neno la kiungu.. Kuna wakati inahitaji tafakuri jadidi ya kiroho kuweza kuelewa
2. Hili la laana lina mlolongo mrefu... Yaani kwanini laana inaenda mpaka vizazi vine!? Hii tuitafsiri kidunia namna hii... Kinapotokea kishindo uzito wake ndio utasababisha kiwango cha madhara na sauti yake itaenda mbali kulingana na uzito wa kishindo husika... Laana si kitu kidogo hata maramoja inapiga kizalia ni kama bomu la nyuklia kule Hiroshima Japan mpaka leo madhara yapo
3. Kuna neno ndani ya Biblia nadhani kwenye kitabu cha ufunuo linasema.... Watakutwa watu wawili kondeni mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.... Baada ya hapo yanatajwa na maeneo mengine, huwa najiuliza sana kwanini wawili? Kwanini mmoja aachwe? Je hata wale wafu kuna mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa?
4. Kwenye hesabu na matendo ya roho huwa kuna vitu vya ajabu vyenye kuacha maswali mengi maswali fikirishi sana....
Ngoja nitoe mifano rahisi ya kidunia labda inaweza kutupa mwanga fulani
.Kwenye martial art kuna nguvu inaitwa chi power (vital energy power)... Ni very damaging power isiyo na madhara ya nje.. Kwa mfano mtu anapanga tofali tatu zinazofanana anapiga ya huu lakini inakatika ya katikati huku ya chini na ya huu zikibaki salama..
. Kwa wale wacheza pool... Kete anayotarajia kupiga iko kushoto mwisho lakini anaipigia hesabu kwa kupiga kete ya kupigia iende kulia kwanza ikagonge mahali fulani ndio irudi kushoto na kugonga target....
. wacheza mpira hasa wafungaji na wapiga penalty.. Kuna namna wamefunzwa kupiga mpira ili golikeeper auone unatoka nje kumbe unakuja kuingilia kwenye pembe... Ama ile ya kuruka kushoto na mpira kwenda kulia
Unajichanganya,unasema Ham alilaaniwa kwa kuangalia uchi wa baba yake,wakati ukisoma biblia inaandika wazi aliyeona uchi wa baba yake ni Caanan na si Ham.Soma vizuri biblia yako.Hoja ya msingi sasa, kwanini aone uchi mwingine,alaaniwe mwingine ambae hata kwenye tukio hakuwepo?nadharia zote zimejikita kwenye chanzo kimoja cha imani yaani bibilia.
nilitegemea mkuu utuwekee vyanzo vya talmud au maandiko mengine ya kiyahudi ambayo hayapo kwenye bibilia,quran(umesema hakuna chanzo), Jashar, Enoch, na vya historia nyingine zinazozungumzia sakata hilo. nasema kwa sababu stori uliyoitoa umeitoa kuktoka katka mwanzo 9, na Sababu ya laana imeandikwa hapohapo. ungetoa na vyanzo vingine mtambuka vyenye sababu hizo nyingine ili msawazo wa mada usiegemee kwwnye bibilia tu.
ili litoe sura ya kwamba nadharia zako zote zina biblical support.
Mchango.
Binafsi kwa msingi wa chanzo bibilia, naamini alilaaniwa kwa sababu ya kuona uchi wa baba yake. na ndivyo ilivyoandikwa na kuelezwa humo. kwa mtiririko wa matukio ya bibilia, sio ajabu mtu na dada yake au ndugu yake kufanya mapenzi mara tu baada ya Uumbaji na Gharika ili kuendeleza vizazi na kuijaza nchi. hivyo sioni sababu ya kulinganisha laana za kipindi cha walawi ambacho tayari watu walikuwa wameshakuwa wengi tuiseme itumike kuhukumu watu wa kizazi cha nuhu au adam.
Ikiwa hoja zote zitajengwe kwenye bibilia fact ni moja tu. Ham alilaaniw kwa kuangalia uchi wa baba yake.
maoni mkuu.
Once again umenikosha sana kwa uchambuzi wako murua kabisa..... Ila mkuu ungetusaidia pia kwanini dhambi afanye mwingine alafu alaaniwe mwingine utakuwa umetusaidia kumaliza sintofahamu yetu humuTuichunguze nadharia ya kwanza hapo juu
Je hamu alilala na mama ake?
Hapana,ukisoma ktk mwanzo 9:22 neno uchi ktk andiko la kiebrania limetumika ERVAH likiwa na maana AIBU,CHUKIZO,SUMBUFU
Pia neno ERVAH linaweza kutumika uhusiano wa kimapenzi lakn halitumiki peke yake mpaka kuwe na neno lingine mfano walawi 18:7 usifunue uchi (GALAH ERVAH ) Hapo inamaanisha kufunua uchi kuwa Na uhusiano wa kimapenzi
Je neno kusex kwa kiebrania linatumikaje?
Kwa kiebrania neno hutumia neno YADA likiwa na maana kumjua mfano mwanzo 4:1 Adam akamjua hawa mkewe naye akapata mimba
Pia kuna neno lingine lenye kumaanisha kusex SHAKABA likiwa Na maana kulala Na Mtu mfano mwanzo 19:33 wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule akaondoka huyo mkubwa akalala nae
Hivyo Kama hamu angesex lingetumika neno YADA Au angelala na mama ake lingetumika neno SHAKABA
Mkuu ngoja tuangalie nikirudi tena namaliziaOnce again umenikosha sana kwa uchambuzi wako murua kabisa..... Ila mkuu ungetusaidia pia kwanini dhambi afanye mwingine alafu alaaniwe mwingine utakuwa umetusaidia kumaliza sintofahamu yetu humu
Karibu tena mkuu kuna mada nimekutag nakusubiri hukoNimetoka kifungoni
Ipi tenaKaribu tena mkuu kuna mada nimekutag nakusubiri huko
Sijakuelewa hata kidogo hebu soma hii:
Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Ezekiel 18:20
Sasa iweje Canaan abebe uovu wa baba yake Ham?
Iweje Watoto wa Akani waangamizwe kisa uovu wa baba yao?
Iweje ardhi ilaaniwe kwa uovu wa Adam?