kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Magulumangu

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
3,047
452
Kwa hadhi na taadhima,kwangu wewe malaika,
Nilipopatwa hujuma,moyo wangu sisimka,
Ya kwanza yetu miama,yako sikuwa hulka,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Nilikuwa mkimbizi, yangu mapenzi moyoni,
Kuvizia kama nzi,kinyesi kwao machoni,
Cheupe kama la nazi,tui lifikapo mbogani,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Sikuivunja safari, siku liposema nkome,
Ilikuwa kama sukari,kwa nyuki ndani kikome,
Nyingine kanza safari,wako wazazi ni ngome,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Hukuona usumbufu, wao kukupa ulinzi,
Ndugu wazazi ubunifu, kwako wote walisizi,
Ukanona yakinifu,si fisadi wa azizi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Moyo uliufungua, mkimbizi kimapenzi,
Limzigo ukanitua, ukasema utalienzi,
Na sasa ninapumua,sina doa kimapenzi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Nilitega tendawili, ndani yangu moyoni,
Miji mingi si miwili,zawadi hadi manyoni,
Nakumbuka hadi pili,kisa eti maskini,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Moyo wangu upo kwako, wewe wake mhifadhi,
Kihalali jipe jiko,kwako yangu ni hifadhi,
Twenzetu hata moroko,ya kizanziba mahadhi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Sina budi kujisifu, lile lako tabasamu,
mwendo wako yakinifu,kama twiga muasimu,
shingo lako malikifu,haleluya kwa karimu,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,

Sio kana sina vina, kichwani wewe mrembo,
usokuwa na kifana,la mgema sio tembo,
njo kwetu pale banana,ya maisha yetu nembo,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
 
Code:
Mashairi nayo kha!!..

DA nimekukosea au? jamani was just my feelings tu kama inakuboa jamani ukimya unakuwa mzuri sana...pole kama yamekuudhi DA sikuwa na nia mbaya na sitegemei uumizwe na feelings zangu....
 
Yes he is back..
Kwa poem nakuheshimu. .

sio kwamba nimerudi, bali yangu imerudi,
sikutumwa kama radi, bali ni yake miadi,
Muulize hata hamadi,sifiki kwake ramadi,
Asante yako heshima, hata wewe lipotea,

Jamani nilikumisi,mithili yake amali,
hata dena amusi,kuponda ya si asili,
tafuta zote kamusi,kithungu na kiswahili,
Asante yako heshima,hata wewe lipotea,

Salamu zangu mahili,mpitishie Osama,
kule aliko kalili,uanzie na Obama,
wala hakuna dalili,mpokee wetu Rahima,
Asante yako heshima,hata wewe lipotea,
 
kuna wanawake wana bahati sana.hongera yake...


strawberry kulamba, avata ya king'asti,
muumbe wetu rahuba,kama za nuhu nyakati,
hata wewe kakuumba,kwa ufundi ha mikakati,
wanawake wenye bahati, wewe ni wao mmoja,

kioo hakikosei, ukiwa mbele jamani,
moyo pia hukusei, akwambiapo mwandani,
msikilize baridei, hata muwapo kigamboni,
wanawake wenye bahati,hata wewe ni wao mmoja,

mwandani sipo sifia, njiani wanalopoka,
wengine hukimbilia,miluzi ya fokafoka,
kwa nyuma ukijazia,namba nane inaita,
wanawake wenye bahati,hata wewe ni wao mmoja,

naomba kura ya ndiyo, nipate wangu uwanja,
mwambieni hata kihiyo,chakachua siwe tija,
aliimba hata Kidjo,agolo yake misija,
wanawake wenye bahati,hata wewe ni wao mmoja,
 
sio kwamba nimerudi, bali yangu imerudi,
sikutumwa kama radi, bali ni yake miadi,
Muulize hata hamadi,sifiki kwake ramadi,
Asante yako heshima, hata wewe lipotea,

Jamani nilikumisi,mithili yake amali,
hata dena amusi,kuponda ya si asili,
tafuta zote kamusi,kithungu na kiswahili,
Asante yako heshima,hata wewe lipotea,

Salamu zangu mahili,mpitishie Osama,
kule aliko kalili,uanzie na Obama,
wala hakuna dalili,mpokee wetu Rahima,
Asante yako heshima,hata wewe lipotea,

mmmmmhhh
kweli kofia nakuvulia ,
kwa mashairi umebarikiwa
heshima busara yako pia..
Kwa Mungu nakuombea ..
Azidi kukuongezea...
 
mmmmmhhh
kweli kofia nakuvulia ,
kwa mashairi umebarikiwa
heshima busara yako pia..
Kwa Mungu nakuombea ..
Azidi kukuongezea...


nambie mtu wangu,
namtafuta hapa judith
ila nasikia anatangaza ndoa,
sasa sijui itakuwaje,
au mambo ya Beijing hayo?
 
Huyajui ya mbele, usiape ya milele,
Wa kike kama upele, utajikuna upige kelele,
Uwele si mchele, shida na tabu ni kilele,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Kuna tofauti malezi, familia imempatia,
Kuna kama walevi, bila sababu hulia,
Pia kuna wezi, mfukoni kucha hupitia,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Wengine wana dharau, tena si wakarimu,
Naomba msinihukumu, tatizo ni baadhi yenu,
Kwa dhati nawaheshimu, nyie viumbe adhimu
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Magulumangu unaweza, vina vimekamilika,
Kwenye mizani umecheza, kama messi unaweza,
Mji nakupa Muheza, kwenye mnazi nakukweza,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua
 
nambie mtu wangu,
namtafuta hapa judith
ila nasikia anatangaza ndoa,
sasa sijui itakuwaje,
au mambo ya Beijing hayo?

hahahah JUdith yupo
Nilimuona jana maeneo
ya kwenye siasa kule
Soshi ndo anakuja na kuondoka
hakai sana humu ndani siku hizi
we mzima kabisa lakini??
 
Code:

DA nimekukosea au? jamani was just my feelings tu kama inakuboa jamani ukimya unakuwa mzuri sana...pole kama yamekuudhi DA sikuwa na nia mbaya na sitegemei uumizwe na feelings zangu....

Pole bana usingizi ulikuwa unasumbua.......pole
 
Huyajui ya mbele, usiape ya milele,
Wa kike kama upele, utajikuna upige kelele,
Uwele si mchele, shida na tabu ni kilele,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Kuna tofauti malezi, familia imempatia,
Kuna kama walevi, bila sababu hulia,
Pia kuna wezi, mfukoni kucha hupitia,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Wengine wana dharau, tena si wakarimu,
Naomba msinihukumu, tatizo ni baadhi yenu,
Kwa dhati nawaheshimu, nyie viumbe adhimu
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Magulumangu unaweza, vina vimekamilika,
Kwenye mizani umecheza, kama messi unaweza,
Mji nakupa Muheza, kwenye mnazi nakukweza,
Ya mbele ni kiza, katu huwezi jua

Mti ulioutua,nadhani upo urimbo,
Fanya uje tutumua,asijekuwa mrembo,
wa kike hatosumbua,iwapo huna uringo,
Niliyaona ya mbele,kioo yeye mrembo,

Tofauti ni malezi,hilo nakupa hakika,
Hata kunguru wa mbezi,hafai ye kufugika,
Wale ulotaja wezi,ukahaba huupika,
Niliyaona ya mbele,kioo yeye mrembo,

Wewe unawaheshimu,hilo mkono nanyosha,
Wao viumbe adhimu,ndo mama yetu maisha,
kamwe huna hukumu,mfano lulu na isha,
Niliyaona ya mbele,kioo yeye mrembo,

Mesi namfagilia,drogba naye ayaweza,
Ngondya mwana aslia,nilishapita muheza,
minazi napalilia,muulize hata mbiza,
Niliyaona ya mbele,kioo yeye mrembo,
 
hahahah JUdith yupo
Nilimuona jana maeneo
ya kwenye siasa kule
Soshi ndo anakuja na kuondoka
hakai sana humu ndani siku hizi
we mzima kabisa lakini??


Nilipitia mitaa ya SIASA duh kina Nnauye wakanitoa eti mi Magamba,
Soshi yeye sijui inakuwaje anakuja na kupotea,
anyway hata mie nipo nipo tu si unajua tena umalenga si lele mama..
Nilikuwa pale DC jana kuonyesha kuwaunga mkono Marekani kwa kumnasa Osama nikitokea Itale pale kumu beatificate Pope II nikiwa na Robert mwana wa Mugabe....
 
wapi babu?? aje aweke shairi la bibi
magulumangu big up sana

hii ni zawadi yako
kwa hiyo tungo yako
mungu ajibu hitaji lako
azidishe maradufu furaha yako.
 
wapi babu?? aje aweke shairi la bibi
magulumangu big up sana

hii ni zawadi yako
kwa hiyo tungo yako
mungu ajibu hitaji lako
azidishe maradufu furaha yako.

Babu bado yu na bibi,wafurahia maisha,
wameenzi kama zinabi,mapenzi yao toisha,
babu asiye kitambi,mazoezi kwake toisha,
Asante mwana birungi,karibu umalengani,

mungu baba hujibu,kila mwenye kuhitaji,
mwenye dhambi pata jibu,bila hata nidi taji,
weusi hata warabu,kwake yeye si miraji,
Asante mwana birungi,karibu umalengani,
 
Back
Top Bottom