Kwanini bidhaa nyingi zinazoagizwa kuja barani Afrika zinatokea China isipokuwa magari ambayo yanatokea Japan?

Kikawaida kama China ingekuwa nchi iliyoendelea bado watu wangeweza kununua kwa wingi magari used kutoka China. Mafano ni nchi za Uarabuni. Hazitengenezi magari lakini bado ni maarufu kwa watu kwenda kununua magari used ambayo mengi yamenunuliwa mapya kutoka nchi nyingine. Lakini hali haiko hivyo kwa upande wa China kwa sababu China nayo ni choka mbaya.
Unafafanua vizuri sana mkuu. Asante kaka mkubwa. Sasa mkuu ina maana kuna baadhi ya wachina wanaagiza magari "second-hand" kutoka katika nchi zingine na kuendesha huko kwao?...
 
Unafafanua vizuri sana mkuu. Asante kaka mkubwa. Sasa mkuu ina maana kuna baadhi ya wachina wanaagiza magari "second-hand" kutoka katika nchi zingine na kuendesha huko kwao?...
Ndiyo mkuu. China japokuwa unaona ina export bidhaa kwa wingi lakini maisha ya wananchi wake bado hayako standard ya nchi zilizoendelea. Ulaya tunapigana nao vikumbo sana kwenye kutafuta maisha mazuri. Hebu jiulize kwa nini wachina wamejaa sana Bongo? Tena wameanza kuja siku hizi hizi tu. Hawa jamaa na wahindi hakuna tofauti.
 
Kuna baadhi ya wadau humu ndani wanadai ya kwamba gari "second-hand" ya mchina inakuwa imechoka sana kiasi kwamba haifai kuja Afrika tofauti na gari ya mjapan...
Hapana China nao walikuwa wagizaji wa magari ya Ulaya sana wameingia kwenye soko la utengenezaji wa magari kwa ajili ya kuuza miaka ya hivi karibuni na taarifa kuna mawakala Tayari wa makari madogo ya kichina
 
Unafafanua vizuri sana mkuu. Asante kaka mkubwa. Sasa mkuu ina maana kuna baadhi ya wachina wanaagiza magari "second-hand" kutoka katika nchi zingine na kuendesha huko kwao?...
Gari zote zinazo agizwa na Wachina sio za bei ndogo wala mchina mwenye kipata cha kawaida hawezi agiza gari ya nje ya China!
Matajiri wa kichina ndio huagiza magari ya Ulaya na huwa ni mapya tajiri wa kichina huwezi mjuwa kwa uvaaji utamjuwa kwa gari anayo endesha na sio jambo jingine!
Pia huamini akiwa na mgeni akimchukuwa kwenye gari ya bei kubwa ndio ata mwamini zaidi!
Mwenyewe binafsi nimepanda gari za dola 7laki saba nikiwa China
Na kuendesha baiskeli za dola 2000 ndani ya viwanda vya china!
 
Miaka ya 80,90 bidhaa nyingi zilikuwa zinatoka Japan na ulaya wahitaji na waliyokuwa na uwezo wa ku afford walikuwa wachache,mchina kachungulia na na akagundua wahitaji ni wengi ndy akaja na bidhaa ambazo zinamgusa kila mtu kwenye kununua

Ova
 
Mchina gari ndogo hana matoleo mengi kuna hizo Great Wall,Foton, Haval.
Kwa Africa tumezoea Second Hand Car, mchina gari take ukinunua second hand inabidi ujipange ni nzuri Kwa mtumiaji wa Kwanza.
Kila nchi inajaribu kuzalisha bidhaa kwa gharama nafuu ili kupata soko kubwa. Kwa mfano, China inatengeneza samani, compyuta, nguo, vifaa vya umeme n.k. ambavyo vinauzika sana Afrika. N pia bei zake si kubwa kama za bidhaa nchi za Ujerumani, Uingereza au Ilatia.
 
Labda hazipo imara, sisi waafrica tumeshazoea kupokezana magari, ukiangalia mfano mabus ya kichina matajiri wananunua mapya kabisa kutokana na bei nzuri ila yakifika miaka 10 yanachoka knoma, anaelipokea linamsumbua
 
Kila nchi inajaribu kuzalisha bidhaa kwa gharama nafuu ili kupata soko kubwa. Kwa mfano, China inatengeneza samani, compyuta, nguo, vifaa vya umeme n.k. ambavyo vinauzika sana Afrika.
Mkuu, kwani mchina hawezi kutengeneza gari za dola 3,000 akauza Afrika?...
 
Ila zile Foton SUV wanazotumia maRPC inaonekana ziko poa na bei nafuu, sijui zilikuwa ni msaada au manunuzi yetu tu. Mwenye uzoefu nazo azielezee, hata kama ni RPC wewe zielezee tu.
Rafiki yangu mbona unatuchokoza lakini hebu acha tuyatumie. Ni makusanyo tu yandani
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu Jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Kwanini bidhaa nyingi zinazoagizwa kuja barani Afrika (Tanzania) zinatokea China isipokuwa magari ambayo yanatokea Japan?

View attachment 1634465

Ukiwa upo katika foleni ya magari barabarani, jaribu kufanya tathmini ya haraka haraka kwa kuangalia tu kwa macho kisha utagundua hizi ninachokisema.

Utagundua ya kuwa 98% ya gari zilizopo hapo ni za kutoka Japan (Toyota, Honda, Nissan, Suzuki, Mazda, Mitsubishi, Subaru, Isuzu) lakini bidhaa zingine madukani ni za kutoka nchini China. Why this? What's wrong with chinese automobile industry?

TAKWIMU NDOGO YA BIASHARA BAINA YA CHINA NA AFRIKA KWA MWAKA 2019
=====
According to statistics from the General Administration of Customs of China, in January-June, China’s total import and export volume with Africa was US$101.86 billion, up 2.9% year on year, exceeding the overall growth rate of foreign trade in the same period by 4.9 percentage points.

View attachment 1634490

Among these, China’s exports to Africa were US$52.86 billion, up 5.2% year on year and China’s imports from Africa were US$49.00 billion, up 0.5% year on year; the trade surplus was US$3.86 billion, up 159.0% year on year.

In June, China’s total import and export volume with Africa was US$17.09 billion, up 2.3% year on year. Among these, China’s exports to Africa were US$9.29 billion, up 0.3% year on year; China’s imports from Africa were US$7.79 billion, up 4.7% year on year; the trade surplus was US$1.50 billion, down 17.6% year on year.

In January-June, the growth rate of China’s trade with Africa was lower than those with Oceania(6.2%) and Europe(3.9%).
=====

View attachment 1634489

Kwanini magari kutoka China sio bidhaa maarufu hapa Africa (Tanzania) kama bidhaa zingine (domestic products) zilizojaa katika masoko/maduka yetu?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
M-TAG mwijage n viwanda vyake 3000 kila mkoa.
Mta- MATAGS mkuu , na wengine wote wanaosema tunaweza kujitegemea kwa maneno huku kila siku wakipokea misaada tena bila kutuambia , kama ile bilioni 70 ya kupambana na korona kumbe ndio wakachapishia kura feki na kulipa MATAGA waliokuwa wanaziingiza vituoni.
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom