Kwanini biashara ya kuzalisha na kusambaza umeme isiwe biashara huria ili TANESCO ishindane na makampuni binafsi?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Wadau, hivi kuna ugumu gani sisi kama nchi tukawa na sera ya kuruhusu makampuni binafsi kusambaza na kuuza umeme kwa wateja badala ya makampuni haya kuruhusiwa kuzalisha umeme tu na kisha kulazimika kuwauzia TANESCO ambao ndio wenye haki pekee ya kusambaza na kuuza umeme hapa nchi?

Faida ya kuwa na sera ya aina hii ni kama hizi zifuatazo:

1.Makampuni binafsi yakiuza umeme moja kwa moja kwa wananchi, bei bila shaka itashuka.

2.Tutakuwa tume-create ushindani hivyo mbali na bei kushuka, ubora wa huduma pia utaongezeka.

3.Serikalii itapata mapato kutoka katika makampuni binafsi yatayokuwa yakilipa kodi serikali.

4.Makampuni binafsi, kupitia sera hiyo, yanaweza pia kuwekaza katika eneo moja tu la kujenga miundombinu ya kusafirisha umeme na makampuni mengine yakatumia miundombinu hiyo na hivyo tunaweza kuondokana na tatizo la kukatika umeme kutokana na uchakavu wa miundombinu ya TANESCO.

5.Ajira zitazalishwa kupitia makampuni haya binafsi yanayoweza ku-opparate kwa ngazi ya wilaya, mkoa, kanda na hata ngazi ya kitaifa kutegemeana na uwezo na mtaji wa kampuni husika.

6. TANESCO itapunguziwa mzigo wa kuhudumia nchi nzima na hivyo inaweza kujiendesha kwa faida tofauti na ilivyo sasa.

7. Serikalini itaondokana na mzigo wa kuibeba TANESCO na kuokoa fedha nyingi za umma zinazoelekezwa katika kusaidia TANESCO.

8.TANESCO inaweza kutumia miundombinu yake kibiashara kwa makampuni mapya yanayoweza kutumia miundombinu ya TANESCO kwa malipo ya kibiashara.

9.Serikali inaweza pia kufanya biashara ya kuuza kwa makampuni binafsi ya kusambaza umeme kutoka katika vyanzo vyake vya kuzalisha umeme mfano Stieglers Gorge ikikamilika.

Tofauti na hapo, ni bora lile wazo la kuivunja TANESCO na kuwa na makampuni matatu ya kuzalisha,kusambaza na kuuza umeme likafanyiwa kazi kuondoa hii monopoly ya TANESCO katika hii biashara ya kuzalisha na kusambaza umeme.
 
Hahaha mmeona yaliyotokea kwenye siasa, ccm wameshindwa kushindana wakaweka mpira kwapani.

Mnataka kushindana na TANESCO mmesahau ya RICHMOND > Dowans> Simbion.

Mmeona yanayowakuta kina Seth Singh na Rugemalila na IPTL hayatoshi.

Mtaambiwa ruksa mkisha wekeza miundombinu mnaanza kushinda MAHAKAMANI hata kabla hamjaanza uzalishaji.

Kwanini watanzania wepesi wa kusahau hivi?!

Mna ule ugonjwa unaitwa AMNESIA?!
 
Hahaha mmeona yaliyotokea kwenye siasa, ccm wameshindwa kushindana wakaweka mpira kwapani.

Mnataka kushindana na TANESCO mmesahau ya RICHMOND > Dowans> Simbion.

Mmeona yanayowakuta kina Seth Singh na Rugemalila na IPTL hayatoshi.

Mtaambiwa ruksa mkisha wekeza miundombinu mnaanza kushinda MAHAKAMANI hata kabla hamjaanza uzalishaji.

Kwanini watanzania wepesi wa kusahau hivi?!

Mna ule ugonjwa unaitwa AMNESIA?!
Sijui kama umesoma na kuelewa hii mada.
 
Upo sawa mkuu! Hili suala hata mie naona tunajichelewesha bure ni kama ilivyokuwa miaka ya nyuma wakati tukitumia visimu vya TTCL, kwanza ghara za mawasiliano zilikuwa kubwa sana alafu ufanisi ulikuwa mdogo sana eti mtu kupiga simu mpaka postermaster akuunganishe na receiver wako,! Lakini tangu teknolojia ya simu za mikononi iingie tumepiga hatua kubwa sana, simu zinauzwa hadi machinga wa mitaani na hata gharama na ufanisi wa mawasiliano ni mzuri!
TANESCO wangejifunza kutoka TTCL.
 
Upo sawa mkuu! Hili suala hata mie naona tunajichelewesha bure ni kama ilivyokuwa miaka ya nyuma wakati tukitumia visimu vya TTCL, kwanza ghara za mawasiliano zilikuwa kubwa sana alafu ufanisi ulikuwa mdogo sana eti mtu kupiga simu mpaka postermaster akuunganishe na receiver wako,! Lakini tangu teknolojia ya simu za mikononi iingie tumepiga hatua kubwa sana, simu zinauzwa hadi machinga wa mitaani na hata gharama na ufanisi wa mawasiliano ni mzuri!
TANESCO wangejifunza kutoka TTCL.
Na bahat mbaya tumesharidhika na kuona hii ni sawa tu kwa TANESCO kuhodhi hii biashaara.
 
Sisi si taifa la kijamaa!? Kanuni za kijamaa haziruhusu hilo.
Tutaendelea kuwa masikini tu kisa sera hizi mbovu za kijamaa na ambazo ni outdated. Hata wachina wanaokumbatia ujamaa, sera za aina hii sidhani kama bado wanazikumbatia.
 
Tutaendelea kuwa masikini tu kisa sera hizi mbovu za kijamaa na ambazo ni outdated. Hata wachina wanaokumbatia ujamaa, sera za aina hii sidhani kama bado wanazikumbatia.
Bila kuukana ujamaa hadharani na kwenye katiba hatuwezi fika popote. Sheria zetu zote zinaundwa kufuata msingi huo. Watu wanasema tunafuata ujamaa jina tu, si kweli.bado hangover ya ujamaa ipo. Inabidi kuukana rasmi.
 
Kwani sasa hivi makampuni binafsi yamezuiwa kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme kwa wananchi??? Unawajua kwa mfano LUMAMA, MVC, Mwenga wanafanya biashara gani kwa sasa
 
Kwani sasa hivi makampuni binafsi yamezuiwa kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme kwa wananchi??? Unawajua kwa mfano LUMAMA, MVC, Mwenga wanafanya biashara gani kwa sasa
Sijajua kuhusu hizo kampuni!

Ninachojua tanesco ni monopoly kwenye umeme wa Tanzania

By the way nakubaliana na mleta mada
 
Wadau, hivi kuna ugumu gani sisi kama nchi tukawa na sera ya kuruhusu makampuni binafsi kusambaza na kuuza umeme kwa wateja badala ya makampuni haya kuruhusiwa kuzalisha umeme tu na kisha kulazimika kuwauzia TANESCO ambao ndio wenye haki pekee ya kusambaza na kuuza umeme hapa nchi?

Faida ya kuwa na sera ya aina hii ni kama hizi zifuatazo:

1.Makampuni binafsi yakiuza umeme moja kwa moja kwa wananchi, bei bila shaka itashuka.

2.Tutakuwa tume-create ushindani hivyo mbali na bei kushuka, ubora wa huduma pia utaongezeka.

3.Serikalii itapata mapato kutoka katika makampuni binafsi yatayokuwa yakilipa kodi serikali.

4.Makampuni binafsi, kupitia sera hiyo, yanaweza pia kuwekaza katika eneo moja tu la kujenga miundombinu ya kusafirisha umeme na makampuni mengine yakatumia miundombinu hiyo na hivyo tunaweza kuondokana na tatizo la kukatika umeme kutokana na uchakavu wa miundombinu ya TANESCO.

5.Ajira zitazalishwa kupitia makampuni haya binafsi yanayoweza ku-opparate kwa ngazi ya wilaya, mkoa, kanda na hata ngazi ya kitaifa kutegemeana na uwezo na mtaji wa kampuni husika.

6. TANESCO itapunguziwa mzigo wa kuhudumia nchi nzima na hivyo inaweza kujiendesha kwa faida tofauti na ilivyo sasa.

7. Serikalini itaondokana na mzigo wa kuibeba TANESCO na kuokoa fedha nyingi za umma zinazoelekezwa katika kusaidia TANESCO.

8.TANESCO inaweza kutumia miundombinu yake kibiashara kwa makampuni mapya yanayoweza kutumia miundombinu ya TANESCO kwa malipo ya kibiashara.

9.Serikali inaweza pia kufanya biashara ya kuuza kwa makampuni binafsi ya kusambaza umeme kutoka katika vyanzo vyake vya kuzalisha umeme mfano Stieglers Gorge ikikamilika.

Tofauti na hapo, ni bora lile wazo la kuivunja TANESCO na kuwa na makampuni matatu ya kuzalisha,kusambaza na kuuza umeme likafanyiwa kazi kuondoa hii monopoly ya TANESCO katika hii biashara ya kuzalisha na kusambaza umeme.
biashara ya umeme ni huria tayari, maana watu wa solar na wauza generator ni watu huru huria,

ila umeme huu wa diazaini ya tanesco ni ngumu kwa watu kujitoa kuinvest, kwanza ni pesa nyingi sana, hebu pata picha minguzo na minyaya ambayo tanesco inasambaz, maintanance wafanyakazi,

gharama zake kuna muda zinazidi mapato ama zinakaribi mapato,
kwa hali ya kawaida, kampuni binafsi huwekekeza sekta ama eneo ambalo kuna low calculated risk na gharama za uendeshani ndogo. we unafikiri wanahisa wa kampuni binafsi watakuwa tayari mipesa yao isambaze umeme vijijini, ilhali soko la mjini ni kubwa na linaingiza pesa za kutosha.
biashara ya umeme wa maji kama tanesco ikifanywa na private huyo private ataimudu ikiwa tu, na yeye ni monopoly kama tanesco, na hata yangekuwelo mashirika private, mwisho wake yangeungana tu kuwa kampuni moja,
 
biashara ya umeme ni huria tayari, maana watu wa solar na wauza generator ni watu huru huria,

ila umeme huu wa diazaini ya tanesco ni ngumu kwa watu kujitoa kuinvest, kwanza ni pesa nyingi sana, hebu pata picha minguzo na minyaya ambayo tanesco inasambaz, maintanance wafanyakazi,

gharama zake kuna muda zinazidi mapato ama zinakaribi mapato,
kwa hali ya kawaida, kampuni binafsi huwekekeza sekta ama eneo ambalo kuna low calculated risk na gharama za uendeshani ndogo. we unafikiri wanahisa wa kampuni binafsi watakuwa tayari mipesa yao isambaze umeme vijijini, ilhali soko la mjini ni kubwa na linaingiza pesa za kutosha.
biashara ya umeme wa maji kama tanesco ikifanywa na private huyo private ataimudu ikiwa tu, na yeye ni monopoly kama tanesco, na hata yangekuwelo mashirika private, mwisho wake yangeungana tu kuwa kampuni moja,
Umeongea vyema sana, mpaka sasa biashara ya umeme ni huria, hamna anayekatazwa kuiendesha. Sema watu wanajua kusafirisha umeme kutoka Dar mpaka Bukoba ni sawa na kusafirisha mawimbi ya simu yanayotumia minara
 
Back
Top Bottom