Kwanini ajira za muda mfupi za kusimamia Uchaguzi kipaumbele wanapewa walimu waliojiriwa?

Bibi shamba

Member
Aug 31, 2020
44
73
Jana tukiwa kwenye foleni ya kupeleka maombi ya kusimamia Uchaguzi Mkuu alisikika mwalim mmoja alisema "Hawa wanajisumbua tu kwanza kisheria mahali popote anapoomba mwalimu wengine wote wanawekwa pembeni anapewa mtumishi kwanza"

Sasa kama kigezo ni ualimu huku nje tuna diploma na degree zaidi ya 50,000 ambazo ni jobless, kwanini Serikali isinge-forcus kuwapa nafasi hawa ambao hawana kazi badala yake inawap watu ambao mwisho wa mwezi wana uhakika wa chochote
 
Aah mwenye nacho ataongezewa, halafu si watu wanalalamikaga walimu maslahi kidogo, labda ndo muda wao wa kuongeza maslahi.
 
Pole mwenye nacho huongezewa pia hutumiwa waalimu vile Ni wazoefu na rahisi kusimamia na ni waelewa wa taratibu tofauti na kuchukua wa mtaani
 
Pole mwenye nacho huongezewa pia hutumiwa waalimu vile Ni wazoefu na rahisi kusimamia na ni waelewa wa taratibu tofauti na kuchukua wa mtaani
Kuna semina ujue afu mwalim wa mtaan na mwalim alieajiliwa tofauti yao ni mmoja ana mshahara na mwingine hana ila wote n waalim
 
Ulikua unapeleka Halmashauri gani Dada??

Hivi Kazi Si Ni ya Siku Mbili !?

JamiiForums1395832429.jpg
 
Jana tukiwa kwenye folen ya kupeleka maombi ya kusimamia uchaguzi mkuu alisikika mwalim mmoja alisema "Hawa wanajisumbua tu kwanza kisheria mahali popote anapoomba mwalimu wengine wote wanawekwa pembeni anapewa mtumishi kwanza"

Sasa kama kigezo ni ualim uku nje tuna diploma na degree zaidi ya 50,000 ambazo ni jobless, kwanini serikali isinge-forcus kuwapa nafasi hawa ambao hawana kazi badala yake inawap watu ambao mwisho wa mwezi wana uhakika wa chochote
ndiyo rushwa yao kutokana na level ya ulewa wao, huoni wanapewa kusimamia uchaguzi na kupewa kanga za TANU?

waalimu ni tabaka hovyo sana,japo siwote, waalimu walikuwa kabla ya 2005 ila wle wa mwendokasi hamna kitu
 
Ulikua unapeleka Halmashauri gani Dada ??
Hivi Kazi Si Ni ya Siku Mbili !?View attachment 1579099
Yaan pale palikua na watu ambao ukiwaangalia adi huruma yupo mmoja kaja na ndala imekatika elim yake degree ya ualim yaan ukimuangalia adi huruma hela tu ya kuprintia cv alikua hana yaan kuna watu io kazi n ya siku mbili lakini kwao n Kama Yesu kaja kuwakomboa yaan watu wamepigika uku nje huwezi jua io hela kwake itasolve nini.
 
Kuna semina ujue afu mwalim wa mtaan na mwalim alieajiliwa tofauti yao ni mmoja ana mshahara na mwingine hana ila wote n waalim
Hapo kuna mwalimu mwenye cheti tu na mwalimu mwenye cheti + anapractise hio fani tayari hapo ni watu tofauti hawawezi kua sawa
 
Hizo ni kazi zao muda mrefu serikali huwa haiwasahau kwenye kazi za muda mfupi kama hizo
Mwaka 2012 tulikuwa na waalimu kibao kwenye sensa,hawangalii elimu,pia kama huna connection sahau labda uwe na bahati ya mtende.....hata mtu wa la saba anaweza pata wewe wa degree 4 ukakosa.
 
Back
Top Bottom