Kwanini baba wa taifa hakuwahi kumpa kinana uongozi wa chama??

Kinana anawanyima watu usingizi kudadadadadadadek.garaza hao kinana tupo nyuma yako.
 
Pale mwisho umesema hana uzalendo wa nji hii,kwa hiyo nyie kaskazini ndio wazalendo?kumbuka mwalim aliwapa za uso kuwa hamfai kushika uongozi wa juu wa nji hii
 
Sema wewe! Alistaafu lini sasa? Kwanza umri wake ni mdogo kuliko wa akina Malecela na Msekwa. Je kama alistaafu kabla ya muda wake wa kustaafu kwa sababu maalum huamini pia? Kama unaamini hilo basi tafuta kwa nini alilazimika kustaafu Jeshini kabla ya muda wake wa kustaafu ndiyo utuambie, labda itasaidia kujua kwa nini asifae kuwa Kiongozi CCM. Mwaka 1952 wote tunajua alikuwa bado hata Jeshi halijui kwa hiyo siyo kigezo cha kutupia janvini hapa.

Unajua ufisadi sasa hivi ni sifa inayotumika kupigana vita vya kusaka uongozi tu. Kwa mfano sasa hivi Lowassa anazunguka nchi nzima akishawishi raia kuwa yeye atakuwa Rais mzuri sana 2015 Anazindua na kuchangia makanisa lukuki kwa feza yake ya nyumbani kwake. Lakini Lowassa huyo huyo ALILAZIMIKA kujiuzulu uWaziri Mkuu katika Serikali hii hii ya Kikwete, kisa ufisadi wa Richmond. Lowassa huyo huyo ndiyo alikwenda Korea kununua mvua ya kutungua kwa bunduki. Wakati wa Lowassa bwawa la Mtera kila siku lilijaa matope, lakini sijasikia mpaka leo catapillar zikienda kutoa matope hayo, na Mtera leo inazalisha umeme. Lakini juzi nimekutana na gari la Mmang'ati mmoja (Masai wengi hawajanunua) limeandikwa (Lowassa-Rais 2012). Mbona huyu hammzuii, mnamshangilia bila kumwita fisadi wakati vituko vyote hapo juu ni ufisadi? Unasema CCM ni fisadi kwa sababu CHADEMA wanataka madaraka, siyo? Wao siyo mafisadi?

Yesu Mwana wa Mungu aliwakuta watu wanataka kumpiga mawe mwanamke wakimtuhumu mzinifu, akawambia (kama) hivi: "Awaye yeyote asiye na zinaa na mwanamke huyu basi awe wa kwanza kutupa jiwe lake." Watu wale walijua ni waongo lakini kwa sababu walikuwa bado wakimjua Mungu na kumwogopa wote walisambaa na kumwacha mwanamke yule aende zake. Tz hata Mungu hatumwogopi! Generali Defao amekuja kutumbuiza tukamsingizia zinaa zisizomhusu wala na mpaka leo ameacha kutumbuiza tena.

Hivyo hatushangaia, tuchafueni tu lakini kwa mapesa ya ufisadi tuliyokwisha kugawana hamtatuweza kamwe, hata Kinana pia. Tz hii, Kinana akiteuliwa na CCM kugombea uRais 2015 si utapiga kura za ndiyo tu?
 
Kwa nini humsemi Lowassa ambaye alikwenda kuchukua fomu za kugombea uRais 1995 Nyerere akamfukuza na leo anapiga jalamba waziwazi hata baada ya kujiuzulu uWaziri Mkuu kwa sababu ya fisadi la Richmond?

Acheni kuleta unafiki kwenye jamvi, pigia wote machapuo au filisi mafisadi wote, hapo tutakuelewa!
 
hoja dhaifu mno kwa hyo haitaji kujadili. Viongozi kwa nyadhifa zote za chama walikuwepo, sasa ulitaka kinana awekwe kwenye ngazi ipi ya uongozi?????? Na zaidi mwenyewe kinana amenukiliwa na kukaliliwa kwa vyombo vya habari ya kuwa anajivunia kwa kufanya kazi na maraisi wa awamu zote nne hasa ndani ya chama na serikalini pia, sasa mpaka hapa uoni ya kuwa hoja yako ni dhaifu!!!!!!!!!!!!!!!!!!. "think big, kila uletapo hoja"
 
me naona unajadili ujinga tu, sasa Uraia wa kinana na CCM wapi na wapi bwana, Kinana ni Raia wa Tanzania na hata kama asingekuwa Raia wa Tanzani basi asingeweza kuwa katika Jeshi la Tanzania na hata kama angezaliwa Somalia akaja kuishi Tanzania na kupata Uraia wa TZ hakuna ubaya kuwa kiongozi, sio kwa sababu hakuchaguliwa na Nyerere basi ndo awe hafai sasa si muda wake hujafika kwani wangapi Nyerere hajawachagua na leo viongozi?? Kwan lazima kiongozi achaguliwe na nyerere?? Yeye Nyerere kwani Nchi ya baba yake au ya kwake??? Hii Nchi ya Watanzania bwana na wala haiitwi Nchi ya Wananyerere kwa hiyo stop kutpa fikra mgando, na Uteuzi wa Chama chochote cha siasa watajua wenyewe kama wewe Chadema ya CCM ya nini??? Acheni kuzingua bwana me sioni Tatizo la Kinana mwacheni mwaka wake Nyota imeng'aa acha ale Bata.
Kila mtu na msimu wake, yuko wapi Mrema mbona aliwika sana kipindi cha Mkapa na upinzani mkubwa lakn sasa hivi hana upinzani, so mambo yanabadilika hata Chadema sasa hivi ndo chama chenye Upinzani sana lakin baadae kitakuja chama kingine wala usijal ni mabadiliko tu. tulia kama moja

brasy coco

Nafikiri wewe hujui unachoongea wala huijui CCM vizuri. Kama wewe ni mpenzi/mwanachama/mkereketwa/mfurukutwa wa CCM basi mwulize Hussein Bashe alipotaka kugombea Ubunge mwaka 2010 atakwambia jinsi CCM walivyomzima kwa kumwita ni MSOMALI. Labda kwa kukumbusha ni kwamba Bashe alizimwa kwa issue ya URAI wake!

Kuna wengi wengine ambao pia walizimwa kwa mtindo huohuo akiwemo gwiji la Habari Tanzania Jenerali Ulimwengu. Kwa hiyo Kinana anaweza kuwa kweli aliwahi kuwa Jeshini na sehemu zingine za kikazi Tanzania hiyo bado haitoshi kumthibitisha kuwa ni RAIA HALISI wa Tanzania. Kuna siku watu watambana kuhusu Kinana kuhusu Uraia wake na ndipo itakapokuwa aibu na fedheha kwa CCM na Serikali yake.

Ipo siku.CCM wasifikiri Kinana ni Mtaji wa kuwavusha uchaguzi wa 2015. Nina hakika mpaka 2015 jina la Kinana litabadilika na atakuwa akiitwa KINENA!!!
 
Baada ya uteuzi wa Sekretariati mpya ya Chama Twawala-CCM na Kinana kuibuka kama Katibu Mkuu mpya wa CCM kwa mara ya kwanza watu wamesifia sana uteuzi huo kutoka kila kona ya nchi hii hasa wanachama wa Chama Cha Mafisadi-CCM.

Mimi nataka tu niwakumbushe hawa wanachama wachovu wa CCM kwamba Kinana alikuwepo tangu enzi za Baba wa Taifa lakini hakuwahi kupewa wadhifa wowote ndani ya TANU wala CCM. Hapa ndipo mahali pakuanzia kutafakari uteuzi huu wa Kinana. Abdurhaman Kinana alikuwa mwanajeshi wa cheo cha Kanali mpaka alipostahafu mwaka 1972 baada ya kuitumikia JWTZ kwa miaka 20 tu. Baada ya hapo hakusikika tena kwenye medani za siasa wala za Jeshi. Sikumbuki hata kamaalishiriki vita vya Nduli Iddi Amini miaka ya 1978/79 sina hakika!!!

Bila shaka Mwalimu(Baba) wa Taifa hili alikuwa akimjua Kinana vizuri sana kuanzia URAIA wake,UZALENDO wake kwa Tanzania na WELEDI wake katika siasa za Tanzania. Nina hakika Mwalimu alikuwa anajua vizuri sana kuhusu URAIA wa Kinana ambaye hapana shaka huyu jamaa ana ASILI ya SOMALIA. Hili mwalimu alilijua na ndiyo maana hakuwahi kumpa nafasi yoyote kubwa katika nyanja za kisiasa maana KINANA'S CITIZENSHIP IS QUESITIONABLE!!!!

Sasa napenda kuwauliza Wana CCM na mwenyekiti wao Kikwete huyu Kinana amepata wapi uzalendo wa kuwa Katibu Mkuu wa Chama chenu cha Mafisadi???Je, wanaweza kututhibitishia pasipo shaka kuwa Kinana ni Raia halisi wa Tanzania? Je, katika vita vya kumwoa Nduli Idd Amini, huyu Kinana alikuwa wapi maana hata kama alistahafu Jeshi mwaka 1972 nijuavyo sheria za Jeshi mahali popote duniani vita vikiripuka hata wanajeshi waliostahafu huitwa kuungana na wenzao ili kuitetea nchi yao. Now CCM tell us Kinana's role in the Tanzania/Uganda war!

Nje ya hapo Kinana hafai kuwa Katibu Mkuu wa Chama chenu cha Mafusadi maana hana Uzalendo wa nji hii.

Nawasilisha.

Mkuu,
Ni vizuri sana kujua historia sahihi ya mhusika kabla ya kumjadili.

Pili, mambo ya kuambiwa, changanya na akili yako ili kujiridhisha. Hivi kwa Kinana huyo unayemwona unaamini kweli alistaafu jeshi mwaka 1972 baada ya kulitumiakia miaka 20? Ina maana aliingia jeshi mwaka 1952? Kama hilo ni kweli basi aliingia jeshi akiwa na umri wa mwaka mmoja.

Kuanzia miaka ya 70 mpaka Nyerere anastaafu, Kinana alikuwa political commissar jeshini. Hao enzi hizo wlaikuwa kama ni walimu wa siasa jeshini. Hizo zilikuwa ni nafasi za chama cha TANU ndani ya jeshi.

Nyerere amestaafu Kinana akiwa kijana kabisa chini ya miaka 35.

Mijadala inakuwa mizuri pale tunapojadili ukweli na sio habari ambayo sio sahihi. Sisi kwenye technology tunasema garbage in garbage out. Kwasababu premise uliyoanza nayo kwenye mjadala huu sio sahii ina maana hata majibu yake au conclusion yake itakuwa sio sahihi.
 
Mkuu,
Ni vizuri sana kujua historia sahihi ya mhusika kabla ya kumjadili.

Pili, mambo ya kuambiwa, changanya na akili yako ili kujiridhisha. Hivi kwa Kinana huyo unayemwona unaamini kweli alistaafu jeshi mwaka 1972 baada ya kulitumiakia miaka 20? Ina maana aliingia jeshi mwaka 1952? Kama hilo ni kweli basi aliingia jeshi akiwa na umri wa mwaka mmoja.

Kuanzia miaka ya 70 mpaka Nyerere anastaafu, Kinana alikuwa political commissar jeshini. Hao enzi hizo wlaikuwa kama ni walimu wa siasa jeshini. Hizo zilikuwa ni nafasi za chama cha TANU ndani ya jeshi.

Nyerere amestaafu Kinana akiwa kijana kabisa chini ya miaka 35.

Mijadala inakuwa mizuri pale tunapojadili ukweli na sio habari ambayo sio sahihi. Sisi kwenye technology tunasema garbage in garbage out. Kwasababu premise uliyoanza nayo kwenye mjadala huu sio sahii ina maana hata majibu yake au conclusion yake itakuwa sio sahihi.

Mtanzania,

Uko sahihi kwa hili. Hata hivyo katika kuchanganya akili zangu na za Absolom Kibanda nilijaribu kutafuta habari za Kinena kwenye search engine kama alizaliwa mwaka gani,alisoma wapi na aliajiriwa lini jeshini mpaka kustahafu kwake sikupata!!!

Kama wewe una taarifa sahihi za Kinena ziweke hadharani ili tujue huyu jamaa ni nani hasa katika siasa za Tanzania na kwanini Baba wa Taifa hakuwahi kumpa madaraka makubwa ya kuongoza TANU na baadaye CCM! Watanzania wanahaki ya kujua undani wa Kinena ili kujenga imani naye au kumtosa!
 
Mtanzania,

Uko sahihi kwa hili. Hata hivyo katika kuchanganya akili zangu na za Absolom Kibanda nilijaribu kutafuta habari za Kinena kwenye search engine kama alizaliwa mwaka gani,alisoma wapi na aliajiriwa lini jeshini mpaka kustahafu kwake sikupata!!!

Kama wewe una taarifa sahihi za Kinena ziweke hadharani ili tujue huyu jamaa ni nani hasa katika siasa za Tanzania na kwanini Baba wa Taifa hakuwahi kumpa madaraka makubwa ya kuongoza TANU na baadaye CCM! Watanzania wanahaki ya kujua undani wa Kinena ili kujenga imani naye au kumtosa!

Mzalendo2015,
Kinana kazaliwa Arusha mwaka 1951 na kasomea Arusha. Baadaye alisoma Yugoslovakia, nafikiri vyuo kama vile walivyoenda kusoma akina Sokoine Bulgaria. Pia ninavyojua mimi ana masters ya Havard ya management and public administration.

Kuwa mwalimu wa siasa jeshini alianza miaka ya 70. Sina uhakika kamili lakini ni around hiyo 1972 na aliendelea mpaka mwaka 1985.

Kwahiyo wakati wa Nyerere yeye alikuwa kijana tu akiwa ameajiriwa jeshini. Hivi kweli ukimwangalia Kinana ana miaka zaidi ya 80? Maana kutumikia jeshi miaka 20 na kuacha jeshi mwaka 1972 ina maana sasa angelikuwa na miaka zaidi ya 80.

Mambo yake yanafanana sana na ya jenerali Ulimwengu kuhusu uraia. Huko nyuma wote walijua ni Watanzania lakini wakati ule wa Mrema ndio wengi wakajua kwamba huenda hawakutimiza sharti la kuukana uraia mwingine. Kinana alikuwa mjanja na akaamua kutokugombea ubunge tena wakati anaweka mambo yake safi. Nafikiri sasa makaratasi yake yako in order sawa tu na akina Ulimwengu.

Nimetumia nafikiri nyingi kwasababu sina uhakika wa asilimia 100. Ila Kinana hakuacha jeshi mwaka 1972; huenda mwaka huo ndio alianza kazi jeshini akiwa na miaka 21.
 
Back
Top Bottom