Kwani Rais Magufuli alitoa ratiba ya kuwapeleka mafisadi mahakamani?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,001
112,619
Nazungumzia ratiba ya kuwapeleka mafisadi kwenye mahakama ya mafisadi na kuwafungulia mashitaka. Inawezekana labda aliwahi kuitoa au kuitaja hiyo ratiba lakini mimi ama sikuiona au sikuisikia.

Hivyo, ndo maana nauliza hapa. Kama kuna anayejua nitamshukuru akitufahamisha sie tusiojua. Aliwahi kuahidi kuwa fulani na fulani atawapeleka kwenye hiyo mahakama na atawapeleka lini?

Kikubwa kilichonifanya niulize ni kile kilichotokea jana kwa wale watu wawili [Harbinder Sing na James Rugemalira] kukamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao.

Inavyoelekea watu walio wengi hawakuwa wakitegemea kuwa hao jamaa wangekamatwa hiyo jana. Na ndo maana kitendo cha wao kukamatwa kimepokelewa kwa mshangao, furaha, na wasiwasi.

Sasa, kuna wale ambao wanahoji kuwa kama Lowassa ni fisadi kwa nini hapandishwi kizimbani. Ndo nami swali linalonijia ni hilo kwenye kichwa cha mada.

Sijui labda watu walitaka kumwona yeye akiwa wa kwanza kupandishwa kizimbani kujibu hizo tuhuma dhidi yake au sijui wanataka kuona kila siku kuna mtu mpya anapandishwa kizimbani!

Muhula wa huyu Ngosha ni bado sana kuisha. Bado ana zaidi ya miaka miwili ndipo amalize muhula wake wa kwanza.

Tayari keshaonyesha kuwa ni mtu ambaye hatabiriki kirahisi wakati mwingine. Hivyo msije shangaa siku moja mnaamka na kumwona [Lowassa] akiwa 'perp walked' nje ya mahakama ya Kisutu.

Hapo naweza hata kutabiri kuwa wengi wenu mnaohoji kwa nini kama yeye ni fisadi hapandishwi kizimbani, mtabadili magoli na si ajabu mkasema kuwa anaonewa kwa sababu za kisiasa.

Vita dhidi ya ufisadi ni vita ndefu na ni endelevu. Mnapokuwa vitani kamanda hawezi ku-telegraph mipango na matendo yake kwani kufanya hivyo kunaweza kumnufaisha adui na akajipanga vizuri ili akushinde.

Siku ya siku ikifika msije kusema sikuwaambia....na msije kulia na kuhamisha magoli hapa!
 
Nazungumzia ratiba ya kuwapeleka mafisadi kwenye mahakama ya mafisadi na kuwafungulia mashitaka.

Inawezekana labda aliwahi kuitoa au kuitaja hiyo ratiba lakini mimi ama sikuiona au sikuisikia.

Hivyo, ndo maana nauliza hapa. Kama kuna anayejua nitamshukuru akitufahamisha sie tusiojua.

Aliwahi kuahidi kuwa fulani na fulani atawapeleka kwenye hiyo mahakama na atawapeleka lini?

Kikubwa kilichonifanya niulize ni kile kilichotokea jana kwa wale watu wawili [Harbinder Sing na James Rugemalira] kukamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yao.

Inavyoelekea watu walio wengi hawakuwa wakitegemea kuwa hao jamaa wangekamatwa hiyo jana.

Na ndo maana kitendo cha wao kukamatwa kimepokelewa kwa mshangao, furaha, na wasiwasi.

Sasa, kuna wale ambao wanahoji kuwa kama Lowassa ni fisadi kwa nini hapandishwi kizimbani.

Ndo nami swali linalonijia ni hilo kwenye kichwa cha mada.

Sijui labda watu walitaka kumwona yeye akiwa wa kwanza kupandishwa kizimbani kujibu hizo tuhuma dhidi yake au sijui wanataka kuona kila siku kuna mtu mpya anapandishwa kizimbani!

Muhula wa huyu Ngosha ni bado sana kuisha. Bado ana zaidi ya miaka miwili ndipo amalize muhula wake wa kwanza.

Tayari keshaonyesha kuwa ni mtu ambaye hatabiriki kirahisi wakati mwingine. Hivyo msije shangaa siku moja mnaamka na kumwona [Lowassa] akiwa 'perp walked' nje ya mahakama ya Kisutu.

Hapo naweza hata kutabiri kuwa wengi wenu mnaohoji kwa nini kama yeye ni fisadi hapandishwi kizimbani, mtabadili magoli na si ajabu mkasema kuwa anaonewa kwa sababu za kisiasa.

Vita dhidi ya ufisadi ni vita ndefu na ni endelevu. Mnapokuwa vitani kamanda hawezi ku-telegraph mipango na matendo yake kwani kufanya hivyo kunaweza kumnufaisha adui na akajipanga vizuri ili akushinde.

Siku ya siku ikifika msije kusema sikuwaambia....na msije kulia na kuhamisha magoli hapa!

Kweli Magu hatabirikj,sitoshangaa na yeye akipandishwa kizimbani kwa kuuza nyumba za serikali,kununua meli mbovu na kuliingiza taifa hasara.
Tusubiri tutaona na kusikia mengi.
 
Kweli Magu hatabirikj,sitoshangaa na yeye akipandishwa kizimbani kwa kuuza nyumba za serikali,kununua meli mbovu na kuliingiza taifa hasara.
Tusubiri tutaona na kusikia mengi.
HIYO TRACK YENU YA NYUMBA ZA SERIKALI HAIICHUJI TU KWENU , NADHANI MAPAKA SASA UNGEKUA USHAITOA KAMA UNGEKUA UMEMSIKILIZA MWENYEKITI WENU WA CHAMA KANDA YA PWANI ALISHALIELEZA HILO VIZURI TU, AU MWENZETU KIZIWI
 
Ushabiki uchwara in the making....

Magufuli yupo smart kuliko mnaoimuimbia mapambio....
Hivi kipindi upinzani unaimba kuwa hizo pesa za Escrow ni za umma mlikuwa upande upi?
Deo filikunjombe alikuwa ni wa chama gani?
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom