Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
Kwa hadhi na taadhima,kwangu wewe malaika,
Nilipopatwa hujuma,moyo wangu sisimka,
Ya kwanza yetu miama,yako sikuwa hulka,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Nilikuwa mkimbizi, yangu mapenzi moyoni,
Kuvizia kama nzi,kinyesi kwao machoni,
Cheupe kama la nazi,tui lifikapo mbogani,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sikuivunja safari, siku liposema nkome,
Ilikuwa kama sukari,kwa nyuki ndani kikome,
Nyingine kanza safari,wako wazazi ni ngome,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Hukuona usumbufu, wao kukupa ulinzi,
Ndugu wazazi ubunifu, kwako wote walisizi,
Ukanona yakinifu,si fisadi wa azizi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Moyo uliufungua, mkimbizi kimapenzi,
Limzigo ukanitua, ukasema utalienzi,
Na sasa ninapumua,sina doa kimapenzi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Nilitega tendawili, ndani yangu moyoni,
Miji mingi si miwili,zawadi hadi manyoni,
Nakumbuka hadi pili,kisa eti maskini,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Moyo wangu upo kwako, wewe wake mhifadhi,
Kihalali jipe jiko,kwako yangu ni hifadhi,
Twenzetu hata moroko,ya kizanziba mahadhi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sina budi kujisifu, lile lako tabasamu,
mwendo wako yakinifu,kama twiga muasimu,
shingo lako malikifu,haleluya kwa karimu,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sio kana sina vina, kichwani wewe mrembo,
usokuwa na kifana,la mgema sio tembo,
njo kwetu pale banana,ya maisha yetu nembo,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Nilipopatwa hujuma,moyo wangu sisimka,
Ya kwanza yetu miama,yako sikuwa hulka,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Nilikuwa mkimbizi, yangu mapenzi moyoni,
Kuvizia kama nzi,kinyesi kwao machoni,
Cheupe kama la nazi,tui lifikapo mbogani,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sikuivunja safari, siku liposema nkome,
Ilikuwa kama sukari,kwa nyuki ndani kikome,
Nyingine kanza safari,wako wazazi ni ngome,
kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Hukuona usumbufu, wao kukupa ulinzi,
Ndugu wazazi ubunifu, kwako wote walisizi,
Ukanona yakinifu,si fisadi wa azizi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Moyo uliufungua, mkimbizi kimapenzi,
Limzigo ukanitua, ukasema utalienzi,
Na sasa ninapumua,sina doa kimapenzi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Nilitega tendawili, ndani yangu moyoni,
Miji mingi si miwili,zawadi hadi manyoni,
Nakumbuka hadi pili,kisa eti maskini,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Moyo wangu upo kwako, wewe wake mhifadhi,
Kihalali jipe jiko,kwako yangu ni hifadhi,
Twenzetu hata moroko,ya kizanziba mahadhi,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sina budi kujisifu, lile lako tabasamu,
mwendo wako yakinifu,kama twiga muasimu,
shingo lako malikifu,haleluya kwa karimu,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,
Sio kana sina vina, kichwani wewe mrembo,
usokuwa na kifana,la mgema sio tembo,
njo kwetu pale banana,ya maisha yetu nembo,
Kwako yangu ni hifadhi, ya milele si ya muda,