ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 19,553
- 44,719
Jibu la Biblia
Jitihada za wanadamu za kuleta amani hazijawahi kufanikiwa na zitaendelea kutofanikiwa kwa sababu kadhaa:
“Njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake.” (Yeremia 10:23) Wanadamu hawakuumbwa wakiwa na uwezo na pia haki ya kujiongoza, hivyo hawatafanikiwa kupata amani ya kudumu.
“Msiwategemee viongozi wa kibinadamu, hakuna mwanadamu anayeweza kukuokoa. Wanapokufa, wanarudi mavumbini; siku hiyo mipango yao yote inakwisha.” (Zaburi 146:3, 4, Good News Translation) Viongozi wa serikali, hata wale walio na nia nzuri kabisa, hawawezi kutokeza suluhisho la kudumu ili kuondoa chanzo kikuu cha vita.
“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa . . . wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.” (2 Timotheo 3:1-4) Tunaishi katika “siku za mwisho” za ulimwengu huu mwovu, wakati ambapo mitazamo ya watu inafanya iwe vigumu kupata amani.
“Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ibilisi, ambaye ni adui ya Mungu, ametupwa katika ujirani wa dunia na anawachochea watu wawe na roho kama yake ya ukatili. Mradi anaendelea kuwa “mtawala wa ulimwengu huu,” hatuwezi kamwe kuishi kwa amani.—Yohana 12:31.
View attachment 2140573
Jitihada za wanadamu za kuleta amani hazijawahi kufanikiwa na zitaendelea kutofanikiwa kwa sababu kadhaa:
“Njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake.” (Yeremia 10:23) Wanadamu hawakuumbwa wakiwa na uwezo na pia haki ya kujiongoza, hivyo hawatafanikiwa kupata amani ya kudumu.
“Msiwategemee viongozi wa kibinadamu, hakuna mwanadamu anayeweza kukuokoa. Wanapokufa, wanarudi mavumbini; siku hiyo mipango yao yote inakwisha.” (Zaburi 146:3, 4, Good News Translation) Viongozi wa serikali, hata wale walio na nia nzuri kabisa, hawawezi kutokeza suluhisho la kudumu ili kuondoa chanzo kikuu cha vita.
“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa . . . wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.” (2 Timotheo 3:1-4) Tunaishi katika “siku za mwisho” za ulimwengu huu mwovu, wakati ambapo mitazamo ya watu inafanya iwe vigumu kupata amani.
“Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ibilisi, ambaye ni adui ya Mungu, ametupwa katika ujirani wa dunia na anawachochea watu wawe na roho kama yake ya ukatili. Mradi anaendelea kuwa “mtawala wa ulimwengu huu,” hatuwezi kamwe kuishi kwa amani.—Yohana 12:31.
View attachment 2140573