Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
18,913
28,522
Noah-sons.jpg

Habari za jioni wanajukwaa....kama kichwa cha uzi kinavyosema ningependa tujadili mada hii Kutokana na hili swali swali kuulizwa mara nyingi kwenye thread zangu nimeona nifungue uzi wake ili tujaribu kulitatua hili swali

Je ni kwanini aliyetenda dhambi ya kumuangulia uchi wa babake ni HAM ila laana ikaenda kwa mwanaye ham aliyeitwa CANAAN....

STORI YENYEWE
Mwanzo 9
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake


Mpaka hapa tunaona anayetajwa kuchungulia uchi ni Ham ila laana inaenda kwa Canaan why?? Embu tusome nadharia hii

NADHARIA #1
Kutoka vyanzo tofauti vya kihistoria na kidini vinaelezea kisa hiki kwamba Nuhu alipolewa Ham hakuona uchi kama uchi ila inaelezwa Ham alilala na Mke wa Nuhu yaani Ham alilala na mama yake mzazi na mwisho wa siku akabeba mimba na akazaliwa Canaan na hii ilipelekea Nuhu amlaani Canaan na sio Ham sababu alikuwa kizazi cha dhambi haramu kabisa..... Na vitabu hivi vinaenda mbali na kusema Ham alimuhasi baba yake alipokuwa amelewa hiyo nayo ikapelekea Nuhu kushindwa kuzaa mtoto mara baada ya gharika!!!

VITABU VYA DINI
Nadharia hii sio tu nje ya vitabu vya dini ila hta vitabu vya dini hasa biblia inaweza kutumika kuijengea hoja embu tuangalie tafsiri yake

Mambo ya walawi 20
11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao

Walawi 18:8
8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako

NB:Kitabu cha mwanzo na mambo ya walawi vyote viliandikwa mwanzoni na Nabii Musa hivyo kama tutachukua tafsiri yake ya ''KUANGALIA UCHI WA BABA YAKO'' inamaanisha kuna ukweli juu ya nadharia hii kuwa Ham alimlala mama yake mzazi/mke wa Nuhu

Na sio kwa baba tuu Musa alielezea zaidi

Walawi 20
20 Tena mtu mume akilala na mke wa mjomba wake, ameufunua utupu wa mjomba wake; watauchukua uovu wao; watakufa bila kuzaa mwana.
21 Tena mtu mume akimtwaa mke wa nduguye, ni uchafu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana


Biblia haikuishia hapo ila ukisoma kitabu cha habakuki kinakataza mtu kulewesha jirani yake ili KUMCHUNGULIA UCHI.... Ikimaanisha kama ambayo Ham alimfanyia baba yake alipokuwa amelewa basi ndio hiko anachokataza habakuk ila sio kuchungulia kwa macho kama wengi tulivyoaminishwa

Habakkuk 2:15
15 Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao!

Mistari iko mingi zaidi ya 10 inayoeleza kwamba kumchungulia kaka baba au mjomba wako ni kulala na mke wake hivyo wa waliouliza swali hili naona tunaweza conclude kwa nadharia hii kuwa HAM alimlala mke wa NUHU ndio baada ya kuja kujua alichofanya na mimba aliobeba akamlaani Canaan sababu ndio zao la dhambi hiyo iliotendeka

NADHARIA #2
Ukisoma vitabu vya dini ya kiyahudi kma midrash vinasema Canaan aliona Nuhu akiwa uchi hivyo akaenda kumuhasi kwa kutumia kamba na alipotoka ndio baadae Ham alikuta Nuhu akiwa amevuliwa nguo yeye akaishia kucheka tu badala ya kumfunika na mwisho wa siku ndipo laana akapewa Canaan kwa kufanya hicho kitendo

NADHARIA #3
Hapa inadaiwa na wanatheolojia kuwa mwandishi wa kitabu hiki alikuwa anatafuta sababu ya kuhalalisha uvamizi wa israel kwenye nchi ya Canaan so akapachika jina Canaan badala ya HAM ili ahalalishe uvamizi wa israel kwa kigezo cha kwamba NENO LA MUNGU LILIANDIKA!!!

NADHARIA #4
Inasema Canaan hakuwa mtoto wa Nuhu ila ndio alirudisha damu ya wanefili baada ya gharika baada ya Malaika aliyeitwa SHAMAEL siku chache kabla ya gharika alimlala mke wa HAM aliyeitwa Neitamuk na kumpa mimba ya mnefili CANAAN na ndio alisababisha maasi na roho ya shetani kupata nguvu upya immediately baada ya gharika na ndiye alipelekea kuzaa wanefili kama wale wa kabla ya gharika hivyo kwa kuona uovu wa HAM aliofanya, hasira za Nuhu zikaishia kwa CANAAN sababu ndio alikuwa uzao wa roho ya kishetani (SHAMAEL) iliosababisha hadi dhambi kurudi baada ya gharika

BAADA YA LAANA
Tunaona canaan akizaa watoto walioishi miji kama sodoma Gomorrah na Gaza zote israel ya sasa na walikuwa na falme zenye nguvu sana ila kwa kuwa laana hii ya Nuhu iliwafuata ilikuja kutimizwa na watoto wa yakobo (uzao wa SHEM) waliokuja kuwapora nchi yao ya CANAAN na wakawachinja takribani kizazi chote rejea kitabu cha joshua na kumbukumbu la torati na hata wachache waliobaki waliendelea kuteswa sana na waisrael na BIFU hili lilienda hadi kwa Yesu alipokataa kumponya mwanamke wa kanaani

Mathayo 15:22
22 Na tazama, mwanamke Mkanaani wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa


CANAAN NA WANEFILI
Hoja ya kwamba canaan huenda alikuwa uzao wa malaika shamael ama uzao wa ajabu wa Ham na mama yake watoto wake wote walikuwa wanefili yaani majitu ya futi mpaka 28..... Kati ya watoto wote wa ukoo wa Nuhu hakuna mtu aliyezaa wanefili kuliko Canaan na makabila yote ya warefai kipindi hicho walitoka familia ya canaan wawe wayebusi wagilgal waamori wahiti wahivi n.k je huu unaweza kuwa ushahidi kuwa hakuwa mtoto wa uzao wa kawaida ndio maana akazaa wanefili watupu huku na yeye akiwa mnefili???

HAM KWENYE UISLAM
Sijapata popote kwenye Quran inapoandikwa kuhusu laana hii ya Canaan ila kwenye ukristo ma uyahudi ndipo imetajwa. Ila ukisoma hadeeth mbalimbali na machapisho ya wasomi nguli wa kiislam wa mwanzo kabisa kina Muhammad ibn-jarir al tabari pamoja na ibn khaldun wanaeleza kwamba HAM alilaaniwa sababu akiwa kwenye Safina ya Nuhu alimlala mke wake kitu kilichokatazwa hivyo alilaaniwa kwa kupewa ngozi nyeusi na ndio maana watoto wake wote wakawa weusi!!! So hawa angalau wamesema HAM alilaaniwa ila kwa kosa tofauti.... Hivyo bado hawajatupa jibu la kisa cha Nuhu na Canaan

HITIMISHO
Mada hii imetumiwa sana na wazungu wakoloni hasa karne ya 19 kuhalalisha ukoloni wa watu weusi kwa kigezo kuwa mwafrika alilaaniwa ila hoja hii naipinga sababu canaan alilaaniwa peke yake na kizazi chake kwa ukubwa kilishafutwa ila waafrika 80% walitokana na kizazi cha wale watoto 3 wa HAM ambao laana hii haikuwahusu hivyo natumia fursa kupinga propaganda hiyo rasmi na ni vizuri waafrika tupende kusoma historia yetu ili wahuni wachache wasipotoshe ukweli

Naomba kuwasilisha

Karibuni wanajukwaa wote tusaidiane kujadili kuhusu nadharia hizi,
 
NB:Mods naomba msihamishe mada hii kwenda jukwaa la dini sababu licha ya kuwa nimequote baadhi ya mistari ya vitabu vya dini ila uzi huu ni mtiririko wa mada zilezile nilizoanza humu JF intelligence kuhusu wanefili na wanadamu wa kale so mkihamisha mtaharibu mtiririko wa mijadala yangu kwa wanaofuatilia.... Ntashkuru kwa ushirikiano wenu

Cc JamiiForums Innovator Invisible Reserved
 
View attachment 775662
Habari za jioni wanajukwaa....kama kichwa cha uzi kinavyosema ningependa tujadili mada hii Kutokana na hili swali swali kuulizwa mara nyingi kwenye thread zangu nimeona nifungue uzi wake ili tujaribu kulitatua hili swali

Je ni kwanini aliyetenda dhambi ya kumuangulia uchi wa babake ni HAM ila laana ikaenda kwa mwanaye ham aliyeitwa CANAAN....

STORI YENYEWE
Mwanzo 9
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake


Mpaka hapa tunaona anayetajwa kuchungulia uchi ni Ham ila laana inaenda kwa Canaan why?? Embu tusome nadharia hii

NADHARIA #1
Kutoka vyanzo tofauti vya kihistoria na kidini vinaelezea kisa hiki kwamba Nuhu alipolewa Ham hakuona uchi kama uchi ila inaelezwa Ham alilala na Mke wa Nuhu yaani Ham alilala na mama yake mzazi na mwisho wa siku akabeba mimba na akazaliwa Canaan na hii ilipelekea Nuhu amlaani Canaan na sio Ham sababu alikuwa kizazi cha dhambi haramu kabisa..... Na vitabu hivi vinaenda mbali na kusema Ham alimuhasi baba yake alipokuwa amelewa hiyo nayo ikapelekea Nuhu kushindwa kuzaa mtoto mara baada ya gharika!!!

VITABU VYA DINI
Nadharia hii sio tu nje ya vitabu vya dini ila hta vitabu vya dini hasa biblia inaweza kutumika kuijengea hoja embu tuangalie tafsiri yake

Mambo ya walawi 20
11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao

Walawi 18:8
8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako

NB:Kitabu cha mwanzo na mambo ya walawi vyote viliandikwa mwanzoni na Nabii Musa hivyo kama tutachukua tafsiri yake ya ''KUANGALIA UCHI WA BABA YAKO'' inamaanisha kuna ukweli juu ya nadharia hii kuwa Ham alimlala mama yake mzazi/mke wa Nuhu

Na sio kwa baba tuu Musa alielezea zaidi

Walawi 20
20 Tena mtu mume akilala na mke wa mjomba wake, ameufunua utupu wa mjomba wake; watauchukua uovu wao; watakufa bila kuzaa mwana.
21 Tena mtu mume akimtwaa mke wa nduguye, ni uchafu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana


Biblia haikuishia hapo ila ukisoma kitabu cha habakuki kinakataza mtu kulewesha jirani yake ili KUMCHUNGULIA UCHI.... Ikimaanisha kama ambayo Ham alimfanyia baba yake alipokuwa amelewa basi ndio hiko anachokataza habakuk ila sio kuchungulia kwa macho kama wengi tulivyoaminishwa

Habakkuk 2:15
15 Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao!

Mistari iko mingi zaidi ya 10 inayoeleza kwamba kumchungulia kaka baba au mjomba wako ni kulala na mke wake hivyo wa waliouliza swali hili naona tunaweza conclude kwa nadharia hii kuwa HAM alimlala mke wa NUHU ndio baada ya kuja kujua alichofanya na mimba aliobeba akamlaani Canaan sababu ndio zao la dhambi hiyo iliotendeka

NADHARIA #2
Ukisoma vitabu vya dini ya kiyahudi kma midrash vinasema Canaan aliona Nuhu akiwa uchi hivyo akaenda kumuhasi kwa kutumia kamba na alipotoka ndio baadae Ham alikuta Nuhu akiwa amevuliwa nguo yeye akaishia kucheka tu badala ya kumfunika na mwisho wa siku ndipo laana akapewa Canaan kwa kufanya hicho kitendo

NADHARIA #3
Hapa inadaiwa na wanatheolojia kuwa mwandishi wa kitabu hiki alikuwa anatafuta sababu ya kuhalalisha uvamizi wa israel kwenye nchi ya Canaan so akapachika jina Canaan badala ya HAM ili ahalalishe uvamizi wa israel kwa kigezo cha kwamba NENO LA MUNGU LILIANDIKA!!!

NADHARIA #4
Inasema Canaan hakuwa mtoto wa Nuhu ila ndio alirudisha damu ya wanefili baada ya gharika baada ya Malaika aliyeitwa SHAMAEL siku chache kabla ya gharika alimlala mke wa HAM aliyeitwa Neitamuk na kumpa mimba ya mnefili CANAAN na ndio alisababisha maasi na roho ya shetani kupata nguvu upya immediately baada ya gharika na ndiye alipelekea kuzaa wanefili kama wale wa kabla ya gharika hivyo kwa kuona uovu wa HAM aliofanya, hasira za Nuhu zikaishia kwa CANAAN sababu ndio alikuwa uzao wa roho ya kishetani (SHAMAEL) iliosababisha hadi dhambi kurudi baada ya gharika

BAADA YA LAANA
Tunaona canaan akizaa watoto walioishi miji kama sodoma Gomorrah na Gaza zote israel ya sasa na walikuwa na falme zenye nguvu sana ila kwa kuwa laana hii ya Nuhu iliwafuata ilikuja kutimizwa na watoto wa yakobo (uzao wa SHEM) waliokuja kuwapora nchi yao ya CANAAN na wakawachinja takribani kizazi chote rejea kitabu cha joshua na kumbukumbu la torati na hata wachache waliobaki waliendelea kuteswa sana na waisrael na BIFU hili lilienda hadi kwa Yesu alipokataa kumponya mwanamke wa kanaani

Mathayo 15:22
22 Na tazama, mwanamke Mkanaani wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa


CANAAN NA WANEFILI
Hoja ya kwamba canaan huenda alikuwa uzao wa malaika shamael ama uzao wa ajabu wa Ham na mama yake watoto wake wote walikuwa wanefili yaani majitu ya futi mpaka 28..... Kati ya watoto wote wa ukoo wa Nuhu hakuna mtu aliyezaa wanefili kuliko Canaan na makabila yote ya warefai kipindi hicho walitoka familia ya canaan wawe wayebusi wagilgal waamori wahiti wahivi n.k je huu unaweza kuwa ushahidi kuwa hakuwa mtoto wa uzao wa kawaida ndio maana akazaa wanefili watupu huku na yeye akiwa mnefili???

HAM KWENYE UISLAM
Sijapata popote kwenye Quran inapoandikwa kuhusu laana hii ya Canaan ila kwenye ukristo ma uyahudi ndipo imetajwa. Ila ukisoma hadeeth mbalimbali na machapisho ya wasomi nguli wa kiislam wa mwanzo kabisa kina Muhammad ibn-jarir al tabari pamoja na ibn khaldun wanaeleza kwamba HAM alilaaniwa sababu akiwa kwenye Safina ya Nuhu alimlala mke wake kitu kilichokatazwa hivyo alilaaniwa kwa kupewa ngozi nyeusi na ndio maana watoto wake wote wakawa weusi!!! So hawa angalau wamesema HAM alilaaniwa ila kwa kosa tofauti.... Hivyo bado hawajatupa jibu la kisa cha Nuhu na Canaan

HITIMISHO
Mada hii imetumiwa sana na wazungu wakoloni hasa karne ya 19 kuhalalisha ukoloni wa watu weusi kwa kigezo kuwa mwafrika alilaaniwa ila hoja hii naipinga sababu canaan alilaaniwa peke yake na kizazi chake kwa ukubwa kilishafutwa ila waafrika 80% walitokana na kizazi cha wale watoto 3 wa HAM ambao laana hii haikuwahusu hivyo natumia fursa kupinga propaganda hiyo rasmi na ni vizuri waafrika tupende kusoma historia yetu ili wahuni wachache wasipotoshe ukweli

Naomba kuwasilisha

Karibuni wanajukwaa wote tusaidiane kujadili kuhusu nadharia hizi,
Mada nzuri sana ila kwenye suala la laana kuna mkanganyiko mkubwa nafikir ilikuwa na laana ya pili baada ya ile ya kwanza kula tunda ata huyu Nuhu alikuwa na laaana sasa anawezaje kutoa laana mwenye laana?
 
NB:Mods naomba msihamishe mada hii kwenda jukwaa la dini sababu licha ya kuwa nimequote baadhi ya mistari ya vitabu vya dini ila uzi huu ni mtiririko wa mada zilezile nilizoanza humu JF intelligence kuhusu wanefili na wanadamu wa kale so mkihamisha mtaharibu mtiririko wa mijadala yangu kwa wanaofuatilia.... Ntashkuru kwa ushirikiano wenu

Cc JamiiForums Innovator Invisible Reserved
nadharia zote zimejikita kwenye chanzo kimoja cha imani yaani bibilia.
nilitegemea mkuu utuwekee vyanzo vya talmud au maandiko mengine ya kiyahudi ambayo hayapo kwenye bibilia,quran(umesema hakuna chanzo), Jashar, Enoch, na vya historia nyingine zinazozungumzia sakata hilo. nasema kwa sababu stori uliyoitoa umeitoa kuktoka katka mwanzo 9, na Sababu ya laana imeandikwa hapohapo. ungetoa na vyanzo vingine mtambuka vyenye sababu hizo nyingine ili msawazo wa mada usiegemee kwwnye bibilia tu.

ili litoe sura ya kwamba nadharia zako zote zina biblical support.

Mchango.
Binafsi kwa msingi wa chanzo bibilia, naamini alilaaniwa kwa sababu ya kuona uchi wa baba yake. na ndivyo ilivyoandikwa na kuelezwa humo. kwa mtiririko wa matukio ya bibilia, sio ajabu mtu na dada yake au ndugu yake kufanya mapenzi mara tu baada ya Uumbaji na Gharika ili kuendeleza vizazi na kuijaza nchi. hivyo sioni sababu ya kulinganisha laana za kipindi cha walawi ambacho tayari watu walikuwa wameshakuwa wengi tuiseme itumike kuhukumu watu wa kizazi cha nuhu au adam.
Ikiwa hoja zote zitajengwe kwenye bibilia fact ni moja tu. Ham alilaaniw kwa kuangalia uchi wa baba yake.
maoni mkuu.
 
View attachment 775662
Habari za jioni wanajukwaa....kama kichwa cha uzi kinavyosema ningependa tujadili mada hii Kutokana na hili swali swali kuulizwa mara nyingi kwenye thread zangu nimeona nifungue uzi wake ili tujaribu kulitatua hili swali

Je ni kwanini aliyetenda dhambi ya kumuangulia uchi wa babake ni HAM ila laana ikaenda kwa mwanaye ham aliyeitwa CANAAN....

STORI YENYEWE
Mwanzo 9
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake


Mpaka hapa tunaona anayetajwa kuchungulia uchi ni Ham ila laana inaenda kwa Canaan why?? Embu tusome nadharia hii

NADHARIA #1
Kutoka vyanzo tofauti vya kihistoria na kidini vinaelezea kisa hiki kwamba Nuhu alipolewa Ham hakuona uchi kama uchi ila inaelezwa Ham alilala na Mke wa Nuhu yaani Ham alilala na mama yake mzazi na mwisho wa siku akabeba mimba na akazaliwa Canaan na hii ilipelekea Nuhu amlaani Canaan na sio Ham sababu alikuwa kizazi cha dhambi haramu kabisa..... Na vitabu hivi vinaenda mbali na kusema Ham alimuhasi baba yake alipokuwa amelewa hiyo nayo ikapelekea Nuhu kushindwa kuzaa mtoto mara baada ya gharika!!!

VITABU VYA DINI
Nadharia hii sio tu nje ya vitabu vya dini ila hta vitabu vya dini hasa biblia inaweza kutumika kuijengea hoja embu tuangalie tafsiri yake

Mambo ya walawi 20
11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao

Walawi 18:8
8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako

NB:Kitabu cha mwanzo na mambo ya walawi vyote viliandikwa mwanzoni na Nabii Musa hivyo kama tutachukua tafsiri yake ya ''KUANGALIA UCHI WA BABA YAKO'' inamaanisha kuna ukweli juu ya nadharia hii kuwa Ham alimlala mama yake mzazi/mke wa Nuhu

Na sio kwa baba tuu Musa alielezea zaidi

Walawi 20
20 Tena mtu mume akilala na mke wa mjomba wake, ameufunua utupu wa mjomba wake; watauchukua uovu wao; watakufa bila kuzaa mwana.
21 Tena mtu mume akimtwaa mke wa nduguye, ni uchafu; ameufunua utupu wa nduguye; hao watakuwa hawana wana


Biblia haikuishia hapo ila ukisoma kitabu cha habakuki kinakataza mtu kulewesha jirani yake ili KUMCHUNGULIA UCHI.... Ikimaanisha kama ambayo Ham alimfanyia baba yake alipokuwa amelewa basi ndio hiko anachokataza habakuk ila sio kuchungulia kwa macho kama wengi tulivyoaminishwa

Habakkuk 2:15
15 Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao!

Mistari iko mingi zaidi ya 10 inayoeleza kwamba kumchungulia kaka baba au mjomba wako ni kulala na mke wake hivyo wa waliouliza swali hili naona tunaweza conclude kwa nadharia hii kuwa HAM alimlala mke wa NUHU ndio baada ya kuja kujua alichofanya na mimba aliobeba akamlaani Canaan sababu ndio zao la dhambi hiyo iliotendeka

NADHARIA #2
Ukisoma vitabu vya dini ya kiyahudi kma midrash vinasema Canaan aliona Nuhu akiwa uchi hivyo akaenda kumuhasi kwa kutumia kamba na alipotoka ndio baadae Ham alikuta Nuhu akiwa amevuliwa nguo yeye akaishia kucheka tu badala ya kumfunika na mwisho wa siku ndipo laana akapewa Canaan kwa kufanya hicho kitendo

NADHARIA #3
Hapa inadaiwa na wanatheolojia kuwa mwandishi wa kitabu hiki alikuwa anatafuta sababu ya kuhalalisha uvamizi wa israel kwenye nchi ya Canaan so akapachika jina Canaan badala ya HAM ili ahalalishe uvamizi wa israel kwa kigezo cha kwamba NENO LA MUNGU LILIANDIKA!!!

NADHARIA #4
Inasema Canaan hakuwa mtoto wa Nuhu ila ndio alirudisha damu ya wanefili baada ya gharika baada ya Malaika aliyeitwa SHAMAEL siku chache kabla ya gharika alimlala mke wa HAM aliyeitwa Neitamuk na kumpa mimba ya mnefili CANAAN na ndio alisababisha maasi na roho ya shetani kupata nguvu upya immediately baada ya gharika na ndiye alipelekea kuzaa wanefili kama wale wa kabla ya gharika hivyo kwa kuona uovu wa HAM aliofanya, hasira za Nuhu zikaishia kwa CANAAN sababu ndio alikuwa uzao wa roho ya kishetani (SHAMAEL) iliosababisha hadi dhambi kurudi baada ya gharika

BAADA YA LAANA
Tunaona canaan akizaa watoto walioishi miji kama sodoma Gomorrah na Gaza zote israel ya sasa na walikuwa na falme zenye nguvu sana ila kwa kuwa laana hii ya Nuhu iliwafuata ilikuja kutimizwa na watoto wa yakobo (uzao wa SHEM) waliokuja kuwapora nchi yao ya CANAAN na wakawachinja takribani kizazi chote rejea kitabu cha joshua na kumbukumbu la torati na hata wachache waliobaki waliendelea kuteswa sana na waisrael na BIFU hili lilienda hadi kwa Yesu alipokataa kumponya mwanamke wa kanaani

Mathayo 15:22
22 Na tazama, mwanamke Mkanaani wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa


CANAAN NA WANEFILI
Hoja ya kwamba canaan huenda alikuwa uzao wa malaika shamael ama uzao wa ajabu wa Ham na mama yake watoto wake wote walikuwa wanefili yaani majitu ya futi mpaka 28..... Kati ya watoto wote wa ukoo wa Nuhu hakuna mtu aliyezaa wanefili kuliko Canaan na makabila yote ya warefai kipindi hicho walitoka familia ya canaan wawe wayebusi wagilgal waamori wahiti wahivi n.k je huu unaweza kuwa ushahidi kuwa hakuwa mtoto wa uzao wa kawaida ndio maana akazaa wanefili watupu huku na yeye akiwa mnefili???

HAM KWENYE UISLAM
Sijapata popote kwenye Quran inapoandikwa kuhusu laana hii ya Canaan ila kwenye ukristo ma uyahudi ndipo imetajwa. Ila ukisoma hadeeth mbalimbali na machapisho ya wasomi nguli wa kiislam wa mwanzo kabisa kina Muhammad ibn-jarir al tabari pamoja na ibn khaldun wanaeleza kwamba HAM alilaaniwa sababu akiwa kwenye Safina ya Nuhu alimlala mke wake kitu kilichokatazwa hivyo alilaaniwa kwa kupewa ngozi nyeusi na ndio maana watoto wake wote wakawa weusi!!! So hawa angalau wamesema HAM alilaaniwa ila kwa kosa tofauti.... Hivyo bado hawajatupa jibu la kisa cha Nuhu na Canaan

HITIMISHO
Mada hii imetumiwa sana na wazungu wakoloni hasa karne ya 19 kuhalalisha ukoloni wa watu weusi kwa kigezo kuwa mwafrika alilaaniwa ila hoja hii naipinga sababu canaan alilaaniwa peke yake na kizazi chake kwa ukubwa kilishafutwa ila waafrika 80% walitokana na kizazi cha wale watoto 3 wa HAM ambao laana hii haikuwahusu hivyo natumia fursa kupinga propaganda hiyo rasmi na ni vizuri waafrika tupende kusoma historia yetu ili wahuni wachache wasipotoshe ukweli

Naomba kuwasilisha

Karibuni wanajukwaa wote tusaidiane kujadili kuhusu nadharia hizi,
Mkuu uz nimeuelewa usiache kun tag mkuu zisiwe zinanipita nyuz kama hiz
 
nadharia zote zimejikita kwenye chanzo kimoja cha imani yaani bibilia.
nilitegemea mkuu utuwekee vyanzo vya talmud au maandiko mengine ya kiyahudi ambayo hayapo kwenye bibilia,quran(umesema hakuna chanzo), Jashar, Enoch, na vya historia nyingine zinazozungumzia sakata hilo. nasema kwa sababu stori uliyoitoa umeitoa kuktoka katka mwanzo 9, na Sababu ya laana imeandikwa hapohapo. ungetoa na vyanzo vingine mtambuka vyenye sababu hizo nyingine ili msawazo wa mada usiegemee kwwnye bibilia tu.

ili litoe sura ya kwamba nadharia zako zote zina biblical support.

Mchango.
Binafsi kwa msingi wa chanzo bibilia, naamini alilaaniwa kwa sababu ya kuona uchi wa baba yake. na ndivyo ilivyoandikwa na kuelezwa humo. kwa mtiririko wa matukio ya bibilia, sio ajabu mtu na dada yake au ndugu yake kufanya mapenzi mara tu baada ya Uumbaji na Gharika ili kuendeleza vizazi na kuijaza nchi. hivyo sioni sababu ya kulinganisha laana za kipindi cha walawi ambacho tayari watu walikuwa wameshakuwa wengi tuiseme itumike kuhukumu watu wa kizazi cha nuhu au adam.
Ikiwa hoja zote zitajengwe kwenye bibilia fact ni moja tu. Ham alilaaniw kwa kuangalia uchi wa baba yake.
maoni mkuu.
Mkuu mitale na midimu kwenye nyuzi yangu mbona nimeweka source kutoka vitabu vya kiyahudi MIDRASH na kwenye uislam nmetoa kwenye waandishi wa HADEETH za kiislam na source nimeweka hivyo mada haijabase kwenye biblia tu...... However nimeweka biblia sababu ndio kirefu inajadili laana hii kwenye maandiko yake mengine

Hoja yako kusema alimchungulia je tueleze kivipi HAM amchungulie alafu alaaniwe CANAAN what's the logic kma aliyechungulia mwingine na aliyelaaniwa mwingine?? Huoni biblia itakua inajichanganya yenyewe??

Na ndio maana kwa sintofahamu hii nikaona tujiulize je kwanini canaan na sio HAM ndio nikasoma DEFINITION ya KUMCHUNGULIA MJOMBA BABU BABA maana yake ni nini.... Ndio Manabii habbakuk musa na Ezekieli wote wanasema KUMCHUNGULIA mtu maana yake ni kulala na mke wake ndio maana nikajengea hoja huenda MUSA kama alivyomaanisha KUMCHUNGULIA baba yako kwenye WALAWI na TORATI basi pia kwa kuwa aliandika kitabu cha mwanzo alimaanisha hivo hivo kuwa HAM alilala na mama yake ndio maana mimba ya mtoto aliyezaliwa yaani CANAAN akalaaniwa

Ukisoma pia Quran Surat ya Hud.... Inamtambua Nabii Nuhu kama ana watoto wanne na jina lake ukilibadilisha kiebrania inakuwa Kahnan same as CANAAN hivyo huoni bado kama CANAAN alitambuliwa na QURAN kama mtoto wa NUHU (sababu ni mtoto wa mke wa Nuhu) haiwezi elezea pia scenario hii

However kwa hoja yako siwezi kupinga ila naomba tusaidie kwa faida ya Jukwaa zima

KWANINI HAM ASILAANIWE KWA DHAMBI ALIYOFANYA ILA AKALAANIWA CANAAN

Barikiwa
 
Mkuu mitale na midimu kwenye nyuzi yangu mbona nimeweka source kutoka vitabu vya kiyahudi MIDRASH na kwenye uislam nmetoa kwenye waandishi wa HADEETH za kiislam na source nimeweka hivyo mada haijabase kwenye biblia tu...... However nimeweka biblia sababu ndio kirefu inajadili laana hii kwenye maandiko yake mengine

Hoja yako kusema alimchungulia je tueleze kivipi HAM amchungulie alafu alaaniwe CANAAN what's the logic kma aliyechungulia mwingine na aliyelaaniwa mwingine?? Huoni biblia itakua inajichanganya yenyewe??

Na ndio maana kwa sintofahamu hii nikaona tujiulize je kwanini canaan na sio HAM ndio nikasoma DEFINITION ya KUMCHUNGULIA MJOMBA BABU BABA maana yake ni nini.... Ndio Manabii habbakuk musa na Ezekieli wote wanasema KUMCHUNGULIA mtu maana yake ni kulala na mke wake ndio maana nikajengea hoja huenda MUSA kama alivyomaanisha KUMCHUNGULIA baba yako kwenye WALAWI na TORATI basi pia kwa kuwa aliandika kitabu cha mwanzo alimaanisha hivo hivo kuwa HAM alilala na mama yake ndio maana mimba ya mtoto aliyezaliwa yaani CANAAN akalaaniwa

Ukisoma pia Quran Surat ya Hud.... Inamtambua Nabii Nuhu kama ana watoto wanne na jina lake ukilibadilisha kiebrania inakuwa Kahnan same as CANAAN hivyo huoni bado kama CANAAN alitambuliwa na QURAN kama mtoto wa NUHU (sababu ni mtoto wa mke wa Nuhu) haiwezi elezea pia scenario hii

However kwa hoja yako siwezi kupinga ila naomba tusaidie kwa faida ya Jukwaa zima

KWANINI HAM ASILAANIWE KWA DHAMBI ALIYOFANYA ILA AKALAANIWA CANAAN

Barikiwa
safi sana mkuu. umeeleza vizuri.
napita tena kudondosha maoni mkuu.
ngoja nijifunze zaidi.
barikiwa zaidi.
 
Hivi inakuwaje kosa afanye mtu mwingine then adhabu apewe mwingine? hii imekaaje? Sometimes Bible huwa siielewi yani
Haahahaaa ngoja wataalam waje majibu tutapata hapahapa.... Ila kwa mtazamo wangu hizo nadharia hapo juu zinaweza kuchangia ila kwa hatua nyingine mtu anaweza laani asiyehusika sababu ANAANGALIA CHANZO mfano Nyoka alimdanganya hawa ndio maana laana akapewa Nyoka pia ingawa kosa alifanya HAWA na hata sasa inawezekana Kosa akafanya waziri wa Tanzania alafu lawama ikaenda kwa MAGUFULI kwa sababu hiyo hiyo

Ngoja wataalam waje CC: SALA NA KAZI Che mittoga Online Pastor
 
Kuna hoja nyingi sana kwenye hii mada chief, hoja zote ulizoandika hapa zina mantiki na zimenipa maswali mengi...

Lkn kuna sababu moja nionhezee hapo, wakati wa gharika watoto wakubwa wa Nuhu yanj Japhet na Shem wao walikua na wake ambao walitokea kwenye kabila ambazo Mungu na Nuhu walizikubali.....ila kwa upande wa Ham yeye hakuwa na mke wa upande huo, inaelezwa kwamba akatafuta mwanamke wa uoande wa waNefili ambao walikataliwa na Mungu pamoja na Nuhu,

Inasemekana Ham alifosi mpaka kuingia nae kwenye safina...na hapo nimeona umesema kwamba alizini nae ndani ya safina pia hivyo ikapelekea kuamsha hasira ya Mungu juu ya Nuhu kwa kushindwa kumzibiti Ham,

Inaelezwa ndio sababu Nuhu akatofautiana sana na Ham hata baada ya gharika kuisha.

Hii stori ya Nuhu na uzao wake ipo deep sana...natamani kujua zaidi, ngoja tusubiri wajuzi zaidi waje kutufunulia mambo hapa.

Asante kwa uzi mzuri.
 
Mkuu mitale na midimu kwenye nyuzi yangu mbona nimeweka source kutoka vitabu vya kiyahudi MIDRASH na kwenye uislam nmetoa kwenye waandishi wa HADEETH za kiislam na source nimeweka hivyo mada haijabase kwenye biblia tu...... However nimeweka biblia sababu ndio kirefu inajadili laana hii kwenye maandiko yake mengine

Hoja yako kusema alimchungulia je tueleze kivipi HAM amchungulie alafu alaaniwe CANAAN what's the logic kma aliyechungulia mwingine na aliyelaaniwa mwingine?? Huoni biblia itakua inajichanganya yenyewe??

Na ndio maana kwa sintofahamu hii nikaona tujiulize je kwanini canaan na sio HAM ndio nikasoma DEFINITION ya KUMCHUNGULIA MJOMBA BABU BABA maana yake ni nini.... Ndio Manabii habbakuk musa na Ezekieli wote wanasema KUMCHUNGULIA mtu maana yake ni kulala na mke wake ndio maana nikajengea hoja huenda MUSA kama alivyomaanisha KUMCHUNGULIA baba yako kwenye WALAWI na TORATI basi pia kwa kuwa aliandika kitabu cha mwanzo alimaanisha hivo hivo kuwa HAM alilala na mama yake ndio maana mimba ya mtoto aliyezaliwa yaani CANAAN akalaaniwa

Ukisoma pia Quran Surat ya Hud.... Inamtambua Nabii Nuhu kama ana watoto wanne na jina lake ukilibadilisha kiebrania inakuwa Kahnan same as CANAAN hivyo huoni bado kama CANAAN alitambuliwa na QURAN kama mtoto wa NUHU (sababu ni mtoto wa mke wa Nuhu) haiwezi elezea pia scenario hii

However kwa hoja yako siwezi kupinga ila naomba tusaidie kwa faida ya Jukwaa zima

KWANINI HAM ASILAANIWE KWA DHAMBI ALIYOFANYA ILA AKALAANIWA CANAAN

Barikiwa
mkuu nimefuatilia kwa ufupi, nimegundua kuna nadharia rundo kuhusu hilo tukio.
na wengine wameenda mbali nadhani umekwepa kuiandika kwa sababu ya kimaadili Huyo Ham alimsodoma (homosexuality) baba yake au hiyo hoja ya castration pia. hii ni kwa mujibu wa babylonian talmud na tafsiri za baadhi ya marabbi. wameenda mbali hadi kutafsiri neno la kigiriki (kutoka kwenye septugiant ) "akamuona" wametafsiri au weka maana ya kimapenzi zaidi.

MAONI YANGU ZAIDI:
Naendelea kujikita kwenye maandiko matakatifu (bibilia ) tu kujenga baadhi ya hoja.

1:Hakuna mambo ya kusodomana, wala kuziniana kwenye hilo tukio, nadhalia hizo naona zinamadhaifu hata jitihada za kuzihusianisha na aya za mbele zisizoumana kimaana.

2: Kwa nini Ham asilaaniwe alaaniwe mwanaye?
*Kumbuka laana hiyo imetolewa na Nuhu sio Mungu. hivyo inatufikirisha zaidi.
*Mungu alikuwa amekwishambariki HAMU.
" Naye Mungu akambariki Noa na wanawe(ham,shem na yapheti), akawaambia: “Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia." Mwanzo 9:1
hapo ni wazi Mungu kambariki HAMU hivyo laana ya nuhu inaweza isifanye kazi, na wenda imeandikwa kuwa inaenda kwa kaanani kwa sababu ndio mzao wake ambae alikuwa hana hizo baraka zilizotolewa na Mungu.
Maoni haya ambayo nayaunga mkono yanaumana na Magombo ya kale yaliyochimbuliwa (dead sea scrolls 4Q252) wakizungumzia tukio hilo.

3:Maoni ya mwanahistoria wa kiyahudi ambaye anatambulika kwa wananzuoni Josephus anasema nuhu hakumlaani HAM kwa sababu ya ukaribu wao hivyo akaamua badala yake amlaani mtoto wa mtoto wake. (maoni haya yanaweza kuleta mantiki ukijumuisha na yale ya mwanzo9:1).


TUKIRUDI KWENYE BIBILIA
kwa sababu ya ukinzani wa nadhalia nyiiingi ambazo nimegundua kuna maelfu ya watu, wasomi wameamua kupiga kambi mahala ambapo bibilia imenyamaza na wao kupajaza na kupashindilia na nadhalia lukuki inanifanya niamini facts ni zile zilizoandikwa katika bibilia.

1:Nuhu alilewa.
2:Kwa Mujibu wa Bibilia Kulewa ni Dhambi (walevi hawatairithi nchi, isipokuwa wametubu. 1Cor6:9-18)
3:Mtoto wake Ham alimchungulia aliuona UCHI wa baba yake.
4:Nuhu sio Mungu, akaamua kumlaani mtoto wa Ham Kaanani kwa sababu zake aliporudiwa na fahamu.
5:Ukiangalia ndugu zake hamu walikuja kumfunika uchi wa baba yao bila kuuangalia, kwa mtiririko wa matukio utaona hakuna element yoyote ya ngono katika tukio hilo lililohusisha wanaume wanne.
5:Hakuna Ushahidi kuwa Laana hiyo ya kifamilia inauhusiano na Uweusi wetu katika bibilia.

magap katkati ya hizo biblical facts yanaweza kujazwa na nadharia yoyote ile mkuu.

nyongeza ya maoni, katikati ya nadharia zote nashikilia hizo biblical facts kama msingi mkuu.

barikiwa mkuu.
 
48 Reactions
Reply
Back
Top Bottom