Kwanini baadhi yetu hatuamini juu ya uwezekano wa Tanzania ya viwanda katika awamu hii ya tano

Massenberg

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
1,173
1,370
Habari za weekend,
Serikali ya awamu ya tano imeingia kwa gear ya kwamba Tanzania ya JPM inakuja kuwa ya viwanda. Ingawa ni vyema kuwa na malengo katika uongozi lakini hii injili ya viwanda ina matatizo.
Tanzania ya JPM sana sana itakuwa ya miaka kumi; hakuna duniani na wala haijawahi kuwepo nchi iliyobadili mfumo wake wa uchumi katika kipindi kifupi namna hiyo. Kuitoa Tanzania hapa ilipo na kuifikisha kwenye uchumi wa viwanda utahitaji miaka si chini ya thelathini.
Nisichukue sana muda lakini hapa chini ni link ya makala inayozungumzia Ethiopia katika safari yake kuelekea kuwa kitovu cha viwanda barani Afrika. Ukifanikiwa kuisoma naomba ulinganishe na haya tunayoambiwa kuhusu viwanda kisha busara zako zikuongoze.

Ethiopia is on track to become Africa’s industrial powerhouse
 
Mimi sihitaji kusoma ya Ethiopia, naamini tunataka kujenga viwanda kama Abunuasi alivyokuwa akijenga nyumba angani. Inaniuma kuona serikali inakuwa hivyo. Kwa nchi ambayo zaidi ya 80% kwa kipindi chote wamekuwa wakitegemea Kilimo mara ghafla unakuja na gear ya viwanda ah uko serious? Wakati unahaweka ktk viwanda kila senti unayoipata huyu mkulima awe anaishi vipi. Ni ile dhana ya aliisha kuwa maskini basi! Watoto wao wasio na kazi nao basi! Ni kweli viongozi wetu hawajui kuwa kujenga viwanda ni process ambayo inachukua muda mrefu na kuwekeza sana? Nimekata tamaa!
 
Mambo yetu mengi ni ya njia za mkato ndiyo maana 2011 maelfu ya Watanzania waliungana na viongozi lukuki wa nchi kwenda Loliondo kunywa mimaji michafu wakiamini ni dawa ya magonjwa yao.
Pengine viongozi wetu wanadhani uchumi wa viwanda ni kuwa na majengo yenye mashine ndani yake tu.
 
Dhana hii ya Tanzania ya viwanda hata mimi naona kama siielewi lakini nimejipa muda wa kutokosoa kwanza. Hebu tuvute subira tuone huko tunaenda na njia gani. Maana sasa hivi ukihoji utajibiwa bado safu inapangwa. Nimesikia kuna kiwanda cha sukari kitajengwa Kigoma hivi karibuni, najiuliza ni kwa miwa ipi?
 
Habari za weekend,
Serikali ya awamu ya tano imeingia kwa gear ya kwamba Tanzania ya JPM inakuja kuwa ya viwanda. Ingawa ni vyema kuwa na malengo katika uongozi lakini hii injili ya viwanda ina matatizo.
Tanzania ya JPM sana sana itakuwa ya miaka kumi; hakuna duniani na wala haijawahi kuwepo nchi iliyobadili mfumo wake wa uchumi katika kipindi kifupi namna hiyo. Kuitoa Tanzania hapa ilipo na kuifikisha kwenye uchumi wa viwanda utahitaji miaka si chini ya thelathini.
Nisichukue sana muda lakini hapa chini ni link ya makala inayozungumzia Ethiopia katika safari yake kuelekea kuwa kitovu cha viwanda barani Afrika. Ukifanikiwa kuisoma naomba ulinganishe na haya tunayoambiwa kuhusu viwanda kisha busara zako zikuongoze.

Ethiopia is on track to become Africa’s industrial powerhouse
Huo Utafiti Umefanyika wapi?kuna nchi zimechukua miaka mia,zingine thelathini kutegemeana na Resources za Nchi husika na uwezo wa Utawala .Hiyo Ndugu ni negative thinking na ndio tatizo la waafrika wengi."kutojiamini".kujiona huwezi kitu,unyonge wa mawazo.Na kukatishana Tamaa.Tubadilike
 
Dhana hii ya Tanzania ya viwanda hata mimi naona kama siielewi lakini nimejipa muda wa kutokosoa kwanza. Hebu tuvute subira tuone huko tunaenda na njia gani. Maana sasa hivi ukihoji utajibiwa bado safu inapangwa. Nimesikia kuna kiwanda cha sukari kitajengwa Kigoma hivi karibuni, najiuliza ni kwa miwa ipi?

Kuna suala la nchi kuwa tayari kwa mfumo fulani mpya. Uchumi wa viwanda unahitaji watu wenye elimu na ujuzi wa kuendesha viwanda vya kisasa na hii inajumuisha ufundi na management, inahitajika nishati ya uhakika na ya kutosha, inahitajika miundombinu ya barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege, vinahitajika vyanzo thabiti vya malighafi kutoka ndani na nje ya nchi, yanahitajika masoko ya uhakika ya kuuza bidhaa, na pia uwezo wa kupambana na nchi zingine kama Kenya na Afrika Kusini kwenye vita ya viwanda.
Je, lini tumejiandaa kwenye maeneo yote haya?
 
Habari za weekend,
Serikali ya awamu ya tano imeingia kwa gear ya kwamba Tanzania ya JPM inakuja kuwa ya viwanda. Ingawa ni vyema kuwa na malengo katika uongozi lakini hii injili ya viwanda ina matatizo.
Tanzania ya JPM sana sana itakuwa ya miaka kumi; hakuna duniani na wala haijawahi kuwepo nchi iliyobadili mfumo wake wa uchumi katika kipindi kifupi namna hiyo. Kuitoa Tanzania hapa ilipo na kuifikisha kwenye uchumi wa viwanda utahitaji miaka si chini ya thelathini.
Nisichukue sana muda lakini hapa chini ni link ya makala inayozungumzia Ethiopia katika safari yake kuelekea kuwa kitovu cha viwanda barani Afrika. Ukifanikiwa kuisoma naomba ulinganishe na haya tunayoambiwa kuhusu viwanda kisha busara zako zikuongoze.

Ethiopia is on track to become Africa’s industrial powerhouse
Mzee unachokiona serikali ya JPM imekosea ni kipi hapo. Kutangaza hiyo nia au kuitaja hiyo miaka kumi? Mi naamini mwanzo ni mgumu. As far serikali hii imeonyesha hiyo nia tunachotakiwa ni kuamini na kuiunga mkono hiyo nia kila MTU kwa nafasi yake.
Ni bora rais kaonyesha hiyo nia mapema maana kuchelewesha ni kuzidi kuchelewesha hayo maendeleo. Atafanya atakayoweza ndani ya miaka yake kumi atakaye mfuatia atayaendeleza.

Ukisoma vizuri hiyo article hata Ethiopia kuna MTU alianzisha wazo hilo aliyepo anaendeleza.

Point ya msingi ambayo naiona hapo ni kwamba ni kweli ni vigumu kufanya maendeleo ya viwanda tunayoyataka kwa miaka kumi. Ila sio kulauumu serikali ambayo imelianzisha wazo zuri kama hilo, zaidi zaidi tuishauri ili iweke mfumo imara ambao utambana rais yeyote atakayeingia madarakani ili aiendeleza hatimaye tufikia lengo kuu la kuwa nchi ya viwanda

Maneno huumba, imani inaweZa kuhanisha mawe hata milima.

Asante JPM na serikali yako kwa kutuonyesha kuwa Tanzania ya viwanda inawezekana. Tuna kila aina ya resource ya kutufanya tuweze kufika huko. Ethiopia na ukame wote ule wameweza why not Tanzania? Ni uongozi wenye maono ya mbali na kuamini ndio unaohitajika. JPM kaliona hilo, let's us support him kwa faida ya Tanzania ya sasa na ijayo

Tusilaumu, kupinga au kuhoji kila kitu kinachofanywa serikali. Tushauri pia
 
Huo Utafiti Umefanyika wapi?kuna nchi zimechukua miaka mia,zingine thelathini kutegemeana na Resources za Nchi husika na uwezo wa Utawala .Hiyo Ndugu ni negative thinking na ndio tatizo la waafrika wengi."kutojiamini".kujiona huwezi kitu,unyonge wa mawazo.Na kukatishana Tamaa.Tubadilike
Umaskini wa mawazo ni umaskini mbaya kuliko wote - Marehemu Julius Kambarage Nyerere.
 
Nchi ngapi duniani zina Helium,gas,Tanzanite,Maziwa,Mito kila Mahali,Hazijaonja Vita ,Geographyical position nzuri kwa biashara na vinginevyo ambavyo Mwenyezi Mungu Ametujaalia?
 
Viwanda sio kauli ya mtu mmoja, Viongozi ni walewale kutoka ndani ya chama kilekile na hata matendo yao ya kiutawala hayana tofauti kubwa. Viwanda haviletwi na Chama kushoka Dola.
 
Nchi ngapi duniani zina Helium,gas,Tanzanite,Maziwa,Mito kila Mahali,Hazijaonja Vita ,Geographyical position nzuri kwa biashara na vinginevyo ambavyo Mwenyezi Mungu Ametujaalia?

Umeisoma makala ya Ethiopia lakini? Kuwa na vitu vyote hivyo kunatufanyaje kuwa na uchumi wa viwanda? Haya mambo si ya kutamka tu majukwaani, yanahitaji mikakati ya kitaalamu na upeo wa hali ya juu ili kufanya maandalizi ya kuwa uchumi wa viwanda.
 
Kuna suala la nchi kuwa tayari kwa mfumo fulani mpya. Uchumi wa viwanda unahitaji watu wenye elimu na ujuzi wa kuendesha viwanda vya kisasa na hii inajumuisha ufundi na management, inahitajika nishati ya uhakika na ya kutosha, inahitajika miundombinu ya barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege, vinahitajika vyanzo thabiti vya malighafi kutoka ndani na nje ya nchi, yanahitajika masoko ya uhakika ya kuuza bidhaa, na pia uwezo wa kupambana na nchi zingine kama Kenya na Afrika Kusini kwenye vita ya viwanda.
Je, lini tumejiandaa kwenye maeneo yote haya?
Ni kweli unachokisema. Mimi nadhani serikali hii kama kweli ina nia ya kuifanya nchi yetu kuwa ya viwanda, iandae mfumo ambao utafanikisha malengo. Si kwamba viongozi waliopita hawakuwa na maono, la hasha, tatizo ni utekelezaji wa sera zao. Imefanikiwa je sera ya kilimo kwanza? Hivi karibuni Mh. Mkapa amekiri makosa katika sera ya ubinafsishaji.
 
Mzee unachokiona serikali ya JPM imekosea ni kipi hapo. Kutangaza hiyo nia au kuitaja hiyo miaka kumi? Mi naamini mwanzo ni mgumu. As far serikali hii imeonyesha hiyo nia tunachotakiwa ni kuamini na kuiunga mkono hiyo nia kila MTU kwa nafasi yake.
Ni bora rais kaonyesha hiyo nia mapema maana kuchelewesha ni kuzidi kuchelewesha hayo maendeleo. Atafanya atakayoweza ndani ya miaka yake kumi atakaye mfuatia atayaendeleza.

Ukisoma vizuri hiyo article hata Ethiopia kuna MTU alianzisha wazo hilo aliyepo anaendeleza.

Point ya msingi ambayo naiona hapo ni kwamba ni kweli ni vigumu kufanya maendeleo ya viwanda tunayoyataka kwa miaka kumi. Ila sio kulauumu serikali ambayo imelianzisha wazo zuri kama hilo, zaidi zaidi tuishauri ili iweke mfumo imara ambao utambana rais yeyote atakayeingia madarakani ili aiendeleza hatimaye tufikia lengo kuu la kuwa nchi ya viwanda

Maneno huumba, imani inaweZa kuhanisha mawe hata milima.

Asante JPM na serikali yako kwa kutuonyesha kuwa Tanzania ya viwanda inawezekana. Tuna kila aina ya resource ya kutufanya tuweze kufika huko. Ethiopia na ukame wote ule wameweza why not Tanzania? Ni uongozi wenye maono ya mbali na kuamini ndio unaohitajika. JPM kaliona hilo, let's us support him kwa faida ya Tanzania ya sasa na ijayo

Tusilaumu, kupinga au kuhoji kila kitu kinachofanywa serikali. Tushauri pia
Tatizo la nchi hii kila kiongozi anakuja na maono yake hivyo hatuwezi kufika popote. Jambo la msingi ulilosema ni kuweka mfumo ambao utawabana viongozi kutokutuyumbisha. Lakini mimi katika serikali hii sijaona sera itakayotufikisha kuwa nchi ya viwanda zaidi ya nadharia zinazotoka mdomoni.
 
Back
Top Bottom