Kwani ni lazima utangaze kafa kwa ukimwi?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
Anakufa mtu unayemjua tangu akiwa mzima wa afya hadi alipougua na kufariki. Kabla hujajua amekufa kwa maradhi gani, unaanza kupita ukinong'ona kwamba, amekufa kwa Ukimwi.

Inawezekana ni kweli amekufa kwa ukimwi, lakini hata kama ni hivyo, ni lazima upite ukitangaza kila mahali?

Je itakupa ahueni gani?

Lakini, hivi ikitokea na wewe unafiwa, halafu anatokea mtu au watu wanapita wakitangaza kuwa huyo mtu wako amekufa kwa Ukimwi utajisikiaje? Bila shaka utajisikia vibaya, utaumia na kukereka..... Ni ujinga eh! Ndio ni ujinga kwa sababu umesahau kuwa jana na juzi ulitenda hivyo kwa mwingine.......
 
Si vizuri, lakini si vizuri pia kuficha mfano kama ni taarifa
kwenye Media husikii mtu kafa kwa ukimwi utasikia tu
baada ya kuugua muda mrefu, mi naona ukimwi ni
ugonjwa wa kawaida kama kisukari huku ukiwa chini ya
kansa lakini umefanywa uonekane unatisha kuliko hata
hiyo kansa!
 
Sio Vibaya ikiwa ameacha makoloni ambayo yatakuwa ni hatari kwa wengine, hivyo inatufanya wengine tuwe makini na wetu ambao amewapitia. Halafu inatukumbusha kuwa kweli ngoma ipo na inaua kikweli.
 
Si vizuri, lakini si vizuri pia kuficha mfano kama ni taarifa
kwenye Media husikii mtu kafa kwa ukimwi utasikia tu
baada ya kuugua muda mrefu, mi naona ukimwi ni
ugonjwa wa kawaida kama kisukari huku ukiwa chini ya
kansa lakini umefanywa uonekane unatisha kuliko hata
hiyo kansa!
Ultimately kinachouwa huwa sio ukimwi bali magonjwa ya kawaida. Kwa hiyo mtu mwenye AIDS atakufa kwa kisukari, malaria etc kama wanavyokufa watu wasio na AIDS kutokana na magonjwa hayohayo. So kama mtu ameumwa malaria na kwa bahati mbaya ikamwondoa kutangaza HIV status yake ni irrelevant and i also believe its useless!
 
ukweli utabaki palepale, ukwimwi ni ugonjwa kama ugonjwa mwengine. na hamna haja ya kuficha ukweli kuwa mgonjwa wako alikufa kwa ukimwi.
 
Tatizo ni sisi wabongo tunachukulia kama m2 akifa na ukimwi ndo alikuwa malaya hajatulia
kumbe unaweza ukawa umetulia na ukaded nao
tusinyosheane vidole hata kidogo,cz ukienda ambako zinachukuliwa dawa za kurefusha maisha
mwenyewe akili itakukaa sawa na kujifikria je mm nimepona kweli au k2 bado hakijaanza kjitokeza
sababu inatisha jamani.....tena huyo anaetangaza akae kimya HALI NI MBAYA JAMANI.
 
Mie nadhani sio kutangaza ni mtu tu kuongea ukweli, na hii yote imetokana na watu kuficha ficha maradhi ndio maana watu nao wanahisi, kwa nn tu isitangazwe kwenye msiba kama kansa au kisukari?
 
ufe na ngiri, kisukari, ukimwi, ugongwe na benzi, wooote mnakuwa hamna thamani, ni wa kuzikwa tu.
Mpe Yesu maisha yako, maana hazina yako ilipo ndipo moyo wako itakapo kuwepo
 
ufe na ngiri, kisukari, ukimwi, ugongwe na benzi, wooote mnakuwa hamna thamani, ni wa kuzikwa tu.
Mpe Yesu maisha yako, maana hazina yako ilipo ndipo moyo wako itakapo kuwepo

Sikujua kama siku hizi umeokoka......................
 
Tatizo ni sisi wabongo tunachukulia kama m2 akifa na ukimwi ndo alikuwa malaya hajatulia
kumbe unaweza ukawa umetulia na ukaded nao
tusinyosheane vidole hata kidogo,cz ukienda ambako zinachukuliwa dawa za kurefusha maisha
mwenyewe akili itakukaa sawa na kujifikria je mm nimepona kweli au k2 bado hakijaanza kjitokeza
sababu inatisha jamani.....tena huyo anaetangaza akae kimya HALI NI MBAYA JAMANI.

Ni kweli mkuu, mimi nilimpeleka wife Kliniki pale Tabata Hospitali, sasa upande wa pili wa hiyo kliniki kuna jengo ambalo sikujua ndipo wanapochukulia dawa za kurefusha maisha. kwa kuwa kulikuwa na TV, nikaona nikae hapo nifuatilie bunge. kulikuwa na akina dada wengi tu wa kutosha na akina kaka pia..........alikuwepo binti mmoja mrembo hivi akawa ananisemesha, tulijikuta tukiwa marafiki ghafla na tulizungumza mambo mengi tu ya kawaida........ baada ya wife kutoka, tukaondoka zetu........... wiki kadhaa nikakutana na yule binti, baada ya kusalimiana akanidadisi kuwa mbona hanioni tena kule kwenye kitengo, na alitaka kujua kama nimebadilii kituo cha kuchukulia dawa au nilienda kwa babu Loliondo......... nilishangaa kidogo, lakini baada ya kumdadisi kidogo kuwa ana maana gani ndipo nikagundua kuwa alidhani na mie ni muathirika na pale nilikwenda kuchukua dawa kama yeye.................. Duh! nilishangaa kidogo, ndipo nilipomueleza kuwa mimi sio muathirika bali nilimsindikiza wife kliniki na wote tumeshapima na tuko salama...........alijisikia aibu kidogo, lakini nilimshauri aishi kwa matumaini na ajitunze, kwani kwa jinsi anavyoonekana mrembo ,anaweza kuingia vishawishi na kueneza maradhi hayo........ alinishukuru na tukaachana, kwa hiyo nakubaliana na wewe, kwa kweli huwezi kujua ni yupi yuko salama na ni yupi ni mgonjwa..................
 
Anakufa mtu unayemjua tangu akiwa mzima wa afya hadi alipougua na kufariki. Kabla hujajua amekufa kwa maradhi gani, unaanza kupita ukinong'ona kwamba, amekufa kwa Ukimwi.

Inawezekana ni kweli amekufa kwa ukimwi, lakini hata kama ni hivyo, ni lazima upite ukitangaza kila mahali?

Je itakupa ahueni gani?

Lakini, hivi ikitokea na wewe unafiwa, halafu anatokea mtu au watu wanapita wakitangaza kuwa huyo mtu wako amekufa kwa Ukimwi utajisikiaje? Bila shaka utajisikia vibaya, utaumia na kukereka..... Ni ujinga eh! Ndio ni ujinga kwa sababu umesahau kuwa jana na juzi ulitenda hivyo kwa mwingine.......

UKIMWI ni upungufu wa kinga mwilini kitu ambacho kinapelekea magonjwa mengine kuvamia mwili na baadaye mtu kufa. Hivyo cheti cha kifo uonesha kuwa mtu amefariki labda kwa TB au malaria kali kutokana na kupungukiwa kinga. Lakini kusema kuwa marehemu alikuwa na ukimwi na kufariki kwa sababu ya malaria kali ni jambo jema kabisa ili wengine wasijaribu kuoa au kuolewa na mwezi aliyebaki, na nyumba ndogo au serengeti boys wajiandae na safari.

Kwa kifupi huyo jamaa anayetangaza kuwa ndugu yako kafa kwa ukimwi ni sahihi kabisa. Inakusumbua wewe kwa sababu ukimwi ni gonjwa la aibu kwani asilimia kubwa ni kuptia ngono.
 
Yaani wewe Mtambuzi unafanya nione TACAIDS na wenzao bado wanakazi, hiyo post yako inaonyesha unyanyapaa tosha, kama tunaambiwa UKIMWI ni ugonjwa kama magonjwa mengine tatizo liko wapi mtu akiambiwa kafa kwa UKIMWI hasa ikiwa ni ukweli, mbona akifa na malaria tunasema, akifa na uti wa mgongo tunasema akifa kwa kansa. Labda useme tuache kusema mtu kafa kwa nini. Fikra kama zako ndio zinazofanya suala la unyanyapaa kutokuisha kabisa na watu kuogopa kujiweka wazi na kuongeza tatizo.

 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom