Kwanini Barrick Gold hawataki tujue kuhusu sheria hii?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kwanza namshukuru Dr. Khamisi ambaye kupitia KLH News alinidokeza uwepo wa nyaraka hii. Barrick Gold ni kampuni iliyosajiliwa Canada. Na kimsingi shughuli zao wanazofanya kule Canada zinaongozwa na sheria za nchi hizo ambazo kwa upande wa madini ni mojawapo ya sheria ambazo zimekomaa zaidi na ni mfano kwa nchi nyingi zaidi.

Niliposoma Mkataba wa Buzwagi, jambo moja lilikuwa linanisumbua; kwanini inaonekana kana kwamba Mkataba unaweka mpaka mkubwa katika masuala ya fedha? Sikuweza kujua chanzo cha hisia hizo hadi nilipopata kuiona sheria hii ya madini ya Canada (ambayo ni sehemu ya Sheria yao ya Ardhi). Nilichogundua ni kuwa kwa mtazamo wa Barrick Gold, mkataba wa Buzwagi ni kinyume kabisa na sheria ya madini ya nyumbani kwao!

Utaona kuwa vipengele ambavyo tumevilalamikia hapa kwenye mkataba huo viko kinyume kabisa vipengele kama hivyo kwenye sheria ya madini ya Kanada. Ni wazi kuwa waliowakilisha Barrick kwenye mazungumzo na serikali yetu walikuwa wanaongozwa na "kwenda kinyume" na sheria ya Canada kwani sheria ya Canada inalenga kunufaisha jamii na nchi na pia kuhakikisha kuwa kampuni inanufaika.

Ni kweli kumbe unaweza kuwa na sheria ya win-win bila kufukuza wawekezaji.

TAFADHALI ipitie sheria hii hasa Kifungu cha 65-67 na ulinganishe na sheria yetu au mkataba wetu na Buzwagi. Tukisema tumeibiwa mchana, tunatumia lugha ya kiungwana, TUMELIZWA!

M. M.
 
Ni kwa sababu hawataki ukweli ujulikane wazi kuwa wanatuibia kupitia viongozi wetu wala rushwa na wezi kuanzia Kikwete hadi Mwanyika
 
Kuna umuhimu wa kuliangalia hili kwa sababu moja au nyingine sifikirii kama Canadian companies wanaruhusiwa kuvunja sheria ambazo hata Canada wanafuata, lakini hili linaweza kuwa ndio moja ya sababu kubwa kwa makampuni mawili au matatu ambayo yameibuka kwa kuogopa kushughulikiwa na serikali ya Canada. (Tanzania Royalty, Pangea etc.). Jinsi unavyozidi kusoma ndio unaona jinsi tulivyoingizwa mjini mchana kweupe.
 
Kwanza namshukuru Dr. Khamisi ambaye kupitia KLH News alinidokeza uwepo wa nyaraka hii. Barrick Gold ni kampuni iliyosajiliwa Canada. Na kimsingi shughuli zao wanazofanya kule Canada zinaongozwa na sheria za nchi hizo ambazo kwa upande wa madini ni mojawapo ya sheria ambazo zimekomaa zaidi na ni mfano kwa nchi nyingi zaidi.

Niliposoma Mkataba wa Buzwagi, jambo moja lilikuwa linanisumbua; kwanini inaonekana kana kwamba Mkataba unaweka mpaka mkubwa katika masuala ya fedha? Sikuweza kujua chanzo cha hisia hizo hadi nilipopata kuiona sheria hii ya madini ya Canada (ambayo ni sehemu ya Sheria yao ya Ardhi). Nilichogundua ni kuwa kwa mtazamo wa Barrick Gold, mkataba wa Buzwagi ni kinyume kabisa na sheria ya madini ya nyumbani kwao!

Utaona kuwa vipengele ambavyo tumevilalamikia hapa kwenye mkataba huo viko kinyume kabisa vipengele kama hivyo kwenye sheria ya madini ya Kanada. Ni wazi kuwa waliowakilisha Barrick kwenye mazungumzo na serikali yetu walikuwa wanaongozwa na "kwenda kinyume" na sheria ya Canada kwani sheria ya Canada inalenga kunufaisha jamii na nchi na pia kuhakikisha kuwa kampuni inanufaika.

Ni kweli kumbe unaweza kuwa na sheria ya win-win bila kufukuza wawekezaji.

TAFADHALI ipitie sheria hii hasa Kifungu cha 65-67 na ulinganishe na sheria yetu au mkataba wetu na Buzwagi. Tukisema tumeibiwa mchana, tunatumia lugha ya kiungwana, TUMELIZWA!

M. M.

Itakuwa vizuri kumuonyesha mkataba huo balozi wa Canada-Tanzania, na kupin point ni wapi katika mkataba huo Barrick wameenda kinyume na sheria za uchimbaji wa madini za Canada. Na ikiwezekana balozi aombwe kutumia wadhifa wake ili aondoe kasoro hiyo.
 
Ni kwa sababu hawataki ukweli ujulikane wazi kuwa wanatuibia kupitia viongozi wetu wala rushwa na wezi kuanzia Kikwete hadi Mwanyika

Kuna umuhimu wa kuliangalia hili kwa sababu moja au nyingine sifikirii kama Canadian companies wanaruhusiwa kuvunja sheria ambazo hata Canada wanafuata, lakini hili linaweza kuwa ndio moja ya sababu kubwa kwa makampuni mawili au matatu ambayo yameibuka kwa kuogopa kushughulikiwa na serikali ya Canada. (Tanzania Royalty, Pangea etc.). Jinsi unavyozidi kusoma ndio unaona jinsi tulivyoingizwa mjini mchana kweupe.

Itakuwa vizuri kumuonyesha mkataba huo balozi wa Canada-Tanzania, na kupin point ni wapi katika mkataba huo Barrick wameenda kinyume na sheria za uchimbaji wa madini za Canada. Na ikiwezekana balozi aombwe kutumia wadhifa wake ili aondoe kasoro hiyo.

Nimewa quote tu kukumbushia ikae..
Kweli na hawa Barrick tumetoka mbali.
 
Kimsingi na kisheria pale makubaliano ya kimkataba baina ya pande mbili toka mamlaka tofauti za kisheria yaani 'different jurisdictions' yanapoingiwa, pande hizo husika huchagua sheria ya mahali itakayoongoza hayo makubaliano. Sasa katika mikataba ya madini kati ya Barrick na serikali yetu, ni sheria zetu za kodi, uwekezaji, madini , makapuni n.k ndio zinaendesha haya masuala na si za Canada.

Isipokuwa katika baadhi ya masuala mathalani, usuluhishi wa migogoro tumeridhia mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji (ICSD) ishughulikie.

Hoja ya kutafuta makosa katika masuala ya uwekezaji kwamba ati Barrick wanakiuka sheria za nchi yao hazina mashiko kimantiki na kisheria, badala yake ni vyema tukatazama sheria zetu zenye dosari nyingi katika masuala ya uwekezaji ambapo ndio kiini cha matatizo. Sheria ya Canada haitatusaidia hatakama ni nzuri kiasi gani haitetei maslahi yetu kisheria ila ya Tanzania yatufanya tunaumia.

Baada ya kujitathimini tulipokosea basi tuchukue hatua.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom