Kwani tukiacha madirisha haya ya aluminiam na PVC, ndiyo kusema sisi hohehahe hatuna madirisha yetu mengine ya kisasa jameni?

Kwamba ukifungua ile space iliyofunguka ni ndogo kulingana na madirisha mbadala ?

Unaona hio point ni duni ?; Kwanza Faida ya Dirisha au umuhimu wa Dirisha ni nini ?

Ukijibu hayo utaona mleta uzi ana point ya maana sana...

Hayo madirisha unayoita mbadala ni yapi ambayo huhitaji hufunguka yote?

Kama hata hujui faida za dirisha ni ngumu kujadili kwa weledi.
 
Mleta Uzi una point sana aisee wewe ni peponi moja kwa moja now kwangu nimeweka grill tu nimetia na nyavu basi kwa sasa kwani kuna jirani yangu kayaweka anapata tabu sana fikiria umeiweka dirisha la 5×5 ukiweka hayo madrisha maana yake dirisha linakuwa 2.5

Hiyo futi 2.5 upana ambayo unaona haitoshi kuingiza hewa ndani unalinganisha na dirisha la aina gani?

Madirisha ya Aluminium ndo maana yamewezesha kuweka upana unaohitaji wewe, huwezi kulinganisha na yale ya nondo na wavu usiofunguka ambayo mara nyingi yalikuwa madogo kiasi.

Bado unajichanga tu ila zikitimia utaweka madirisha, acha wivu kwa huyo jirani kakutangulia tu…. jipe muda utamfikia au endelea kujitekenya.
 
Vitu viko on point mno. Mafundi sasa hapo uende akutengenezee hivyo atakutolea kitu cha ajabu mpaka ushangae

Halafu kitu kingine nilishawahi kunote na kusema humu. Tanzania ni kama hatuna architecture binafsi. Majengo yoote karibia tunajenga mjengo wa aina moja tofauti yetu ni ukubwa wa vyumba tu

Watu hawaji na idea mpya za majengo zaidi ya Yale Yale na mapaa Yale Yale sijui wenye hela za kujenga kwanini mmejificha kwenye kaboksi

Ngoja mie nijikusanye nijenge niache mdomo kusema ya watu😂😂
 
Hii tumei discuss sana na mwanang mmoja hivi, ni kweli haina maana zaidi ya show tuuu, dirisha linatumika nusu
Tatizo wabongo tunskurupukia mambo,hizo dirisha za aluminum ni lazima iwe kubwa minimum futi 5*5 sasa mtu hata futi 4 anaona kubwa eti anakwepa gharama.

Design ya hayo madirisha yanataka hivyo, pili zile vents za juu ziwe wazi hata ukilala ucku
 
Vitu viko on point mno.Mafundi sasa hapo uende akutengenezee hivyo atakutolea kitu cha ajabu mpaka ushangae

Halafu kitu kingine nilishawahi kunote na kusema humu. Tanzania ni kama hatuna architecture binafsi. Majengo yoote karibia tunajenga mjengo wa aina moja tofauti yetu ni ukubwa wa vyumba tu

Watu hawaji na idea mpya za majengo zaidi ya Yale Yale na mapaa Yale Yale sijui wenye hela za kujenga kwann mmejificha kwenye kaboksi

Ngoja mie nijikusanye nijenge niache mdomo kusema ya watu😂😂
Wabunifu wapo tatizo ni ushamba na kuona eti kulipia ramani ni ghali wanachukua ya fundi Michael, kingine ni uoga wa gharama kwa vitu vipya.

Matokeo yake nyumba zote mtaani zinafanana tofauti ni ukubwa na rangi za mabati, mtaani kuna nyumba za ajabu Sana.
 
Wabunifu wapo tatizo ni ushamba na kuona eti kulipia ramani ni ghali wanachukua ya fundi Michael, kingine ni uoga wa gharama kwa vitu vipya.

Matokeo yake nyumba zote mtaani zinafanana tofauti ni ukubwa na rangi za mabati, mtaani kuna nyumba za ajabu Sana.
Yaaani mimi hata huwa sielewi mtu anaposema kajenga nyumba Kali nikija kuiona naona ile ile tu kama lodge tunazolala na nyumba nyingine.

Hakuna uniqueness katika architecture ya bongo kabisa.
 
Binafsi si shabiki wa madirisha yanayotamba siku hizi, aluminiamu na pvc. Sababu kubwa ni kutokuwa na uimara wa kutosha na pia hata yakifunguliwa yanachukua sehemu kubwa ya dirisha na hivyo kuzuia hewa.

Hii ni mbaya zaidi kwa mimi wa sehemu ya joto. Madirisha haya yakifungwa, huko ndani mtajuta kuishi ndani hilo jengo. Kwani madirisha mengine ya kisasa ni yepi tukiacha yale ya tulipotoka?

Ndiyo tumekwama hapo?

Wabunifu mpo wapi?
Ulipaswa wewe ndio utupe mbadala badala ya kuwatupia wengine mzigo.
 
Kuingiza mbu kwenye madirisha ya aluminium ni tatizo la fundi wako.
 
Tatizo wabongo tunskurupukia mambo,hizo dirisha za aluminum ni lazima iwe kubwa minimum futi 5*5 sasa mtu hata futi 4 anaona kubwa eti anakwepa gharama.

Design ya hayo madirisha yanataka hivyo,pili zile vents za Juu ziwe wazi hata ukilala ucku
Ehee! Kuna kitu wajengaji wa siku hizi wanakisahau.

Siku hizi nimeona hawaweki venti. Nilimuuliza jamaa yangu mmoja kwa nini hajaweka venti, akasema ni ushamba!

Jamani, venti ni muhimu ili hewa iingie ukifunga hilo dirisha la alluminium. Ukiliacha wazi usiku, vibaka wanatamani kuja kujaribu bahati yao.

Venti zirudi jamani, tena zile zinazoonesha mwaka zilikuwa poa kweli!

Unaweka frame na wavu kwenye venti safii!
 
Asante sana. Haya ni mazuri mno. Kwa mimi, aluminium haziingii hapa hata kwa 1/4. Swali ni , wavu wa mbu unakaa wapi hapo?
Ukipata fundi mzuri anakutengenezea inakuwa na double shutter, ndani kunakuwa na shutter za wavu halafu nje zinakuwa hizo.. Hapo mbu utawasikia kwa jirani.
 
kati kati ya zile sliders mbili za vioo kuna upenyo mdogo, kwa mbu ni hallway ya mita 500

ikifika saa 12 jioni inabidi ufunge, yawe sealed shut, la sivyo utalia, ndani panakua nje, bora hata nje

ukifunga jiandae na 'suffocation' ya kutosha , ikifika saa 3 usiku uyafungue tena, ukisahau ukalala

iyoivyo bila 'AC' kuwa ON ( sio feni )

kesho asubuhi jiandae na 'kizunguzungu'[/]


faida moja kubwa ya dirisha la alminium au kioo ni kuzuia vumbi ndan na moshi maana huku uswahili mtu kujichomea nyasi au takataka kawaida sasa bila madirisha hayo moshi wote utajaa ndan

swala la mbu basi kama kuna dirisha uliona liko hivyo litakuwa liliwekwa vibaya au ni cheap quality maana yanatofautiana ubora jinsi ya kuwekwa

hakuna namna mbu anaingi na ukiacha waz kuna nyavu za kuzuia mbu, maana hayo madirisha kwenye huo uwaz kuna raba flan inawekwa..ya kuzuia wadudu wa kutambaa na hata mbu hiyo rubber inakuwa inagusa kwenye kioo ukifunga au kufungua

mie natumia na wakati wa usiku nayafunga yote na situmii fan wala hakuna suffocation .. joto la dar hata uweke wavu mtupu kipind cha joto utaitafuta fan.. tumezaliwa na kukulia kwenye madirisha ya wavu na bado joto lilitukomesha

kama ni kiangaz na hakuna upepo jua lote la
mchana limechoma aridhi na kuta za nyumba usiku hakuwez kuacha kuwa na joto
 
Ukipata fundi mzuri anakutengenezea inakua na double shutter, ndani kunakua na shutter za wavu alafu nje zinakua hizo.. Hapo mbu utawasikia kwa jirani.
Hili ndio suluhisho. Kuna Nyumba niliwahi kuona hii kitu. Wameweka na wavu wa kuslide kwa ndani ya dirisha
 
Back
Top Bottom