Kwanini bunge letu lisivunjwe katika mabunge mawili?

Godwine

JF-Expert Member
Jan 15, 2010
1,371
281
Nadhani imefika wakati wa kuligawa Bunge letu katika sehemu mbili ili kuongeza ufanisi na kupunguza madhaifu yanayojitokeza kwa sasa kwani bunge moja linakuwa limeshehena kazi nyingi kupita uwezo wa mipango yake . nionavyo mimi tunaweza kuwa na mabunge mawili ambayo kila moja linaweza kuwa na wawakilishi kama 120 na kuwa na majukumu yake kuliko kuendelea kuwa na bunge moja ambalo zaidi ya asilimia 90% ya wabunge wake wanakuwa wamelala wakati miswada ikiwa inaendelea. tukiwa na mabunge mawili yenye wajumbe wachache inaweza kufanya wabunge wengi kuwa wafuatiliaji na kuongeza ufanisi na usimamizi na ata ufuatiliaji wa mikataba inayoliumiza taifa letu.
 
Heshima mbele mkuu Godwine. Mkuu ukiangalia nchi karibia zote zenye mabunge mawili una kuta hao wana fuata mfumo wa federal government. Kwa maana serikali kuu ina mamlaka yake na serikali za majimbo nazo zina mamlaka yake yanayo jitegemea. Maana ya kuwa na mabunge kwenye federal states ni hivi. Labda nitoe mfano wa Marekani.

1)Bunge moja lina fuata uwakilishi wa watu. Kwamba mbunge mmoja ana wakilisha watu wa idadi fulani. Kwa Marekani hii ni Congress ambao wawakilishi wao wana toka kwenye constituencies na kila Constituency ina wakilisha watu wa idadi fulani. Hii ina maana majimbo yenye watu wengi zaidi ina toa wawakilishi wengi zaidi.

2)Bunge la pili ni la majimbo. Kwa maana haijalishi ukubwa wa jimbo lakini kila jimbo lina toa idadi fulani ya wabunge. Kwa Marekani hii ni senate anbalo kila jimbo lina toa maseneta wawili au watatu kama sikosei. Hii ina toa balance kwa Congress kwa maana hata majimbo madogo inapo kuja kwenye senate wana nguvu na uwakilishi sawa na majimbo makubwa in theory.

Sasa kwa nchi kama ya kwetu kuwa na mabunge mawili yanayo fuata practicality ina maana mikoa nayo lazima iwe na nguvu na chaguzi inayo jitegemea. Kwa maana mkuu wa mkoa ana chaguliwa na wananchi na si raisi na serikali ya mkoa ina kuwa na mamlaka ambayo haitegemei serikali kuu. Sasa hivi serikali za mikoa zinafuata tu maagizo ya serikalo kuu.

Just a foot note: Kwa Tanzania chama kinacho unga mkono serikali ya majimbo ni Chadema kama ilivyo ainishwa kwenye ilani yao mwaka 2005 na kupiganiwa na mwenyekiti wao Freeman Mbowe.
 
Miaka miwili toka kutolewa wazo la kuwa na Mabunge mawili CCM kupitia kikao chake cha chama CC na NEC wameamua kulifanyia kazi, ni vema wameliona hili lakini kikubwa ni waweke mfumo madhubuti ya upatikanaji wa mabunge yenye nguvu na si mihuri ya watawala
 
Heshima mbele mkuu Godwine. Mkuu ukiangalia nchi karibia zote zenye mabunge mawili una kuta hao wana fuata mfumo wa federal government. Kwa maana serikali kuu ina mamlaka yake na serikali za majimbo nazo zina mamlaka yake yanayo jitegemea. Maana ya kuwa na mabunge kwenye federal states ni hivi. Labda nitoe mfano wa Marekani.

1)Bunge moja lina fuata uwakilishi wa watu. Kwamba mbunge mmoja ana wakilisha watu wa idadi fulani. Kwa Marekani hii ni Congress ambao wawakilishi wao wana toka kwenye constituencies na kila Constituency ina wakilisha watu wa idadi fulani. Hii ina maana majimbo yenye watu wengi zaidi ina toa wawakilishi wengi zaidi.

2)Bunge la pili ni la majimbo. Kwa maana haijalishi ukubwa wa jimbo lakini kila jimbo lina toa idadi fulani ya wabunge. Kwa Marekani hii ni senate anbalo kila jimbo lina toa maseneta wawili au watatu kama sikosei. Hii ina toa balance kwa Congress kwa maana hata majimbo madogo inapo kuja kwenye senate wana nguvu na uwakilishi sawa na majimbo makubwa in theory.

Sasa kwa nchi kama ya kwetu kuwa na mabunge mawili yanayo fuata practicality ina maana mikoa nayo lazima iwe na nguvu na chaguzi inayo jitegemea. Kwa maana mkuu wa mkoa ana chaguliwa na wananchi na si raisi na serikali ya mkoa ina kuwa na mamlaka ambayo haitegemei serikali kuu. Sasa hivi serikali za mikoa zinafuata tu maagizo ya serikalo kuu.

Just a foot note: Kwa Tanzania chama kinacho unga mkono serikali ya majimbo ni Chadema kama ilivyo ainishwa kwenye ilani yao mwaka 2005 na kupiganiwa na mwenyekiti wao Freeman Mbowe.

hatimaye mawazo yamefika kwenye katiba sasa
 
Back
Top Bottom