Kwanini 99% ya wale ‘ Wanaomfolo ‘ Mbabe wa Waziri Kangi Lugola kule ‘ Twitani ‘ wanatumia Majina Feki na ya ajabu ajabu sana?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,546
108,877
Kila ukiangalia idadi ya Watu ‘ wanaomfolo ‘ ni Kubwa sana na kila Siku inazidi tu Kuongezeka lakini cha Kushangaza kama si Kusikitisha pia ni kwamba karibia 99% ya wale ‘ Wanaomfolo ‘ wanatumia Majina ‘ Feki ‘ huku mengine yakiwa ni ya ajabu ajabu tupu.

Kwanini hawa ‘ wanaomfolo ‘ huyo Mbabe wa Waziri Kangi Lugola huko ‘ Twitani ‘ wanajichifa kwa kutotaka Majina yao halisi yatumike? Kwani kuna dhambi yoyote ile ‘ Kumfolo ‘ huyu Mbabe aliyeshindikana? Je, na Sisi wengine ‘ tunaomfolo ‘ kwa Majina yetu halisi kama Mimi Karemera Rwigyema Mazimpaka ( GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ) na tunachangia mno huko tuko salama au hatarini?

Na kama labda kutakuwa na Hatari yoyote ya Kutumia Majina yetu halisi katika ' Kumfolo ' huyo Mbabe wa Waziri Kangi Lugola huko ' Twitani ' basi nawaombeni wana JamiiForums mnichagulie na Mimi jina la ' ajabu ajabu ' kama wanayotumia huko Watu wengine ili nami nianze Kulitumia badala ya hili Jina langu halisi nililopewa na Wazazi wangu la Karemera Rwigyema Mazimpaka kutoka huko Kwetu Ututsini ' nchini Rwanda kwa Wanyarwanda.
 
Nimefatilia Sana account ha kigogo kwa umakini mkubwa na nimepata vitu baadhi ambavyo kigogo asipokuwa makini vitamuharibia au kumkamatisha,

Zipo account Zinazo msapoti kigogo kila post na kila ponit, Hizi awe makini nazo Sana, mfano hii ya son of kigogo huyu jamaa yupo karibu Sana ktk kila tweet jamaa atachangia tu, huenda wanajuana au jamaa anajiweka karibu ili kupata detail muhimu za kumpata kigogo

Wanawake wengi pia naona wanafuatlia tweet zake hapa ajiangalie Sana asije akakutana michezo ya urusi,

Ila kigogo Ni watu kadhaa ambao wapo committed haswa na wanajua Nini wanafanya, kuisambaratisha hii account hawataweza Maana Ni watu na si mtu na mawasiliano Yao hutumia email jinsi ya kupeana updates hivyo hata wadukue simu kamwe watafeli tu,

Zaidi kigogo Ni system ndani ya system( system within a system) Serikali inapigana Vita na watu usiowajua lakini wao wanaijua vzr serikali
 
Back
Top Bottom